以西结书 8 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以西结书 8:1-18

圣城中的可憎之事

1第六年六月五日,我正在家中与犹大的众长老同坐,主耶和华的能力降在我身上。 2我观看,只见有一位形状像人,祂的腰部以下像火,腰部以上像闪亮的金属。 3祂好像伸出一只手,抓住我的头发。在异象中,灵把我举到天地之间,将我带到耶路撒冷圣殿内院的北门,那里供奉着惹耶和华愤恨的神像。 4我忽然看见那里有以色列上帝的荣耀,跟我在平原所见的一样。

5祂对我说:“人子啊,你举目北望。”于是,我举目朝北一望,见在祭坛门的北面有惹耶和华愤恨的神像。 6祂又对我说:“人子啊,你看见以色列人的所作所为了吗?他们在这里行那些极其可憎的事,以致我远离我的圣所。你会看到更可憎的事。”

7祂带我到院子的门口,我看见墙上有一个洞。 8祂对我说:“人子啊,你挖这墙。”我挖开墙后,看见一道门。 9祂对我说:“你进去看看他们在这里做的邪恶可憎的事吧。” 10我进去后,看见四周的墙上画满了各种爬虫、可憎的兽类和以色列人拜的神像。 11神像前面站着以色列的七十个长老,沙番的儿子雅撒尼亚也在当中,他们每人手中都拿着香炉,烟雾缭绕。 12祂又对我说:“人子啊,你看见以色列的长老在自己藏神像的房间里暗中所做的了吗?他们说,‘耶和华看不见我们,祂已经抛弃了这片土地。’” 13祂继续说:“你会看到他们做更可憎的事。”

14祂带我来到耶和华的殿外院的北门,看见一些妇女坐在那里为搭模斯神像哭泣。 15祂对我说:“人子啊,你看见了吗?你会看到更可憎的事。”

16祂带我来到耶和华殿的内院,在殿门口,走廊和祭坛中间约有二十五个人背向耶和华的殿,面向东方朝拜太阳。 17祂又对我说:“人子啊,你看见了吗?犹大人的这些可憎行径还算小事吗?他们到处行残暴之事,再三惹我发怒,手拿树枝举向鼻前祭拜偶像。 18因此,我必愤怒地对待他们,我必不顾惜他们,也不怜悯他们,即使他们大声向我呼求,我也不听。”

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 8:1-18

Ibada Ya Sanamu Hekaluni

18:1 2Fal 6:32; Eze 14:1; 33:31; 40:1; 24:1Katika siku ya tano ya mwezi wa sita mwaka wa sita, baada ya kupelekwa uhamishoni nilipokuwa nimeketi katika nyumba yangu na wazee wa Yuda walikuwa wameketi mbele yangu, mkono wa Bwana Mwenyezi ulikuja juu yangu. 28:2 Eze 1:4, 26-27; Dan 7:9Nikatazama, nikaona umbo mfano wa mwanadamu. Kutokana na kile kilichoonekana kuwa kiuno chake kuelekea chini alifanana na moto. Kuanzia kwenye kiuno kuelekea juu sura yake kama chuma kingʼaavyo kikiwa ndani ya moto. 38:3 Eze 3:12; 11:1; Kut 20:5; Kum 32:16; Yer 7:30; Kut 24:10; Eze 2:9Akanyoosha kitu kilichoonekana kama mkono, akaniinua kwa kushika nywele za kichwa changu. Roho akaniinua juu kati ya nchi na mbingu nikiwa katika maono ya Mungu akanichukua mpaka Yerusalemu, kwenye ingilio la lango la upande wa kaskazini ya ukumbi wa ndani, mahali iliposimama ile sanamu ichocheayo wivu. 48:4 Kut 24:16; Eze 1:28; 3:22Hapo mbele yangu palikuwa na utukufu wa Mungu wa Israeli, kama utukufu ule niliouona katika maono kule ua wa ndani.

58:5 Za 78:58-60; Yer 4:1; 32:34Kisha akaniambia, “Mwanadamu, tazama kuelekea kaskazini.” Hivyo nikatazama na kwenye ingilio upande wa kaskazini wa lango la madhabahu, nikaona sanamu hii ya wivu.

68:6 Eze 5:11; Kum 31:16; Hos 5:6Ndipo akaniambia, “Mwanadamu, je, unaona yale wanayofanya, haya mambo ya machukizo kabisa nyumba ya Israeli wanayotenda hapa, ambayo yatanifanya niende mbali na mahali pangu patakatifu? Lakini utaona vitu ambavyo vinachukiza zaidi hata kuliko hivi.”

7Kisha akanileta mpaka ingilio la ukumbi. Nikatazama, nami nikaona tundu ukutani. 8Akaniambia, “Mwanadamu, sasa toboa kwenye ukuta huu.” Ndipo nikatoboa ule ukuta, nikaona hapo pana mlango.

9Naye akaniambia, “Ingia ndani, ukaone maovu na machukizo wanayofanya humu.” 108:10 Kum 4:15-18; Yer 16:18; Amu 17:4-5; Eze 23:14; Yer 44:4; Kut 20:4Hivyo nikaingia ndani na kutazama, nikaona kuta zote zimechorwa kila aina ya vitu vitambaavyo na ya wanyama wachukizao wa kila aina na sanamu zote za nyumba ya Israeli. 118:11 Hes 16:17; Yer 26:24; Law 10:1; Hes 16:17-35; Kut 3:16; Eze 11:1-2Mbele yao walisimama wazee sabini wa nyumba ya Israeli, naye Yaazania mwana wa Shafani alikuwa amesimama miongoni mwao. Kila mmoja alikuwa na chetezo mkononi na moshi wa harufu nzuri ya uvumba ulikuwa unapanda juu.

128:12 2Fal 21:16; Za 10:11; Ay 22:13; Isa 29:15; Eze 9:9Akaniambia, “Mwanadamu, umeona wanayoyafanya wazee wa nyumba ya Israeli gizani, kila mmoja kwenye sehemu yake mwenyewe ya kufanyia ibada za sanamu yake? Wao husema, ‘Bwana hatuoni, Bwana ameiacha nchi.’ ” 13Akasema tena, “Bado utaona machukizo wanayofanya ambayo ni makubwa kuliko haya.”

148:14 Eze 11:12Ndipo akanileta mpaka ingilio la lango la kaskazini la nyumba ya Bwana, nami nikaona wanawake wameketi hapo, wakimwombolezea Tamuzi. 15Akaniambia, “Unaliona hili, mwanadamu? Utaona vitu ambavyo ni machukizo kuliko hili.”

168:16 Yoe 2:17; Kum 4:19; Ay 31:28; Mwa 1:16; Yer 2:27; Eze 40:6; 9:6Ndipo akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani wa nyumba ya Bwana, nako huko katika ingilio la Hekalu, kati ya baraza na madhabahu, walikuwepo wanaume wapatao ishirini na watano. Wakiwa wamelipa kisogo Hekalu la Bwana na kuelekeza nyuso zao upande wa mashariki, wakilisujudia jua huko mashariki.

178:17 Mwa 6:11; Ezr 9:6; Hes 11:33; 1Fal 14:9; Eze 16:2; 16:26Akaniambia, “Je, umeona hili mwanadamu? Je, ni jambo dogo sana kwa nyumba ya Yuda kufanya machukizo wanayoyafanya hapa? Je, ni lazima pia waijaze nchi dhuluma na kuendelea siku zote kunikasirisha? Watazame wanavyonibania pua kana kwamba ninanuka! 188:18 Yer 13:14; 44:6; Eze 24:14; Isa 1:15; Mik 3:4; Mit 1:28; 1Sam 8:18; Isa 58:4; Eze 9:10Kwa hiyo nitashughulika nao kwa hasira, sitawaonea huruma wala kuwaachilia. Wajapopiga makelele masikioni mwangu, sitawasikiliza.”