Wafilipi 2:14-18
2:14 1Kor 10:10; 1Pet 4:9Fanyeni mambo yote bila kunungʼunika wala kushindana, 2:15 Mt 5:45, 48; Efe 5:1; Mdo 2:40ili msiwe na lawama wala hatia, bali mwe wana wa Mungu wasio na kasoro katika kizazi chenye ukaidi na kilichopotoka, ambacho ndani yake ninyi mnangʼaa kama mianga ulimwenguni. 2:16 1The 2:19Mkilishika neno la uzima, ili nipate kuona fahari siku ya Kristo kwamba sikupiga mbio wala kujitaabisha bure. 2:17 2Tim 4:6; Rum 15:16Lakini hata kama nikimiminwa kama sadaka ya kinywaji kwenye dhabihu na huduma itokayo katika imani yenu, mimi ninafurahi na kushangilia pamoja nanyi nyote. 2:18 Flp 3:1; 4:4Vivyo hivyo, ninyi nanyi imewapasa kufurahi na kushangilia pamoja nami.