约伯记 39 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

约伯记 39:1-30

1“你知道野山羊何时生产吗?

你看过母鹿产仔吗?

2你能算出它们怀胎的月数吗?

你知道它们分娩的日期吗?

3它们几时屈身产仔,

结束分娩之痛?

4幼仔健壮,在荒野长大,

离群而去,不再回来。

5“谁让野驴逍遥自在?

谁解开了它的缰绳?

6我使它以旷野为家,

以盐地作居所。

7它嗤笑城邑的喧闹,

不听赶牲口的吆喝。

8它以群山作草场,

寻找青翠之物。

9“野牛岂肯为你效劳,

在你的槽旁过夜?

10你岂能用缰绳把野牛牵到犁沟?

它岂肯跟着你在山谷耕地?

11你岂能倚靠它的大力,

把你的重活交给它?

12岂能靠它运回粮食,

替你堆聚到麦场?

13“鸵鸟欢然拍动翅膀,

它岂有白鹳的翎羽?

14它将蛋产在地上,

使蛋得到沙土的温暖,

15却不知蛋会被踩碎,

或遭野兽践踏。

16它苛待雏鸟,好像它们并非己出,

就算徒劳一场,它也不怕。

17因为上帝未赐它智慧,

没有给它悟性。

18然而,一旦它展翅奔跑,

必嗤笑马儿和骑士。

19“马的力量岂是你赐的?

它颈上的鬃毛岂是你披的?

20岂是你使它跳跃如蝗虫,

发出令人胆寒的长嘶?

21它在谷中刨地,

炫耀力量,奋力冲向敌军。

22它嘲笑恐惧,毫不害怕,

不因刀剑而退缩。

23它背上的箭袋铮铮作响,

长矛和投枪闪闪发光。

24角声一响,它便无法静立,

狂烈地颤抖,急于驰骋大地。

25听到角声,它就发出长嘶,

它老远便嗅到战争的气味,

并听见吶喊和将领的号令。

26“鹰隼展翅翱翔,飞往南方,

岂是靠你的智慧?

27秃鹰腾飞,在高处搭窝,

岂是奉你的命令?

28它居住在悬崖上,

盘踞在山岩峭壁,

29它从那里搜寻猎物,

它的目光直达远方。

30它的幼雏噬血,

哪里有尸体,它就在哪里。”

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 39:1-30

139:1 Kum 14:5“Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa?

Je, watambua ni wakati gani kulungu jike azaapo mtoto wake?

239:2 Mwa 31:7-9Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo?

Je, unajua majira yao ya kuzaa?

3Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao;

utungu wa kuzaa unakoma.

4Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani;

huenda zao wala hawarudi tena.

539:5 Mwa 16:12; Ay 6:5“Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru?

Ni nani aliyezifungua kamba zake?

639:6 Za 107:34; Yer 2:24; 14:6; Hos 8:9Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake,

nchi ya chumvi kuwa makao yake.

739:7 Ay 5:22; 3:18Huzicheka ghasia za mji,

wala hasikii kelele za mwendesha gari.

839:8 Isa 32:20Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho

na kutafuta kila kitu kibichi.

939:9 Hes 23:22; Kum 33:17“Je, nyati atakubali kukutumikia?

Atakaa karibu na hori lako usiku?

1039:10 Ay 41:13; Za 32:9Je, waweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba?

Je, atalima mabonde nyuma yako?

1139:11 Ay 40:16; 41:12, 22; Za 147:10Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi?

Utamwachia yeye kazi zako nzito?

12Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani

kutoka shambani na kuikusanya kwenye sakafu yako ya kupuria?

1339:13 Zek 5:9“Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha,

lakini hayawezi kulinganishwa

na mabawa na manyoya ya korongo.

14Huyataga mayai yake juu ya ardhi,

na kuyaacha yapate joto mchangani,

1539:15 2Fal 14:9bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda,

kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.

1639:16 Ay 39:17; Mao 4:3Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake;

hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,

1739:17 Ay 21:22; 39:16kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima,

wala hakumpa fungu la akili njema.

1839:18 Ay 5:22Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia,

humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.

1939:19 Ay 39:11“Je, wewe humpa farasi nguvu

au kuivika shingo yake manyoya marefu?

2039:20 Yoe 2:4-5; Ufu 9:7; Yer 8:16Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige,

akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?

2139:21 Yer 8:6Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake,

husonga mbele kukabiliana na silaha.

2239:22 Ay 5:22Huicheka hofu, haogopi chochote,

wala haukimbii upanga.

2339:23 Isa 5:28; Yer 5:16; Nah 3:3Podo hutoa sauti kando yake,

pamoja na mkuki unaongʼaa na fumo.

2439:24 Hes 10:9; Eze 7:14Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi,

wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.

2539:25 Yos 6:5; Yer 8:6; Amo 2:2Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’

Hunusa harufu ya vita toka mbali,

sauti ya mtoa amri na ukelele wa vita.

26“Je, mwewe huruka kwa hekima yako

na kuyakunjua mabawa yake kuelekea kusini?

27Je, tai hupaa juu kwa amri yako

na kujenga kiota chake mahali pa juu?

28Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku;

majabali yenye ncha kali ndiyo ngome yake.

29Kutoka huko hutafuta chakula chake;

macho yake hukiona kutoka mbali.

3039:30 Mt 24:28; Lk 17:37Makinda yake hujilisha damu,

na pale palipo na machinjo, ndipo yeye alipo.”