列王纪下 19 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

列王纪下 19:1-37

希西迦向以赛亚求助

1希西迦王听了就撕裂衣服,披上麻衣,进入耶和华的殿。 2他派身披麻衣的宫廷总管以利亚敬、书记舍伯那和祭司中的长者去见亚摩斯的儿子以赛亚先知, 3对他说:“希西迦说,‘今天是遭难、蒙羞、受辱的日子,就像婴儿要出生,产妇却无力生产一样。 4亚述王派他的将军来辱骂永活的上帝,也许你的上帝耶和华听见那些话,就会惩罚他。所以,请你为我们这些剩下的人祷告。’” 5希西迦王的臣仆说完这些话后, 6以赛亚对他们说:“告诉你们主人,耶和华这样说,‘你不要因亚述王的仆人那些亵渎我的话而害怕。 7我必惊动19:7 惊动”希伯来文是“使灵进入”。亚述王的心,让他听见一些风声后便返回本国,在那里死于刀下。’”

希西迦向上帝祷告

8亚述的将军听说亚述王已离开拉吉,便回去见王,发现王在攻打立拿9亚述王听说古实特哈加正前来攻打他,便再次派使者去对希西迦说: 10“不要让你所倚靠的上帝愚弄你,说什么耶路撒冷必不会被亚述王攻陷。 11你肯定听过亚述诸王扫灭列国的事,难道你能幸免吗? 12我先祖毁灭了歌散哈兰利色提·拉撒伊甸人,这些国家的神明救得了他们吗? 13哈马王、亚珥拔王、西法瓦音城的王、希拿王和以瓦王如今在哪里呢?”

14希西迦从使者手中接过信,读完后走进耶和华的殿,在耶和华面前展开信, 15祷告说:“坐在二基路伯天使之上、以色列的上帝耶和华啊,唯有你是天下万国的上帝,你创造了天地。 16耶和华啊,求你侧耳垂听!耶和华啊,求你睁眼察看!求你听听西拿基立派使者来辱骂永活上帝的话。 17耶和华啊,亚述诸王确实扫灭列国,使其土地荒凉, 18把列国的神像丢在火中。因为那些神像只是人用木头石头制造的,根本不是神。 19我们的上帝耶和华啊,现在求你从亚述王手中拯救我们,让天下万国都知道唯有你是耶和华。”

以赛亚给希西迦的信息

20亚摩斯的儿子以赛亚派人告诉希西迦:“以色列的上帝耶和华说,‘我已经听见你关于亚述西拿基立的祷告。 21以下是耶和华对他的判语,

“‘锡安的居民藐视你,嘲笑你;

耶路撒冷的居民朝你逃窜的背影摇头。

22你在侮辱、亵渎谁呢?

你不放在眼里、

高声骂的是谁呢?

以色列的圣者!

23你借你的使者辱骂主,

你说你率领许多战车上到群山之巅,

上到黎巴嫩的巅峰,

砍下最高的香柏树和上好的松树,

征服最高的山和最美的树林。

24你自夸已在外邦之地挖井取水,

已用脚掌踏干埃及的河流。

25“‘难道你不知道这是我在太初所定、

在亘古就筹划好的吗?

如今我实现了所定的计划——

借着你使坚城沦为废墟。

26城中的居民软弱无力,

惊慌失措,羞愧难当,

脆弱如野草和菜蔬,

又像还未长大就被晒焦的房顶草。

27“‘你起你坐,你出你进,

你向我发怒,我都知道。

28因为你向我发怒,

你狂傲的话达到了我耳中,

我要用钩子钩住你的鼻子,

把嚼环放在你嘴里,

使你原路返回。’

29希西迦啊,我要赐给你们一个兆头,你们今年要吃野生的,明年也要吃自然生长的,后年要播种收割,栽种葡萄园,吃园中的果子。 30犹大的幸存者要再次向下扎根,向上结果。 31因为将有余民从耶路撒冷出来,有幸存者从锡安山出来。耶和华必热切地成就这事。

32“至于亚述王,耶和华说,‘他必不能进这城或向这里射一箭,必不能手持盾牌兵临城下或修筑攻城的高台。 33他从哪条路来,也将从哪条路回去,他必进不了这城。这是耶和华说的。 34我必为自己和我仆人大卫而保护、拯救这城。’”

35当晚,耶和华的天使到亚述营中杀了十八万五千人。人们清早起来,发现到处是尸体。 36亚述西拿基立便拔营回国,住在尼尼微37一天,亚述王在他的神明尼斯洛的庙里祭拜时,他的两个儿子亚得米勒沙利色用刀杀了他,逃往亚拉腊。他的另一个儿子以撒哈顿继位。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 19:1-37

Hezekia Autafuta Msaada Wa Bwana

(Isaya 37:1-20)

119:1 Mwa 37:34; Hes 14:6Mfalme Hezekia aliposikia haya, akararua nguo zake na kuvaa nguo ya gunia, naye akaenda katika Hekalu la Bwana. 219:2 Yer 19:1; Mwa 37:34Akawatuma Eliakimu msimamizi wa nyumba ya mfalme, Shebna mwandishi, na viongozi wa makuhani, wote wakiwa wamevaa nguo za magunia, waende kwa nabii Isaya mwana wa Amozi. 319:3 Hos 13:13Wakamwambia, “Hili ndilo asemalo Hezekia: Siku hii ni siku ya dhiki, ya kukaripiwa na ya aibu, kama wakati watoto wanapofikia karibu kuzaliwa na kumbe hakuna nguvu ya kuwazaa. 419:4 2Sam 16:12; Yer 37:3Yamkini Bwana, Mungu wako atayasikia maneno ya jemadari wa jeshi, ambaye bwana wake, mfalme wa Ashuru, amemtuma kumdhihaki Mungu aliye hai, tena kwamba atamkemea kwa maneno ambayo Bwana, Mungu wako ameyasikia. Kwa hiyo omba kwa ajili ya mabaki ambao bado wako.”

5Maafisa wa Mfalme Hezekia walipofika kwa Isaya, 619:6 Kum 3:2; Yos 1:9Isaya akawaambia, “Mwambieni bwana wenu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Usiogope kwa hayo uliyoyasikia, yale maneno ambayo watumishi wa mfalme wa Ashuru wamenitukana nayo. 719:7 Kut 14:24; 2Nya 32:21Sikiliza! Nitatia roho fulani ndani yake ili atakaposikia taarifa fulani, atarudi nchi yake mwenyewe, nami huko nitafanya auawe kwa upanga.’ ”

819:8 2Fal 18:14; Hes 33:20Jemadari wa jeshi aliposikia kwamba mfalme wa Ashuru ameondoka Lakishi, alirudi, akamkuta mfalme akipigana na Libna.

9Basi Senakeribu akapata taarifa kwamba Tirhaka, Mkushi mfalme wa Misri, alikuwa anaenda kupigana naye. Basi akatuma tena wajumbe kwa Hezekia na neno hili: 1019:10 2Fal 18:5“Mwambieni Hezekia mfalme wa Yuda: Usikubali huyo Mungu unayemtumainia akudanganye wakati anaposema, ‘Yerusalemu haitatiwa mkononi mwa mfalme wa Ashuru.’ 11Hakika umesikia yale ambayo wafalme wa Ashuru wametenda kwa nchi zote, wakiwaangamiza kabisa. Je, wewe utaokolewa? 1219:12 2Fal 18:33; Mwa 11:31Je, miungu ya mataifa ambayo yaliangamizwa na baba zangu iliweza kuwaokoa, hiyo miungu ya Gozani, Harani, Resefu, na ya watu wa Edeni waliokuwa Telasari? 1319:13 2Fal 5:7Yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme wa Arpadi, mfalme wa mji wa Sefarvaimu, au wa Hena au wa Iva?”

Maombi Ya Hezekia

1419:14 2Fal 5:7Hezekia akapokea barua kutoka kwa wale wajumbe, naye akaisoma. Kisha akapanda katika Hekalu la Bwana, akaikunjua mbele za Bwana. 1519:15 Mwa 3:24; Kut 25:22Naye Hezekia akamwomba Bwana akisema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, uketiye juu ya kiti cha enzi kati ya makerubi, wewe peke yako ndiwe Mungu juu ya falme zote za dunia. Wewe umeumba mbingu na nchi. 1619:16 Za 31:2; Kut 3:16Tega sikio, Ee Bwana, usikie; fungua macho yako, Ee Bwana, uone; sikiliza maneno ambayo Senakeribu ametuma kumtukana Mungu aliye hai.

17“Ni kweli, Ee Bwana, kwamba wafalme wa Ashuru wameyaangamiza mataifa haya na nchi zao. 1819:18 Yer 10:3-10; Mdo 17:29Wameitupa miungu yao kwenye moto na kuiangamiza, kwa kuwa haikuwa miungu, bali miti na mawe tu iliyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu. 1919:19 1Sam 12:10; Yos 4:24Sasa basi, Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe kutoka mkononi mwake, ili falme zote duniani zipate kujua kwamba wewe peke yako, Ee Bwana, ndiwe Mungu.”

Isaya Anatoa Unabii Wa Kuanguka Kwa Senakeribu

(Isaya 37:21-38)

2019:20 1Fal 9:3Kisha Isaya mwana wa Amozi akapeleka ujumbe kwa Hezekia, akasema: “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nimesikia maombi yako kuhusu Senakeribu mfalme wa Ashuru. 2119:21 Isa 47:1; Mao 2:13; Ay 16:4Hili ndilo neno ambalo Bwana amelisema dhidi yake:

“ ‘Bikira Binti Sayuni anakudharau na kukudhihaki.

Binti Yerusalemu anatikisa kichwa chake unapokimbia.

2219:22 Law 19:2; Hos 11:9Ni nani uliyemtukana na kumkufuru?

Ni nani uliyeinua sauti yako dhidi yake,

na kumwinulia macho yako kwa kiburi?

Ni dhidi ya yule Aliye Mtakatifu wa Israeli!

2319:23 Za 20:7; Eze 31:3Kupitia kwa wajumbe wako

umelundika matukano juu ya Bwana.

Nawe umesema,

“Kwa magari yangu mengi ya vita,

nimepanda juu ya vilele vya milima,

vilele vya juu sana katika Lebanoni.

Nami nimeiangusha mierezi yake mirefu,

misunobari yake iliyo bora sana.

Nimefikia sehemu zake zilizo mbali sana,

misitu yake iliyo mizuri sana.

24Nimechimba visima katika nchi za kigeni

na kunywa maji yake.

Kwa nyayo za miguu yangu

nimekausha vijito vyote vya Misri.”

2519:25 Isa 22:11; Mik 1:6“ ‘Je, hujasikia?

Zamani sana niliamuru hili.

Siku za kale nilipanga hili;

sasa nimelifanya litokee,

kwamba umegeuza miji yenye ngome

kuwa malundo ya mawe.

2619:26 Eze 7:17; Ay 8:12Watu wa miji hiyo wameishiwa nguvu,

wanavunjika mioyo na kuaibishwa.

Wao ni kama mimea katika shamba,

kama machipukizi mororo ya kijani,

kama majani yachipuayo juu ya paa la nyumba,

ambayo hukauka kabla ya kukua.

2719:27 Za 139:1-4“ ‘Lakini ninajua mahali ukaapo,

kutoka kwako na kuingia kwako,

na jinsi unavyoghadhibika dhidi yangu.

2819:28 2Nya 33:11; Eze 29:4Kwa sababu unaghadhibika dhidi yangu,

na ufidhuli wako umefika masikioni mwangu,

nitaweka ndoana yangu puani mwako

na hatamu yangu kinywani mwako,

nami nitakufanya urudi kwa njia ile uliyoijia.’

2919:29 Lk 2:12; Za 107:37“Hii ndiyo itakuwa ishara kwako, ee Hezekia:

“Mwaka huu utakula kile kiotacho chenyewe,

na mwaka wa pili utakula kutoka machipukizi yake.

Lakini katika mwaka wa tatu, panda na uvune,

panda mashamba ya mizabibu na ule matunda yake.

3019:30 Mwa 45:7; Amo 9:14Mara nyingine tena mabaki ya nyumba ya Yuda

wataeneza mizizi chini na kuzaa matunda juu.

3119:31 Mwa 45:7; Isa 9:7Kwa kuwa kutoka Yerusalemu watakuja mabaki,

na kutoka Mlima Sayuni kundi la walionusurika.

Wivu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote ndio utatimiza jambo hili.

32“Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana kuhusu mfalme wa Ashuru:

“Hataingia katika mji huu

wala hatapiga mshale hapa.

Hatakuja mbele yake akiwa na ngao,

wala kupanga majeshi kuuzingira.

33Kwa njia ile aliyoijia, ndiyo atakayorudi;

hataingia katika mji huu,

asema Bwana.

3419:34 2Fal 20:6; 2Sam 7:15Nitaulinda mji huu na kuuokoa,

kwa ajili yangu mwenyewe,

na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.”

3519:35 Ay 24:24Usiku ule, malaika wa Bwana akaenda, akawaua wanajeshi 185,000 katika kambi ya Waashuru. Wenzao walipoamka asubuhi yake, walikuta maiti kila mahali! 3619:36 Mwa 10:11Basi Senakeribu mfalme wa Ashuru akavunja kambi na kuondoka. Akarudi Ninawi na kukaa huko.

3719:37 2Fal 17:31; Mwa 8:4Siku moja, alipokuwa akiabudu katika hekalu la mungu wake Nisroki, wanawe Adrameleki na Shareza wakamuua kwa upanga, nao wakakimbilia nchi ya Ararati. Naye Esar-Hadoni mwanawe akawa mfalme badala yake.