约书亚记 7 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

约书亚记 7:1-26

亚干犯罪

1以色列人在当毁灭之物的事上犯了罪。因为犹大支派中谢拉的曾孙、撒底的孙子、迦米的儿子亚干拿了一些本该毁灭的东西,耶和华便向以色列人发怒。

2当时,约书亚耶利哥派人去侦察伯特利东边靠近伯·亚文城。 3他们侦察回来后对约书亚说:“那里的居民很少,我们不必劳师动众派所有的人上去,只要派两三千人上去便可以攻取城。” 4于是,大约有三千以色列人去攻打城,不料却被城人击溃。 5城的人杀了他们三十六人,从城门前追杀他们,一直到示巴琳,在下坡处杀败他们。以色列人吓得心惊胆战。

6约书亚以色列的长老便撕裂衣服,把灰撒在头上,俯伏在耶和华的约柜面前,直到晚上。 7约书亚说:“唉!主耶和华啊,你让我们过了约旦河,为什么把我们交在亚摩利人手上,让他们毁灭我们呢?倒不如让我们住在约旦河对岸! 8主啊,现在以色列人被仇敌打败,我还有什么话可说呢? 9迦南人和这一带的人听到这消息以后,必从四面八方来围攻我们,将我们从地上斩尽杀绝。那时候,你的威名又何在呢?”

10耶和华对约书亚说:“起来吧!你为何俯伏在地? 11以色列人犯了罪,违背了我吩咐他们应守的约,偷拿了本该毁灭的东西放在自己的行囊里,还撒谎。 12所以,以色列人受咒诅,无法抵挡敌人,掉头败逃。你必须将那些本该毁灭的东西从你们中间除掉,不然我就不再与你们同在。 13起来吧!去吩咐民众洁净自己,让他们为明天洁净自己,因为以色列的上帝耶和华这样说,‘以色列啊!你们中间有本该毁灭的东西,你们不除掉这些东西就无法抵挡敌人。 14明天早上,你们要按支派一个一个前来,耶和华指出哪个支派,哪支派的各宗族便要前来。耶和华指出哪个宗族,哪宗族的各家族便要前来。耶和华指出哪个家族,哪家族的各成员便要前来。 15哪个人被指出拿了本该毁灭的东西,哪个人及其所有的东西就要被火焚烧。因为他违背了耶和华的约,在以色列人中做了可耻的事。’”

16第二天清早,约书亚按照支派召来以色列人,结果抽中犹大支派; 17他让犹大支派各宗族前来,结果抽中谢拉宗族;他让谢拉宗族前来,结果抽中撒底家族; 18他让撒底家族的人一个一个前来,结果抽中迦米的儿子亚干19约书亚亚干说:“孩子啊,我劝你把荣耀归给以色列的上帝耶和华,向祂认罪,把你所做的事告诉我,不要隐瞒。” 20亚干答道:“我的确得罪了以色列的上帝耶和华。事情是这样的, 21在夺得的财物中,我看上了一件漂亮的示拿外衣、两千二百克银子和五百五十克金子,我一时贪心便拿去了,藏在我帐篷的地底下,银子就放在衣服下面。”

22约书亚派人跑到他的帐篷里,果然在那里找到了那件衣服和衣服下面的银子。 23他们将这些东西带到约书亚和民众那里,摆在耶和华面前。 24约书亚和全体以色列人把谢拉家族的亚干、那些银子、衣服和金子及其儿女、牛、驴、羊、帐篷和一切所有都带到亚割谷。 25约书亚亚干说:“你为什么给我们惹祸呢?今天耶和华要降祸给你。”于是,以色列人便拿石头打死了他和他一切的人畜,将其烧毁。 26他们在亚干身上堆起一大堆石头,那些石头今天还在。耶和华这才息怒,因此那地方至今还叫亚割7:26 亚割”意思是“连累”。谷。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoshua 7:1-26

Dhambi Ya Akani

17:1 Yos 6:18; 1Nya 2:7; Yos 22:20; Hes 1:4; Kut 4:14; 32:20; Law 10:6Lakini Waisraeli hawakuwa waaminifu kuhusu vile vitu vilivyowekwa wakfu; Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, wa kabila la Yuda, alivichukua baadhi ya hivyo vitu. Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli.

27:2 Mwa 12:8; Yos 8:1, 28; 18:12; 1Sam 14:23; Hos 4:15; 5:8; 10:5; Mwa 12:8; Yos 12:16; 16:1; Amu 1:22; 1Sam 30:27; 2Fal 23:15; Yer 48:13; Amo 3:14; 4:4; 5:5-6; 7:10, 13; Hes 21:32Basi Yoshua akatuma watu kutoka Yeriko waende Ai, karibu na Beth-Aveni mashariki ya Betheli, akawaambia, “Pandeni mkaipeleleze nchi.” Basi wale watu wakapanda wakaipeleleza Ai.

3Waliporudi kwa Yoshua, wakasema, “Si lazima watu wote waende kupigana na Ai. Watume watu elfu mbili au tatu wakauteke huo mji. Usiwachoshe watu wote, kwa sababu huko kuna watu wachache tu.” 47:4 Law 26:17; Kum 28:25; 32:30; Isa 30:17; 59:2Basi wakapanda kama watu elfu tatu tu, lakini wakashambuliwa na watu wa Ai, 57:5 Yos 22:20; Mwa 42:28; Za 22; 14; Isa 13:7; Eze 21:7; Nah 2:10; Law 26:36ambao waliwaua watu kama thelathini na sita miongoni mwao. Wakawafukuza Waisraeli kutoka lango la mji hadi Shebarimu, nao wakawauwa huko kwenye materemko. Kutokana na hili mioyo ya watu ikayeyuka ikawa kama maji.

67:6 Mwa 37:29; 17:3; 1Nya 21:16; Eze 9:8; Amu 20:23; Yos 8:10; 9:11; 20:4; 23:2; 1Sam 4:12; 2Sam 13:19; 15:32; Neh 9:1; Ay 2:12; Eze 27:30; Ufu 18:19Ndipo Yoshua akayararua mavazi yake, akaanguka kifudifudi mbele ya Sanduku la Bwana, na akabakia hapo mpaka jioni. Wazee wa Israeli nao wakafanya vivyo hivyo wakatia mavumbi vichwani mwao. 77:7 1Sam 4:3; Kut 5:22; Hes 14:16; 2Fal 3:10Yoshua akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, kwa nini umewavusha watu hawa ngʼambo ya Yordani ili kututia mikononi mwa Waamori watuangamize? Laiti tungeliridhika kukaa ngʼambo ile nyingine ya Yordani! 8Ee Bwana, niseme nini sasa, ikiwa sasa Israeli ameshafukuzwa na adui zake? 97:9 Kut 32:12; Kum 9:28; 28:58; 1Sam 12:22; Za 48:10; 106:8; Yer 14:21Wakanaani na watu wengine wa nchi watasikia habari hii, nao watatuzunguka na kutufutilia jina letu duniani. Utafanya nini basi kwa ajili ya jina lako mwenyewe lililo kuu?”

10Bwana akamwambia Yoshua, “Simama! Unafanya nini hapo chini kifudifudi? 117:11 Kut 9:27; Kum 29:27; Yos 24:16-27; 2Fal 17:7; Hos 10:9; Yos 6:17-19; 23:16; Amu 2:20; 1Sam 15:24; Za 78:10; Mdo 5:1-2Israeli ametenda dhambi. Wamekiuka agano langu nililowaamuru kulishika. Wamechukua baadhi ya vitu vilivyowekwa wakfu, wameiba, wamesema uongo, wameviweka pamoja na mali zao. 127:12 Law 26:37; Za 18:40; 21:12; Law 26:17; Yos 6:18; Za 44:9; 60:10Ndiyo sababu Waisraeli hawawezi kusimama dhidi ya adui zao. Wanawapa visogo na kukimbia kwa kuwa wanastahili maangamizi. Sitakuwa pamoja nanyi tena mpaka mwangamize kila kitu miongoni mwenu kilichotengwa kwa maangamizi.

137:13 Law 11:44; Yos 3:5; Kut 19:10“Nenda, ukawatakase watu. Waambie, ‘Jitakaseni mjiandae kwa kesho; kwa sababu hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Kitu kilichowekwa wakfu kipo katikati yenu, ee Israeli. Hamwezi kusimama dhidi ya adui zenu mpaka mtakapokiondoa.

147:14 1Sam 10:19; Mit 16:33; 1Sam 14:41-42; Yn 1:7; Mdo 1:24-26“ ‘Asubuhi, mjihudhurishe kabila kwa kabila. Itakuwa kabila lile atakalolitwaa Bwana litakuja mbele ukoo kwa ukoo, ukoo ule atakaoutwaa Bwana utakuja mbele jamaa kwa jamaa, nayo jamaa ile atakayoitwaa Bwana itakuja mbele mtu kwa mtu. 157:15 Yos 6:18; Kum 7:25; 2Fal 25:9; 1Nya 14:12; Isa 37:19; Yer 43:12; Eze 30:16; 1Sam 14:39; Mwa 34:7Yule atakayekutwa na vitu vilivyowekwa wakfu, atateketezwa kwa moto, pamoja na vitu vyote alivyo navyo. Kwa kuwa amelivunja agano la Bwana na kufanya kitu cha aibu katika Israeli!’ ”

16Kesho yake asubuhi na mapema Yoshua akawaamuru Israeli kuja mbele kabila kwa kabila; na Yuda akatwaliwa. 177:17 Hes 26:20Koo za Yuda zikaja mbele, naye akawatwaa Wazera. Akaamuru ukoo wa Wazera kuja mbele jamaa kwa jamaa, nayo jamaa ya Zabdi ikatwaliwa. 187:18 Yos 7:1; Law 24:11; Yn 1:7; Mdo 5:1-10; Yer 2:26; Mit 13:21; Hes 32:23; Mwa 4:7Yoshua akaamuru watu wa jamaa ya Zabdi kuja mbele mtu kwa mtu, naye Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, wa kabila la Yuda, akatwaliwa.

197:19 Kut 14:17; 1Sam 6:5; Za 96:8; Isa 42:12; Yer 13:16; Yn 9:24; Law 5:5; 1Sam 14:43Ndipo Yoshua akamwambia Akani, “Mwanangu, mtukuze Bwana, Mungu wa Israeli, nawe ukiri kwake. Niambie ni nini ulichotenda; usinifiche.”

20Akani akamjibu Yoshua, “Ni kweli! Nimetenda dhambi dhidi ya Bwana, Mungu wa Israeli. Hili ndilo nililofanya: 217:21 Mwa 34:29; 49:27; Kum 7:25; Efe 5:5; 1Tim 6:10; Kut 20:17; 1Fal 21:1; 2Fal 5:20-27; Mit 15:27; Hab 2:9; Lk 12:15; Rum 7:7, 8Nilipoona katika nyara joho zuri la kutoka Babeli, shekeli mia mbili7:21 Shekeli 200 za fedha ni sawa na kilo 2.3. za fedha, na kabari ya dhahabu ya uzito wa shekeli hamsini,7:21 Shekeli 50 ni sawa na gramu 600. nikavitamani na nikavichukua. Tazama, vimefichwa ardhini ndani ya hema langu, pamoja na hiyo fedha chini yake.”

22Kwa hiyo Yoshua akatuma wajumbe, nao wakapiga mbio mpaka hemani, tazama, vile vitu vilikuwa vimefichwa hemani mwake, pamoja na ile fedha chini yake. 23Wakavichukua vile vitu toka mle hemani, wakamletea Yoshua pamoja na Waisraeli wote, na wakavitandaza mbele za Bwana.

247:24 Hes 16:27; Yos 7:26; 15:7; Isa 65:10; Hos 2:15Basi Yoshua, pamoja na Israeli yote, wakamchukua Akani mwana wa Zera, pamoja na ile fedha, lile joho, ile kabari ya dhahabu, wanawe na binti zake, ngʼombe, punda na kondoo wake, hema yake pamoja na vitu vyote alivyokuwa navyo, wakavileta katika Bonde la Akori. 257:25 Yos 6:18; Law 20:2; Kum 17:5; 1Fal 12:18; 2Nya 10:18; 24:21; Neh 9:26; Mwa 38:24; 1Nya 2:7; Gal 5:12Yoshua akasema, “Kwa nini umeleta taabu hii juu yetu? Bwana ataleta taabu juu yako leo hii.”

Ndipo Israeli yote ikampiga Akani kwa mawe, na baada ya kuwapiga jamaa yake yote kwa mawe, wakawateketeza kwa moto. 267:26 2Sam 18:17; Mwa 35:20; Hes 25:4; Kum 13:17; Isa 65:10; Hos 2:15; Yos 8:29; 2Sam 18:17; Mao 3:53; Kum 13:17; 2Sam 21:14Wakakusanya lundo la mawe juu ya Akani, ambalo lipo mpaka leo. Naye Bwana akageuka kutoka hasira yake kali. Kwa hiyo mahali pale pakaitwa Bonde la Akori7:26 Akori yamaanisha taabu. tangu siku hiyo.