何西阿书 4 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

何西阿书 4:1-19

耶和华指控以色列

1以色列人啊,

你们要留心听耶和华的话。

祂指控住在这片土地上的居民,说:

“这片土地上的人不忠不信,

毫无良善,不认识上帝。

2他们咒诅、撒谎、凶杀、偷窃、通奸,

为所欲为,血案累累。

3所以,这片土地要哀鸣,

所有的居民都要消亡,

田间的野兽、空中的飞鸟、

水里的鱼类也要灭绝。”

4耶和华说:

“谁都不要指控别人,

谁都不要责备别人,

因为我要指控的是你们祭司。

5你们白天黑夜都要跌倒,

先知也要跟你们一起跌倒,

所以我要毁灭你们的母亲以色列

6我的子民因不认识我而遭毁灭。

因为你们拒绝认识我,

我也要拒绝让你们做我的祭司;

因为你们忘记我的律法,

我也要忘记你们的儿女。

7你们祭司越增多,

所犯的罪也越多,

所以我要使你们的尊荣变为羞耻。

8你们祭司借我子民的赎罪祭自肥,

满心希望他们犯罪。

9将来,我的子民如何,

你们祭司也如何。

我要照你们的所作所为惩罚你们、报应你们,

10使你们吃却不得饱足,

行淫却不得后代4:10 行淫却不得后代”此处的意思是指责以色列人祭拜迦南人掌管生育的神明。他们以为这样能带来更多后代。

因为你们背弃耶和华,

11沉溺酒色,丧失心志。

12“我的子民祈求木头,

随从木杖的指引。

淫乱的心使他们走入歧途,

他们不忠不贞,背弃他们的上帝。

13他们在山顶和高岗上的橡树、

杨树和栗树下献祭烧香,

因为树荫怡人。

“所以,你们的女儿卖淫,

你们的儿媳通奸。

14但我不会因此而惩罚她们,

因为你们也与娼妓苟合,

与庙妓一起献祭。

无知的民族必走向灭亡。

15“虽然以色列如同妓女,对我不忠,

但不要使犹大犯罪。

不要到吉甲去,

不要到伯·亚文4:15 伯·亚文”意思是“罪恶之家”,在此指伯特利。“伯特利”意思是“上帝之家”,但当时已变成祭拜偶像之地。去,

不要凭永活的耶和华起誓。

16以色列桀骜不驯,

如同桀骜不驯的母牛。

耶和华怎能牧养他们,

如同在草场上牧养羊羔呢?

17以法莲4:17 以法莲”为北国以色列最大的支派,圣经中有时用来代指北国以色列。本卷书中下同。与偶像为伍,

任由他吧!

18他们酒足兴尽之后,

便不住地行淫;

他们的首领恋慕羞耻之事。

19风要把他们卷走,

他们必因所献的祭而蒙羞。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hosea 4:1-19

Shtaka Dhidi Ya Israeli

14:1 Mit 10:21; 24:2; Mik 6:2; Isa 1:3; Ay 10:2; Yer 2:9; 7:28; 51:5; Hos 2:20Sikieni neno la Bwana, enyi Waisraeli,

kwa sababu Bwana analo shtaka

dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi:

“Hakuna uaminifu, hakuna upendo,

hakuna kumjua Mungu katika nchi.

24:2 Isa 59:3; Hos 5:2; 6:2; 7:1; 11:12; Eze 22:2-9; 1Fal 21:16Kuna kulaani tu, uongo na uuaji,

wizi na uzinzi,

bila kuwa na mipaka,

nao umwagaji damu mmoja

baada ya mwingine.

34:3 Yer 4:25, 28; 9:10; Amo 8:8; Isa 15:6; 33:9; Sef 1:3Kwa sababu hii nchi huomboleza,

wote waishio ndani mwake wanadhoofika,

wanyama wa kondeni, ndege wa angani

na samaki wa baharini wanakufa.

44:4 Kum 17:12; Eze 3:26“Lakini mtu awaye yote na asilete shtaka,

mtu yeyote na asimlaumu mwenzake,

kwa maana watu wako ni kama wale

waletao mashtaka dhidi ya kuhani.

54:5 Eze 7:19; 14:7; Hos 2:2Unajikwaa usiku na mchana,

nao manabii hujikwaa pamoja nawe.

Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:

64:6 Mit 10:21; Hos 2:13; 8:1-12; Mal 2:7-8watu wangu wanaangamizwa

kwa kukosa maarifa,

“Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa,

mimi nami nitakukataa wewe

usiwe kuhani kwangu mimi;

kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako

mimi nami sitawajali watoto wako.

74:7 Hab 2:16; Hos 9:11; 13:6Kadiri makuhani walivyoongezeka,

ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu,

walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.

84:8 Isa 56:11; Mik 3:11; Hos 14:1Hujilisha dhambi za watu wangu

na kupendezwa na uovu wao.

94:9 Isa 24:2; Yer 5:31; Hos 8:13; 10:10; 12:2Hata itakuwa: Kama walivyo watu,

ndivyo walivyo makuhani.

Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao

na kuwalipa kwa matendo yao.

104:10 Mik 6:14; Isa 55:2; Hos 7:14; 9:17; Eze 22:9; Law 26:26“Watakula lakini hawatashiba;

watajiingiza katika ukahaba

lakini hawataongezeka,

kwa sababu wamemwacha Bwana

na kujiingiza wenyewe

114:11 Isa 28:7; Hos 5:4; Mit 20:1; Law 10:9; 1Sam 25:36katika ukahaba,

divai ya zamani na divai mpya,

ambavyo huondoa ufahamu

124:12 Yer 2:27; Ufu 17:2; Hab 2:19; Isa 44:20; Hes 15:39; Za 73:27wa watu wangu.

Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti

nao hujibiwa na fimbo ya mti.

Roho ya ukahaba imewapotosha,

hawana uaminifu kwa Mungu wao.

134:13 Isa 1:28; Hos 2:13; 10:9; Yer 2:20; Amo 7:17; Rum 1:28Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima

na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima,

chini ya mialoni, milibua na miela,

ambako kuna vivuli vizuri.

Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba

na wake za wana wenu uzinzi.

144:14 Mwa 38:21; Hos 9:10; Mit 10:21“Sitawaadhibu binti zenu wakati

wanapogeukia ukahaba,

wala wake za wana wenu

wanapofanya uzinzi,

kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya

na kutambikia pamoja na makahaba

wa mahali pa kuabudia miungu:

watu wasiokuwa na ufahamu

wataangamia!

154:15 Hos 9:15; 12:11; Amo 4:4; Yos 7:2“Ingawa umefanya uzinzi, ee Israeli,

Yuda naye asije akawa na hatia.

“Usiende Gilgali,

usipande kwenda Beth-Aveni4:15 Beth-Aveni maana yake Nyumba ya Ubatili (au Uovu), jina lingine la Betheli kwa dhihaka.

Wala usiape,

‘Hakika kama Bwana aishivyo!’

164:16 Isa 5:17; 7:25; Kut 32:9; Yer 31:18Waisraeli ni wakaidi,

kama mtamba wa ngʼombe ambaye ni mkaidi.

Ni jinsi gani basi Bwana anaweza kuwachunga

kama wana-kondoo

katika shamba la majani?

174:17 Mt 15:14Efraimu amejiunga na sanamu,

ondokana naye!

184:18 Mik 3:11; 7:3Hata wakati wamemaliza vileo vyao

wanaendelea na ukahaba wao,

watawala wao hupenda sana

njia za aibu.

194:19 Hos 12:11; 13:15; Isa 1:29Kisulisuli kitawafagilia mbali

na dhabihu zao zitawaletea aibu.