Job 10 – NIV & NEN

New International Version

Job 10:1-22

1“I loathe my very life;

therefore I will give free rein to my complaint

and speak out in the bitterness of my soul.

2I say to God: Do not declare me guilty,

but tell me what charges you have against me.

3Does it please you to oppress me,

to spurn the work of your hands,

while you smile on the plans of the wicked?

4Do you have eyes of flesh?

Do you see as a mortal sees?

5Are your days like those of a mortal

or your years like those of a strong man,

6that you must search out my faults

and probe after my sin—

7though you know that I am not guilty

and that no one can rescue me from your hand?

8“Your hands shaped me and made me.

Will you now turn and destroy me?

9Remember that you molded me like clay.

Will you now turn me to dust again?

10Did you not pour me out like milk

and curdle me like cheese,

11clothe me with skin and flesh

and knit me together with bones and sinews?

12You gave me life and showed me kindness,

and in your providence watched over my spirit.

13“But this is what you concealed in your heart,

and I know that this was in your mind:

14If I sinned, you would be watching me

and would not let my offense go unpunished.

15If I am guilty—woe to me!

Even if I am innocent, I cannot lift my head,

for I am full of shame

and drowned in10:15 Or and aware of my affliction.

16If I hold my head high, you stalk me like a lion

and again display your awesome power against me.

17You bring new witnesses against me

and increase your anger toward me;

your forces come against me wave upon wave.

18“Why then did you bring me out of the womb?

I wish I had died before any eye saw me.

19If only I had never come into being,

or had been carried straight from the womb to the grave!

20Are not my few days almost over?

Turn away from me so I can have a moment’s joy

21before I go to the place of no return,

to the land of gloom and utter darkness,

22to the land of deepest night,

of utter darkness and disorder,

where even the light is like darkness.”

Kiswahili Contemporary Version

Ayubu 10:1-22

Ayubu: Nayachukia Maisha Yangu

110:1 Hes 11:15; 1Sam 1:10; Ay 7:11; 9:18, 21; 1Fal 19:4“Nayachukia sana haya maisha yangu;

kwa hiyo nitatoa malalamiko yangu kwa wazi bila kujizuia,

nami nitanena kutokana na uchungu wa moyo wangu.

210:2 Ay 13:3; 40:1; Isa 3:13; Hos 4:1; 5:1; Mik 6:2; Rum 8:33Nitamwambia Mungu: Usinihukumu,

bali niambie una mashtaka gani dhidi yangu.

310:3 Ay 9:24; 22:18; 31:23; Mwa 1:26; Za 138:8; Isa 60:21; 64:8; Za 8:6; 95:6; 100:3Je, inakupendeza wewe kunionea,

kuikataa kwa dharau kazi ya mikono yako,

huku wewe ukitabasamu juu ya mipango ya waovu?

410:4 Mit 5:21; Yer 16:17; 1Sam 16:7; Ay 11:11; 14:16; Za 11:4; 33:15; Mit 15:3; Yer 11:20-23Je, wewe una macho ya kimwili?

Je, wewe huona kama mwanadamu aonavyo?

510:5 Za 102:24; 2Pet 3:8; Ay 36:26; Za 39:5; 90:2, 4Je, siku zako ni kama zile za mwanadamu,

au miaka yako ni kama ile ya mtu,

610:6 Ay 14:16ili kwamba utafute makosa yangu

na kuichunguza dhambi yangu;

710:7 Ay 10:15; 6:29; 11:4; 16:17; Kum 32:39ingawa wajua kuwa mimi sina hatia,

na hakuna awezaye kunitoa mkononi mwako?

810:8 Za 119:73; Isa 43:7; Mwa 2:7; 2Sam 14:14; Ay 30:15“Mikono yako ndiyo iliyoniumba na kunifanya.

Je, sasa utageuka na kuniangamiza?

910:9 Isa 29:16; 64:8; Mwa 2:7; Ay 7:21; 4:19Kumbuka kuwa ulinifinyanga kama udongo wa mfinyanzi.

Je, sasa utanifanya kuwa mavumbi tena?

10Je, wewe hukunimimina mimi kama maziwa,

na kunigandisha kama jibini,

1110:11 Za 139:13, 15ukanivika ngozi na nyama,

na kuniunga pamoja kwa mifupa na mishipa?

1210:12 Mwa 2:7; 24:12; 45:5; 1Pet 2:25Umenipa uhai na kunitendea wema,

katika uangalizi wako umeilinda roho yangu.

1310:13 Ay 23:13; Za 115:3“Lakini hili ndilo ulilolificha moyoni mwako,

nami ninajua kuwa hili lilikuwa katika nia yako:

1410:14 Kut 34:7; Ay 7:21; 13:27Kama nilifanya dhambi, ungekuwa umeniona,

wala usingeacha kosa langu lipite bila kuadhibiwa.

1510:15 Ay 9:13; 10:7; Isa 3:11; Za 25:18; 25:16Kama nina hatia, ole wangu!

Hata kama ningekuwa sina hatia,

siwezi kukiinua kichwa changu,

kwa kuwa nimejawa na aibu,

na kuzama katika mateso yangu.

1610:16 Yer 5:6; Hos 5:14; 1Sam 28:21; Isa 38:16; Za 7:2; 1Sam 17:38; Mao 3:10Kama nikiinua kichwa changu juu, unaninyatia kama simba,

na kuonyesha tena uwezo wa kutisha dhidi yangu.

1710:17 1Fal 21:10; Ay 16:8; Rut 1:21Wewe waleta mashahidi wapya dhidi yangu

na kuzidisha hasira yako juu yangu;

nazo nguvu zako zinanijia wimbi moja baada ya jingine.

1810:18 Ay 3:8; 3:26; Za 22:9; Mhu 4:2; 7:1“Kwa nini basi ulinitoa tumboni?

Ninatamani ningekufa kabla jicho lolote halijaniona.

1910:19 Ay 3:3; Yer 15:10Laiti nisingekuwako kamwe,

au ningekuwa nimechukuliwa moja kwa moja

kutoka tumboni kwenda kaburini!

2010:20 Mhu 6:12; Ay 7:16-19; 5:7; Za 39:13; Ay 9:25Je, siku zangu chache si zimekaribia kuisha?

Niachie ili niweze kupata muda mfupi wa kufurahi

2110:21 2Sam 12:23; Za 88:12; 23:4; Ay 3:13; Mhu 2:9kabla sijaenda mahali ambapo hakuna kurudi tena,

katika nchi ya giza na uvuli wa mauti,

2210:22 Ay 3:5; 1Sam 2:9nchi ya giza kuu sana,

yenye uvuli wa giza na machafuko,

mahali ambapo hata nuru ni giza.”