以西结书 44 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以西结书 44:1-31

君王,利未人和祭司

1那人又把我带到圣殿外院的东门,门关闭着。 2耶和华对我说:“这门必须关闭,不可打开。没有人能从这门进入,因为以色列的上帝耶和华已从这门进入,所以这门必须关闭。 3只有君王可以坐在里面,在耶和华面前进食。他要从门廊进入,也要从原路出去。”

4他带我从北门来到殿前,我看见耶和华的荣光充满了祂的殿,我就俯伏在地。 5耶和华对我说:“人子啊,你要认真看,仔细听我讲有关圣殿的一切规矩和法则,记住所有的出入口。 6然后告诉那些叛逆的以色列人,‘主耶和华这样说,以色列人啊,你们行可憎的事,该够了吧! 7你们献上食物、脂肪和血的同时,竟将那些身心未受割礼的外族人领进我的圣所,亵渎我的殿,破坏我的约,使你们罪上加罪。 8你们自己不管理我的圣物,却把我的圣所给外人治理。

9“‘因此,主耶和华说,以色列人中身心未受割礼的外族人不可进入我的圣所。

10“‘以色列人走入歧途时,有些利未人也远离我、追随偶像,他们必须承担自己犯罪的后果。 11然而,他们仍要在我的圣殿供职,看管殿门,为百姓屠宰燔祭牲和其他祭牲,服侍他们。 12因为利未人带动以色列人拜偶像,使以色列人陷入罪中,所以我起誓,他们必承担自己犯罪的后果。这是主耶和华说的。 13他们不得走近我,不可做我的祭司,也不得走近我的圣物或至圣之物,他们必因自己的可憎行径蒙羞。 14然而,我要委派他们管理圣殿,办理殿中所有的事务。

15“‘以色列人走入歧途时,利未撒督的子孙仍然在我的圣所尽忠职守,因此他们可以接近我、事奉我,侍立在我面前,献上脂肪和祭牲的血。这是主耶和华说的。 16只有他们可以进入我的圣所,在我的桌前事奉我,遵行我的吩咐。 17他们从内院的门进入殿内供职的时候,要穿细麻布衣服,不可穿羊毛衣服。 18他们要戴细麻布头巾,穿细麻布裤子,不可穿使人容易出汗的衣服。 19他们出去外院见百姓的时候,必须脱下供职时穿的衣服,放在圣屋,穿上普通的衣服后再出去,免得通过圣衣把圣洁带到百姓身上。 20他们不可剃光头,也不可留长头发,只可修剪头发。 21祭司进入内院之前,不可喝酒。 22他们不可娶寡妇或被休的妇女为妻,只能娶以色列的处女或祭司的遗孀。 23他们要教导我的子民辨别圣与俗,洁净与不洁净。 24他们要审理诉讼之事,按我的律例断是非。他们必须按我定的律例和法度遵守一切节期,守安息日为圣日。 25他们不可走近死尸,免得玷污自己,除非死者是自己的父母、子女、弟兄或未出嫁的姊妹。 26祭司得到洁净后,要再等七天。 27他进入内院的圣所事奉时,要为自己献上赎罪祭,这是主耶和华说的。

28“‘祭司不可在以色列拥有自己的产业,因为我就是他们的产业。 29他们的食物是以色列人献上的素祭、赎罪祭和赎过祭。凡献给耶和华的都归他们, 30各种初熟的出产和各种供物都应归给祭司。你们将初熟的麦子磨成面给祭司,福气就必临到你们的家。 31无论是自然死亡的,还是被其他野兽咬死的禽兽,祭司都不可吃。

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 44:1-31

Mkuu, Walawi, Makuhani

144:1 Eze 43:1Ndipo yule mtu akanirudisha mpaka kwenye lango la nje la mahali Patakatifu, lile linaloelekea upande wa mashariki, nalo lilikuwa limefungwa. 244:2 Eze 43:4-5Bwana akaniambia, “Lango hili litabaki limefungwa. Haliruhusiwi kufunguliwa, wala hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kuingilia kwenye lango hili. Litabaki limefungwa kwa sababu Bwana, Mungu wa Israeli, ameingia kwa kupitia lango hili. 344:3 Zek 6:12; Kut 24:9-11; Eze 46:2-8Yeye aliye mkuu peke yake ndiye anayeweza kukaa penye njia ya hilo lango na kula chakula mbele za Bwana. Itampasa aingie kwa njia hiyo ya lango la ukumbini na kutokea njia iyo hiyo.”

444:4 Isa 6:4; Ufu 15:8; Eze 1:28; Dan 8:17; Eze 40:35; 10:4Kisha yule mtu akanileta kwa njia ya lango la kaskazini mpaka mbele ya Hekalu. Nikatazama nami nikauona utukufu wa Bwana ukilijaza Hekalu la Bwana, nami nikaanguka kifudifudi.

544:5 Eze 40:4; 43:10-11; 42:9Bwana akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa uangalifu, usikilize kwa bidii na uzingatie kila kitu ninachokuambia kuhusu masharti yote yanayohusu Hekalu la Bwana. Uwe mwangalifu kuhusu wale wanaoruhusiwa hekaluni na wale wasioruhusiwa kuingia mahali patakatifu. 644:6 Eze 3:19Iambie nyumba ya kuasi ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Matendo yenu ya machukizo yatosha, ee nyumba ya Israeli! 744:7 Law 26:4; Mwa 17:14; Kut 12:48; Mdo 21:28; Law 22:25Zaidi ya matendo yenu yote ya machukizo, mmewaleta wageni wasiotahiriwa mioyo na miili katika patakatifu pangu, mkilinajisi Hekalu langu, huku mkinitolea chakula, mafuta ya wanyama na damu, nanyi mmevunja Agano langu. 844:8 Law 22:2; Hes 18:7; 2Tim 4:1Badala ya kutimiza wajibu wenu kuhusiana na vitu vyangu vitakatifu, mmeweka watu wengine kuwa viongozi katika patakatifu pangu. 944:9 Yoe 3:17; Zek 14:21Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakuna mgeni asiyetahiriwa moyo na mwilini anayeruhusiwa kuingia patakatifu pangu, wala hata wageni wanaoishi miongoni mwa Waisraeli.

1044:10 Neh 9:34; 2Fal 23:8; Za 95:10; Hes 18:23“ ‘Walawi walioniacha wakati Waisraeli walipopotoka wakatoka kwangu na kutangatanga kwa kufuata sanamu zao, watachukua adhabu ya dhambi zao. 1144:11 2Nya 29:34; Hes 16:9; 1Nya 26:12-19; Hes 3:5-37Wanaweza wakatumika katika mahali patakatifu pangu, wakiwa na uangalizi wa malango ya Hekalu, nao watachinja sadaka za kuteketezwa na dhabihu kwa ajili ya watu na kusimama mbele ya watu ili kuwahudumia. 1244:12 2Fal 16:10-16; Yer 14:10; Za 106:26; Yer 18:15Lakini kwa sababu waliwatumikia watu mbele ya sanamu zao na kuifanya nyumba ya Israeli ianguke kwenye dhambi, kwa hiyo nimeapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba ni lazima wachukue matokeo ya dhambi yao, asema Bwana Mwenyezi. 1344:13 Eze 16:6; Hes 18:3; Hos 5:1Hawaruhusiwi kukaribia ili kunitumikia kama makuhani wala kukaribia chochote changu kilicho kitakatifu au sadaka iliyo takatifu kupita zote, bali watachukua aibu ya matendo yao ya kuchukiza. 1444:14 1Sam 2:36; 2Fal 23:9; 1Nya 23:28-32Lakini nitawaweka katika uangalizi wa Hekalu na kazi zote zile zinazotakiwa kufanyika ndani yake.

1544:15 Yer 33:18; Zek 3:7; Kum 10:8; 2Sam 8:17; Eze 7:2; Kum 29:13; Eze 40:46“ ‘Lakini makuhani, ambao ni Walawi na wazao wa Sadoki, ambao walitimiza wajibu wao kwa uaminifu katika patakatifu pangu wakati Waisraeli walipopotoka, watakaribia ili kutumika mbele zangu. Itawapasa wasimame mbele zangu ili kutoa dhabihu za mafuta ya wanyama na damu, asema Bwana Mwenyezi. 1644:16 Eze 41:22; 1Sam 2:35; Mal 2:7; Law 3:16-17; Hes 8:15; Law 17:5-6Wao peke yao ndio wenye ruhusa ya kuingia mahali patakatifu pangu. Wao peke yao ndio watakaokaribia meza yangu ili kuhudumu mbele zangu na kufanya utumishi wangu.

1744:17 Kut 39:27-28; Ufu 19:8“ ‘Watakapoingia kwenye malango ya ukumbi wa ndani, watavaa nguo za kitani safi, hawaruhusiwi kamwe kuvaa mavazi ya sufu wakati wanapokuwa wakihudumu kwenye malango ya ukumbi wa ndani wala ndani ya Hekalu. 1844:18 Kut 28:39; Isa 3:20; Law 16:4; Kut 28:42Watavaa vilemba vya kitani safi vichwani mwao na nguo za ndani za kitani safi viunoni mwao. Hawatavaa chochote kitakachowafanya kutoa jasho. 1944:19 Law 6:27; Eze 46:20; Kut 39:27-29; Law 6:10-11Watakapotoka ili kuingia katika ukumbi wa nje mahali watu walipo, watavua nguo walizokuwa wakihudumu nazo na wataziacha katika vyumba vitakatifu nao watavaa nguo nyingine, ili kwamba wasije wakaambukiza watu utakatifu kwa njia ya mavazi yao.

2044:20 Law 21:5; Hes 6:5; Isa 28:7“ ‘Hawatanyoa nywele za vichwa vyao wala kuziacha ziwe ndefu, bali watazipunguza. 2144:21 Law 10:9Kuhani yeyote asinywe mvinyo aingiapo katika ukumbi wa ndani. 2244:22 Law 21:7Wasioe wanawake wajane wala walioachika, inawapasa kuoa wanawake bikira wenye heshima wa Israeli au wajane wa makuhani. 2344:23 Eze 22:26; Hag 2:11-13; Mal 2:7; Mwa 7:2; Law 13:50; Yer 15:19Watawafundisha watu wangu tofauti kati ya vitu vitakatifu na vitu vya kawaida na kuwaonyesha jinsi ya kupambanua kati ya vitu najisi na vitu safi.

2444:24 1Tim 4:5; 1Nya 23:4; 2Nya 19:8; Kum 17:8-9; 19:17“ ‘Katika magombano yoyote, makuhani watatumika kama mahakimu na kuamua hilo jambo kufuatana na sheria zangu. Watazishika sheria zangu na maagizo yangu katika sikukuu zangu zote zilizoamriwa, nao watatakasa Sabato zangu.

2544:25 Law 21:1-4“ ‘Kuhani asijitie unajisi kwa kukaribia maiti, lakini, kama mtu aliyekufa alikuwa baba yake au mama yake, mwana au binti yake, ndugu yake au dada ambaye hajaolewa, basi aweza kujitia unajisi kwa hao. 2644:26 Law 21:1-4; Hes 6:10Baada ya kujitakasa, atakaa hali hiyo kwa muda wa siku saba. 2744:27 Hes 3:28; 6:11; Law 4:28Siku atakapoingia katika ukumbi wa ndani wa mahali patakatifu ili kuhudumu, atatoa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe, asema Bwana Mwenyezi.

2844:28 Kum 10:9; Yos 13:33; Hes 18:20; Kum 18:1-2“ ‘Mimi nitakuwa ndio urithi pekee walio nao makuhani katika Israeli. Msiwape wao milki, mimi nitakuwa milki yao. 2944:29 Law 27:21; Hes 18:9, 14; Yos 13:14; Law 6:16Wao watakula sadaka za nafaka, sadaka za dhambi na sadaka za hatia na kila kitu kitakachotolewa kwa Bwana katika Israeli kitakuwa chao. 3044:30 Hes 18:12-13; 2Nya 31:5; Hes 15:18-21; Neh 10:35-37; 2Nya 30:10Yote yaliyo bora ya malimbuko ya vitu vyote na matoleo yenu maalum vitakuwa vya makuhani. Inawapasa kuwapa malimbuko ya kwanza ya unga wenu ili kwamba baraka ipate kuwa katika nyumba zenu. 3144:31 Kut 22:31; Law 22:8; 11:39-40Makuhani hawaruhusiwi kula chochote, ikiwa ni ndege au mnyama, aliyekutwa akiwa amekufa au aliyeraruliwa na wanyama pori.