箴言 6 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

箴言 6:1-35

日常警言

1孩子啊,你若为邻人作保,

为外人击掌立约;

2你若被自己口中的话套住,

被自己的诺言缠住,

3孩子啊,你已落入邻人的手中,

你当如此自救:

要谦卑地向他求情。

4勿让你的眼睛睡觉,

莫叫你的眼皮打盹。

5要救自己脱离困境,

像羚羊挣脱猎人的手,

飞鸟逃脱捕鸟人的手。

6懒惰的人啊,去看看蚂蚁,

观察它的生活,就会有智慧。

7蚂蚁没有元帅,

没有官长,

也没有君王,

8却在夏季储备粮食,

在收割时积聚食物。

9懒惰的人啊,你要躺到何时?

要睡到何时才起床?

10再睡一会儿,再打个盹儿,

抱着手躺一会儿,

11贫穷要像盗贼一样攻击你,

缺乏要像武士一样扑向你。

12无赖与恶人满口诡诈,

13挤眉弄眼,手脚示意,

14心术不正,设下诡计,惹事生非。

15因此,灾难必突然临到,

他们顷刻之间遭到毁灭,

无可挽救。

16耶和华所憎恶的事有六样,

连祂厌恶的事共有七样:

17高傲的眼睛,

撒谎的舌头,

杀害无辜的手,

18图谋诡计的心,

奔跑作恶的脚,

19撒谎的假证人和在弟兄中挑起争端的人。

20孩子啊,要遵守你父亲的诫命,

不可背弃你母亲的训言。

21你要常常将这些刻在心坎上,

系在颈项上。

22你行走,它们必引领你;

你躺卧,它们必护卫你;

你醒来,它们必与你交谈。

23因为诫命是灯,训言是光,

管教责备是生命之道,

24能使你远离邪恶的女人,

避开油嘴滑舌的妓女。

25你的心不要贪恋她的美色,

也不要被她的媚眼所迷惑,

26因为娼妓会使人倾家荡产6:26 娼妓会使人倾家荡产”或译“娼妓的淫资不过是一个饼”。

淫妇会猎杀人宝贵的生命。

27人若将火藏在怀中,

哪能不烧着衣服呢?

28人若行走在火炭上,

哪能不烫伤双脚呢?

29与别人妻子通奸也是这样,

凡靠近她的必难逃罪责。

30贼因充饥而偷,

没有人藐视他;

31但若被抓到,他要偿还七倍,

就是倾家荡产也要偿还。

32和有夫之妇通奸的,

实在愚不可及,

他是自寻死路。

33他必挨打,受辱,

他的耻辱永难抹去。

34那丈夫妒火燃烧,

报仇时绝不留情。

35赔他再多财物,他也不会接受;

送他再多礼物,他都不肯罢休。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 6:1-35

Maonyo Dhidi Ya Upumbavu

16:1 Mwa 43:9; Ebr 7:22; Ezr 10:27; Mit 17:18Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako,

ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi

kwa ajili ya mwingine,

2kama umetegwa na ulichosema,

umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,

3basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru,

kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako:

Nenda ukajinyenyekeshe kwake;

msihi jirani yako!

46:4 Rut 3:18; Za 132:4Usiruhusu usingizi machoni pako,

usiruhusu kope zako zisinzie.

56:5 Za 91:3; 2Sam 2:18; Isa 13:14; Za 91:3Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji,

kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.

66:6 Mit 6:11Ewe mvivu, mwendee mchwa;

zitafakari njia zake ukapate hekima!

7Kwa maana yeye hana msimamizi,

wala mwangalizi, au mtawala,

86:8 Mit 30:24-25; 10:4lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi

na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.

96:9 Mit 24:30-34; 26:13-16Ewe mvivu, utalala hata lini?

Utaamka lini kutoka usingizi wako?

106:10 Mit 24:33; Mhu 4:5Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo,

bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:

116:11 Mit 6:10-11; 20:13; 24:30-34hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi,

na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.

12Mtu mbaya sana na mlaghai,

ambaye huzungukazunguka

na maneno ya upotovu,

136:13 Za 35:19; Mit 16:30ambaye anakonyeza kwa jicho lake,

anayetoa ishara kwa miguu yake

na kuashiria kwa vidole vyake,

146:14 Za 36:4; 140:2; Mik 2:1; Isa 32:7ambaye hupanga ubaya

kwa udanganyifu moyoni mwake:

daima huchochea fitina.

15Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula;

ataangamizwa mara, pasipo msaada.

166:16 Mit 3:32; 8:13; 15:8, 9, 26; 16:5Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana,

naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:

176:17 Za 120:2; Mit 12:22; Yer 2:34; Mik 7:2; Hos 4:1-2macho ya kiburi,

ulimi udanganyao,

mikono imwagayo damu isiyo na hatia,

186:18 Mwa 6:5; Ay 15:31; Rum 3:15moyo uwazao mipango miovu,

miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,

196:19 Kum 19:16; Za 27:12; Mit 15:18; Zek 8:17shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo,

na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.

Onyo Dhidi Ya Uasherati

206:20 Mit 3:21; 1:8Mwanangu, zishike amri za baba yako,

wala usiyaache mafundisho ya mama yako.

216:21 Kum 6:8; Mit 3:3Yafunge katika moyo wako daima,

yakaze kuizunguka shingo yako.

226:22 Mit 3:23; 2:11Wakati utembeapo, yatakuongoza;

wakati ulalapo, yatakulinda;

wakati uamkapo, yatazungumza nawe.

236:23 Za 19:8; 10:17Kwa maana amri hizi ni taa,

mafundisho haya ni mwanga

na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,

246:24 Mwa 39:8; Za 55:21yakikulinda na mwanamke aliyepotoka,

kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.

256:25 2Sam 11:2-5; Mt 5:28Moyo wako usitamani uzuri wake

wala macho yake yasikuteke,

266:26 Mit 27:22-23; 29:3; Eze 13:18kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini,

hata ukose kipande cha mkate,

naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.

27Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake

bila nguo zake kuungua?

28Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka

bila miguu yake kuungua?

296:29 Kut 20:14; Mit 2:16-19Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine;

hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.

30Watu hawamdharau mwizi kama akiiba

kukidhi njaa yake wakati ana njaa.

316:31 Kut 22:1-14Pamoja na hayo, kama akikamatwa,

lazima alipe mara saba,

ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.

326:32 Kut 20:14; Mit 7:7; 9:4, 16Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa;

yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.

336:33 Mit 5:9-14Mapigo na aibu ni fungu lake

na aibu yake haitafutika kamwe;

346:34 Hes 5:14; Mwa 34:7kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume,

naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.

356:35 Ay 31:9-11; Wim 8:7Hatakubali fidia yoyote;

atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.