约书亚记 14 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

约书亚记 14:1-15

约旦河西土地的分配

1以下是祭司以利亚撒的儿子约书亚以色列各支派的首领在迦南分给以色列人的产业, 2是照耶和华给摩西的指示,用抽签的方式分给九个半支派的。 3摩西约旦河东已经把产业分给了吕便迦得支派和玛拿西半个支派,只是没有把产业分给利未人。 4约瑟的子孙已分为玛拿西以法莲两个支派。利未人没有分到地,但有城邑居住,还有城郊可以牧养牲畜,安置财物。 5以色列人照耶和华给摩西的指示分配这些土地。

迦勒分得希伯仑

6那时,犹大支派的人来到吉甲约书亚,其中有基尼洗耶孚尼的儿子迦勒。他对约书亚说:“你知道耶和华在加低斯·巴尼亚跟上帝的仆人摩西提到关于你和我的事。 7我四十岁那年,耶和华的仆人摩西加低斯·巴尼亚派我来侦察这地方,我如实禀告他。 8与我同去的弟兄的禀告令以色列人胆战心惊,但我忠心地追随我的上帝耶和华。 9所以,当日摩西就向我起誓,‘你脚踏过的地方必永远归你和你的子孙作产业,因为你忠心地追随我的上帝耶和华。’ 10耶和华照祂的应许,让我又活了四十五年,这些日子都是跟以色列人在旷野一起度过的。看!我现在已经八十五岁了, 11仍像当年摩西派我出去时那样身强力壮,跟当年一样能征善战。 12现在,求你照耶和华当日向我应许的,把这山区赐给我。你亲耳听到那里有亚衲人,他们的城池高大坚固。但如果耶和华与我同在,我必照着祂的应许把这些人赶走。”

13于是,约书亚便祝福耶孚尼的儿子迦勒,把希伯仑给他,作为他的产业。 14所以,希伯仑至今仍是基尼洗耶孚尼的儿子迦勒的产业,因为他忠心地追随以色列的上帝耶和华。 15希伯仑从前名叫基列·亚巴,亚巴原是亚衲族中最伟大的人。从此,境内太平,没有战争。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoshua 14:1-15

Mgawanyo Wa Nchi Magharibi Mwa Yordani

114:1 Yos 11:23; Za 16:6; 136:21; Kut 6:23; Yos 21:1; Hes 26:53; 34:17-18; Yos 19:51Basi haya ndiyo maeneo Waisraeli waliyopokea kama urithi katika nchi ya Kanaani, ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliwagawia. 214:2 Law 16:8; Hes 34:13; Za 16:5; Mit 16:33; 18:18Urithi wao uligawanywa kwa kura kwa yale makabila tisa na nusu, kama Bwana alivyoamuru Mose. 314:3 Hes 32:33; 34:14; 35:2; Yos 13:14Mose alikuwa amewapa yale makabila mawili na nusu urithi wao upande wa mashariki mwa Yordani, lakini Walawi hawakupewa urithi miongoni mwa hao wengine, 414:4 Mwa 41:54; Amu 1:29; Hes 35:2-3; Yos 21:2kwa kuwa wana wa Yosefu walikuwa makabila mawili; Manase na Efraimu. Walawi hawakupata mgawo wa ardhi, bali walipewa miji tu kwa ajili ya kuishi, pamoja na maeneo ya malisho kwa ajili ya makundi yao ya kondoo, mbuzi na ngʼombe wao. 514:5 Hes 34:13; 35:2; Yos 21:2; Eze 45:1-8; 48:8, 22Kwa hiyo Waisraeli wakagawana ile nchi, kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.

Kalebu Anapewa Mji Wa Hebroni

614:6 Kum 11:30; Hes 13:6; 14:30; Kum 33:1; Hes 14:38; Yos 15:17; Kum 1:19Kisha watu wa Yuda wakamwendea Yoshua huko Gilgali, naye Kalebu mwana wa Yefune yule Mkenizi, akamwambia, “Unajua jambo ambalo Bwana alimwambia Mose mtu wa Mungu huko Kadesh-Barnea kukuhusu wewe na mimi. 714:7 Yos 15:6; Hes 13:17; 13:30; 14:6-9Nilikuwa na umri wa miaka arobaini, wakati Mose mtumishi wa Bwana, aliponituma kutoka Kadesh-Barnea kuipeleleza hiyo nchi. Nami nikamletea taarifa kama kulingana na nilivyosadiki moyoni. 814:8 Hes 13:31; 14:24; 32:12; Kum 1:36; Ufu 14:4Lakini ndugu zangu tuliopanda nao waliifanya mioyo ya watu iyeyuke kwa hofu. Bali mimi, nilimfuata Bwana Mungu wangu kwa moyo wote. 914:9 Kum 11:24; Hes 14:24; Yos 1:3; Hes 13:22Hivyo katika siku ile, Mose akaniapia, ‘Nchi ambayo umeikanyaga kwa miguu yako itakuwa urithi wako na wa watoto wako milele, kwa sababu umemfuata Bwana Mungu wangu kwa moyo wote.’

1014:10 Hes 11:28; 14:30; Yos 5:6; 13:1; Hes 14:30; Kum 31:2; Za 90:10“Sasa basi, kama vile Bwana alivyoahidi, ameniweka hai kwa miaka arobaini na mitano tangu wakati alipomwambia Mose jambo hili, wakati Waisraeli wakiwa wanazunguka jangwani. Hivyo mimi hapa leo, nina umri wa miaka themanini na mitano! 1114:11 Kum 34:7; Mwa 15:15Bado ninazo nguvu kama siku ile Mose aliponituma. Bado ninazo nguvu za kwenda vitani sasa kama vile nilivyokuwa wakati ule. 1214:12 Hes 14:24-28; 13:33; 1Sam 14:6; 2Nya 14:11, 12; Za 18:32; 44:3; Rum 8:31; Flp 4:13; Yos 15:14; Amu 1:10Basi nipe nchi hii ya vilima, ambayo Bwana aliniahidi siku ile. Wewe mwenyewe ulisikia wakati ule kwamba Waanaki walikuwako huko na miji yao ilikuwa mikubwa na yenye maboma, lakini, kwa msaada wa Bwana, nitawafukuza watoke huko kama vile alivyonena.”

1314:13 Yos 22:6-7; 1Sam 30:14; Mwa 23:19; Yos 10:36; Amu 1:26; 1Nya 6:56Ndipo Yoshua akambariki Kalebu mwana wa Yefune, na akampa Hebroni kama urithi wake. 1414:14 Hes 14:24Hivyo Hebroni imekuwa mali ya Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi tangu wakati ule, kwa sababu alimwandama Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wote. 1514:15 Mwa 23:2; Yos 15:13; 11:23; Amu 3:11; 1Fal 4:24; 5:4; 1Nya 22:9(Hebroni uliitwa Kiriath-Arba hapo mwanzo, kutokana na huyo Arba ambaye alikuwa mtu mkuu kupita wote miongoni mwa Waanaki.)

Kisha nchi ikawa na amani bila vita.