申命记 19 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

申命记 19:1-21

设立避难城

1“你们的上帝耶和华毁灭那些民族,把他们的土地赐给你们,使你们赶走他们,住进他们的城邑和房屋后, 2-3你们要把土地划分为三个地区,在每个地区设立一座避难城,修好通往这三座城的道路,以便误杀人者可以逃往最近的避难城。

4“如果有人无意间杀了素无冤仇的同伴,他可以逃往避难城,以保住性命。 5例如,有人和朋友去森林砍树,斧头脱柄,误杀了朋友,他就可以逃往避难城,以保住性命。 6否则,如果避难城离误杀人者太远,怒火中烧的报仇者就会追上去杀死他。其实他是不该死的,因为他与被误杀的人素无冤仇。 7因此,我吩咐你们要设立三座避难城。

8-9“如果你们谨遵我今天吩咐你们的这一切诫命,爱你们的上帝耶和华,一生遵行祂的旨意,祂就会按照祂对你们祖先所起的誓,扩张你们的疆域,把应许给你们祖先的土地赐给你们。那时,你们要再设三座避难城, 10免得无辜人的血流在你们的上帝耶和华赐给你们作产业之地,以致你们担当枉杀无辜的罪。

11“如果有人因憎恨邻居而暗中埋伏,杀了邻居,然后逃到避难城, 12他本城的长老要派人去把他带回来,交给复仇的人,将他处死。 13不可怜悯他,要从以色列除掉这种滥杀无辜的罪,这样你们才会顺利。

14“在你们的上帝耶和华将要赐给你们作产业之地,你们不可挪动邻居的界石,因为那是先人立的。

15“如果人犯了什么罪或有什么过失,不可凭一个证人作证就定罪,要有两三个证人才可以定案。 16如果有人作伪证诬陷别人, 17诉讼双方要站在耶和华面前,让当值的祭司和审判官定夺。 18审判官要仔细审查案件,如果发现那人作伪证, 19就要按照他企图加给被诬告者的伤害处罚他。这样,就从你们当中除掉了罪恶。 20其他人听说后,都会害怕,不敢再做这种恶事。 21你们对恶人不可心软,要以命偿命,以眼还眼,以牙还牙,以手还手,以脚还脚。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 19:1-21

Miji Ya Makimbilio

(Hesabu 35:9-34; Yoshua 20:1-9)

119:1 Kum 6:10-11; 12:29Wakati Bwana Mungu wenu atakapokuwa amewaangamiza mataifa ambayo nchi yao anawapa ninyi, wakati mtakapokuwa mmewafukuza na kuishi katika miji yao na nyumba zao, 219:2 Yos 20:2ndipo mtenge miji mitatu iliyopo katikati ya nchi kwa ajili yenu, katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kuimiliki. 3Jengeni barabara katika miji hiyo na kuigawa mara tatu, nchi anayowapa Bwana Mungu wenu kama urithi, ili kwamba yeyote amuuaye mtu aweze kukimbilia humo.

4Hii ndiyo kanuni kuhusu mtu amuuaye mwingine na kukimbilia humo kuokoa maisha yake, yaani, yeye amuuaye jirani yake bila kukusudia, wala hakumchukia kabla ya hapo. 5Kwa mfano, mtu aweza kwenda msituni na jirani yake kukata miti, naye anapozungusha shoka kuangusha mti, shoka linaweza kuchomoka kutoka kwenye mpini na kumpiga jirani yake na kumuua. Yule mtu anaweza kukimbilia katika mmojawapo ya miji hii na kuokoa maisha yake. 619:6 Hes 35:12Kama sivyo, mlipiza kisasi cha damu anaweza kumfuatilia kwa hasira kali, naye akamkamata na kumuua kama umbali ni mrefu sana hata ingawa hastahili kifo, kwa sababu amemuua jirani yake bila kukusudia. 7Hii ndiyo sababu nimewaagiza ninyi kutenga miji mitatu ya makimbilio kwa ajili yenu.

819:8 Kut 34:24; Mwa 15:18; Kum 11:24Kama Bwana Mungu wenu akipanua nchi yenu, kama alivyoahidi kwa kiapo kwa baba zenu na kuwapa nchi yote aliyowaahidi, 919:9 Kum 6:5; Yos 20:7-8kwa sababu mmefuata kwa uangalifu sheria zote ninazowaamuru leo, kumpenda Bwana Mungu wenu na kuenenda siku zote katika njia zake, ndipo mtenge miji mingine, mitatu zaidi. 1019:10 Mit 6:17; Yer 7:6; 26:15; Kum 21:1-9; Hes 35:33Fanyeni hivi ili damu isiyo na hatia isimwagwe katika nchi yenu, ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi wenu, ili kwamba msije mkawa na hatia ya kumwaga damu.

1119:11 Kut 21:12; Hes 35:16; 1Yn 3:15; Mit 28:17; 29:10Lakini kama mtu anamchukia ndugu yake, akamvizia, akamshambulia na kumuua, kisha akakimbilia katika mmojawapo ya miji hii, 12wazee wa mji wake watatuma ujumbe kwake, kumleta kutoka mji ule na kumkabidhi mlipiza kisasi cha damu kumuua. 1319:13 Kum 7:2; 21:9; 1Fal 2:31Msimwonee huruma. Lazima mwondoe katika Israeli hatia ya umwagaji damu isiyo na hatia ili kwamba mpate kufanikiwa.

1419:14 Kum 27:17; Ay 24:2; Za 16:6; Mit 15:25; 22:28; 23:10; Isa 1:23; Hos 5:10Usisogeze jiwe la mpaka wa jirani yako ambao uliwekwa na wale waliokutangulia katika urithi upokeao katika nchi Bwana Mungu wako anayowapa kuimiliki.

Mashahidi

1519:15 Kum 17:6; Mt 18:16; 26:60; 2Kor 3:1; Yn 8:17; 1Tim 5:19; Ebr 10:28Shahidi mmoja hatoshi kumtia hatiani mtu kwa uhalifu au kosa lolote ambalo anaweza kuwa amelitenda. Lazima shauri lolote lithibitishwe kwa ushuhuda wa mashahidi wawili au watatu.

1619:16 Kut 23:1; Mit 6:19; Za 27:12; 1Fal 21:13Kama shahidi mwenye nia ya kumdhuru mwingine akisimama kumshtaki mtu kwa uhalifu, 1719:17 Kut 21:6; Kum 17:6watu wawili wanaohusika katika mabishano lazima wasimame mbele za Bwana na mbele ya makuhani na waamuzi ambao wako kazini wakati huo. 1819:18 Kut 23:7Waamuzi lazima wafanye uchunguzi kwa makini na shahidi akionekana kuwa ni mwongo, akitoa ushuhuda wa uongo dhidi ya ndugu yake, 1919:19 Mit 19:5-10; 1Kor 5:13; Dan 6:24basi mtende kama alivyotaka kumtendea ndugu yake. Ni lazima mwondoe uovu miongoni mwenu. 2019:20 Kum 13:11; 17:13; 13:13; 21:21Watu watakaosalia watasikia hili na kuogopa, uovu kama huo kamwe hautatendeka tena miongoni mwenu. 2119:21 Kut 21:24; Mt 5:38Msionyeshe huruma, uhai kwa uhai, jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu.