约伯记 42 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

约伯记 42:1-17

1约伯回答耶和华说:

2“我知道你无所不能,

你的旨意无不成就。

3你问,‘谁用无知的话使我的旨意晦暗不明?’

诚然,我对自己所谈论的事一无所知,

这些事太奇妙,我无法明白。

4你说,‘你且听着,我要发言。

我来提问,你来回答。’

5我从前风闻有你,

现在亲眼看见你。

6因此我厌恶自己,

在尘土和炉灰中忏悔。”

结语

7耶和华对约伯说完这些话后,就对提幔以利法说:“你和你的两个朋友令我愤怒,因为你们对我的议论不如我仆人约伯说的有理。 8现在你们要取七头公牛和七只公羊,到我仆人约伯那里,为自己献上燔祭,因为你们对我的议论不如我仆人约伯说的有理。我仆人约伯会为你们祷告,我会悦纳他的祷告,不按你们的愚妄惩罚你们。” 9于是,提幔以利法书亚比勒达拿玛琐法遵命而行,耶和华悦纳了约伯的祷告。

10约伯为朋友们祷告后,耶和华恢复了他以前的昌盛,并且耶和华赐给他的比以前多一倍。 11约伯的兄弟姊妹和从前的朋友都来探望他,在他家里一同吃饭,为他遭受耶和华所降的种种灾难而安抚、慰问他。他们每人送他一块银子和一个金环。

12耶和华赐给约伯晚年的福分比起初更多:他有一万四千只羊、六千只骆驼、一千对牛和一千头母驴。 13他还有七个儿子和三个女儿。 14他给长女取名叫耶米玛、次女叫基洗亚、三女叫基连·哈朴15那地方找不到像约伯三个女儿那样美丽的女子。约伯让她们与弟兄一同承受产业。 16此后,约伯又活了一百四十年,得见四代子孙。 17约伯年纪老迈,寿终正寝。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 42:1-17

Sehemu Ya Tano

(Ayubu 42)

Ayubu Anamjibu Bwana

1Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:

242:2 Mwa 18:14; Yer 32:17; Mt 19:26; 2Nya 20:6; Efe 1:11“Ninajua ya kuwa unaweza kufanya mambo yote,

wala hakuna mpango wako unaoweza kuzuilika.

342:3 Ay 34:35; 38:2; Za 40:5Uliuliza, ‘Ni nani huyu afichaye mashauri yangu bila maarifa?’

Hakika nilisema juu ya mambo niliyokuwa siyaelewi,

mambo ya ajabu mno kwangu mimi kuyajua.

442:4 Ay 38:3; 40:7“Ulisema, ‘Sikiliza sasa, nami nitanena;

nitakuuliza swali, nawe yakupasa kunijibu.’

542:5 Ay 26:14; Rum 10:17; Amu 13:22; Mt 5:8Masikio yangu yalikuwa yamesikia habari zako,

lakini sasa macho yangu yamekuona.

642:6 Eze 6:9; Rum 12:3; Kut 10:3; Ezr 9:6Kwa hiyo najidharau mwenyewe,

na kutubu katika mavumbi na majivu.”

Mwisho: Marafiki Wa Ayubu Wanafedheheshwa

742:7 Yos 1:7; Ay 32:3, 8; 9:15Baada ya Bwana kusema mambo haya yote na Ayubu, akamwambia Elifazi Mtemani, “Nina hasira juu yako na juu ya rafiki zako wawili, kwa sababu hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu. 842:8 Hes 23:29; Eze 45:23; Mwa 20:17; Yak 5:15-17; Ay 22:30Basi sasa chukueni mafahali saba na kondoo dume saba mkamwendee mtumishi wangu Ayubu nanyi mkatoe sadaka za kuteketezwa kwa ajili yenu wenyewe. Mtumishi wangu Ayubu ataomba kwa ajili yenu, nami nitayakubali maombi yake ili nisiwatendee sawasawa na upumbavu wenu. Ninyi hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.” 942:9 Ay 2:11; Mwa 19:21; 20:17; Eze 14:14Kwa hiyo Elifazi Mtemani, Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi wakafanya kama Bwana alivyowaambia; naye Bwana akayakubali maombi ya Ayubu.

1042:10 Kum 30:3; Za 14:7; 126:5-6; Yak 5:11Baada ya Ayubu kuwaombea rafiki zake, Bwana akamwondoa kwenye uteka, akamfanikisha tena naye akampa mara mbili ya vile alivyokuwa navyo hapo mwanzoni. 1142:11 Ay 19:13Ndipo ndugu zake wote waume kwa wake na kila mtu aliyemfahamu mwanzoni, wakaja wakala pamoja naye katika nyumba yake. Wakamfariji na kumtuliza moyo juu ya taabu yote Bwana aliyoileta juu yake, nao kila mmoja akampa kipande cha fedha na pete ya dhahabu.

1242:12 Yak 5:11Bwana akaibariki sehemu ya mwisho ya maisha ya Ayubu kuliko ile ya kwanza. Alikuwa na kondoo elfu kumi na nne, ngamia elfu sita, jozi za mafahali elfu moja, na punda wa kike elfu moja. 13Tena alikuwa na wana saba na binti watatu. 14Binti wa kwanza aliitwa Yemima, wa pili Kesia na wa tatu Keren-Hapuki. 15Hapakuwepo mahali popote katika nchi ile yote palipopatikana wanawake wazuri kama binti za Ayubu; naye baba yao akawapa urithi pamoja na ndugu zao.

16Baada ya hili Ayubu akaishi miaka 140; akawaona wanawe na wana wa wanawe hata kizazi cha nne. 1742:17 Mwa 15:15; 25:8Hivyo Ayubu akafa, akiwa mzee aliyekuwa ameshiba siku.