2 Kungaboken 11 – NUB & NEN

Swedish Contemporary Bible

2 Kungaboken 11:1-21

Atalja regerar i Juda

(2 Krön 22:10-12)

1När Atalja, Achasjas mor, såg att hennes son var död, bestämde hon sig för att förgöra hela kungahuset. 2Men Josheva, kung Jorams dotter och Achasjas syster, lyckades gömma undan Achasjas son Joash, just när kungasönerna skulle dödas. Hon gömde honom och hans sköterska för Atalja i ett sovrum, så att han inte dödades. 3Joash hölls gömd av henne i Herrens hus i sex år, medan Atalja regerade i landet.

Joash blir kung

(2 Krön 23:1-21)

4Under sjunde året skickade Jojada bud efter officerarna, karierna och livgardet och förde dem till Herrens hus. Han slöt ett förbund med dem och tog en ed av dem i Herrens hus. Sedan visade han dem kungens son.

5Han gav dem följande instruktioner: ”Så här ska ni göra: En tredjedel av er som går i tjänst på sabbaten har som uppgift att bevaka kungapalatset, 6en tredjedel att bevaka Surporten och en tredjedel porten bakom vakten. Ni ska hålla vakt vid huset i tur och ordning.11:6 Innebörden av versen är oklar i sammanhanget. 7De övriga två kompanierna, som i vanliga fall går av vakten på sabbaten, ska bevaka Herrens hus åt kungen. 8Ni ska ställa upp er runt kungen med vapen i hand. Den som försöker bryta sig igenom leden ska dödas. Ni ska stanna hos kungen vart han än går.”

9Officerarna gjorde som de blivit beordrade av prästen Jojada. Var och en tog sina män, både dem som gick på och dem som gick av sitt pass på sabbaten, och kom så till prästen Jojada. 10Sedan gav prästen Jojada officerarna de spjut och koger som hade tillhört kung David och fanns i Herrens hus. 11Vakterna ställde sig på sina poster, var och en med vapen i sin hand, runt omkring kungen, från templets södra sida till dess norra, framför altaret och tempelhuset.

12Sedan förde Jojada ut kungasonen, satte en krona på hans huvud, gav honom förbundsförordningarna11:12 Eller: kungainsignierna. och utropade honom till kung. De smorde honom, applåderade och ropade: ”Länge leve kungen!”

13När Atalja hörde folkets jubel, gick hon till dem som var i Herrens hus. 14Där fick hon se kungen stå bredvid en pelare, så som seden var, och bredvid honom officerarna och trumpetarna. Allt folket jublade och lät trumpeterna ljuda.

Då rev Atalja sönder sina kläder och ropade: ”Förräderi! Förräderi!”

15Prästen Jojada gav order till officerarna, som hade befälet över trupperna, och befallde: ”För ut henne bortom gången och om någon följer henne, ska han huggas ner med svärd.” Prästen hade nämligen sagt: ”Ni får inte döda henne i Herrens hus.”

16Då grep de henne och ledde ut henne till Hästporten i kungapalatset och dödade henne där.

17Jojada slöt sedan ett förbund mellan Herren och kungen och folket, att de skulle vara Herrens folk. Ett förbund mellan kungen och folket ingicks också. 18Hela folket begav sig sedan till Baals tempel, rev ner det och bröt sönder altarna och gudabilderna och dödade Mattan, Baals präst, framför altarna. Prästen Jojada placerade sedan vakter vid Herrens hus. 19Sedan tog han med sig officerarna, karierna, livgardet och allt folket och ledde kungen från Herrens hus, förbi vakthuset och in i palatset, och kungen satte sig på sin tron.

20Allt folket i landet gladde sig, och det blev lugnt i staden, när Atalja dödats med svärd i kungapalatset.

21Joash var sju år gammal när han blev kung i Juda.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 11:1-21

Athalia Na Yoashi

(2 Nyakati 22:10–23:21)

111:1 2Fal 8:18Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme. 211:2 2Fal 12:1Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, aliyekuwa pia dada yake Ahazia, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala na kumficha humo ili Athalia asimwone; kwa hiyo hakuuawa. 3Alibaki amefichwa pamoja na yaya wake katika Hekalu la Bwana kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.

411:4 2Fal 11:19Katika mwaka wa saba, Yehoyada akatumania wakuu wa vikundi vya mamia, na Wakari,11:4 Yaani Wakerethi (ona 1Sam 30:14; Eze 25:16; Sef 2:5, 6). na walinzi, nao wakaletwa kwake katika Hekalu la Bwana. Alifanya agano nao na kuwaapisha katika Hekalu la Bwana. Ndipo akawaonyesha mwana wa mfalme. 511:5 1Nya 9:25Akawaamuru akisema, “Hivi ndivyo iwapasavyo kufanya: Ninyi ambao mko makundi matatu mnaoingia zamu siku ya Sabato, theluthi yenu inayolinda jumba la kifalme, 6theluthi nyingine Lango la Suri, na theluthi nyingine lango lililo nyuma ya walinzi, ambao hupeana zamu kulinda Hekalu, 7nanyi ambao mko katika makundi mengine mawili ambao kwa kawaida hupumzika Sabato, wote mtalinda Hekalu kwa ajili ya mfalme. 8Jipangeni kumzunguka mfalme, kila mtu akiwa na silaha yake mkononi. Yeyote anayesogelea safu zenu lazima auawe. Kaeni karibu na mfalme popote aendapo.”

9Wakuu wa vikosi vya mamia wakafanya kama vile kuhani Yehoyada aliagiza. Kila mmoja akawachukua watu wake, wale waliokuwa wakiingia zamu siku ya Sabato na wale waliokuwa wakienda mapumziko, nao wakaja kwa kuhani Yehoyada. 1011:10 2Sam 8:7Ndipo akawapa wale wakuu mikuki na ngao zilizokuwa za Mfalme Daudi, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana. 11Wale walinzi, kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, wakajipanga kumzunguka mfalme, karibu na madhabahu na Hekalu, kuanzia upande wa kusini hadi upande wa kaskazini mwa Hekalu.

1211:12 Kut 25:16; 1Sam 10:24; Isa 55:12Yehoyada akamtoa mwana wa mfalme na kumvika taji, akampa nakala ya agano, na kumtangaza kuwa mfalme. Wakamtia mafuta, nao watu wakapiga makofi na kupaza sauti, wakisema, “Mfalme aishi maisha marefu!”

13Athalia aliposikia kelele iliyofanywa na walinzi pamoja na watu, akawaendea watu pale penye Hekalu la Bwana. 1411:14 1Fal 1:39; Mwa 37:29; 2Fal 9:23Akaangalia, na tazama alikuwako mfalme, akiwa amesimama karibu na nguzo, kama ilivyokuwa desturi. Maafisa na wapiga tarumbeta walikuwa pembeni mwa mfalme, nao watu wote wa nchi walikuwa wakifurahi na kupiga tarumbeta. Ndipo Athalia akararua mavazi yake na kulia, “Uhaini! Uhaini!”

15Kuhani Yehoyada akawaagiza majemadari wa vikosi vya mamia, waliokuwa viongozi wa jeshi, “Mleteni nje kati ya safu, na mkamuue kwa upanga yeyote anayemfuata.” Kwa kuwa kuhani alikuwa amesema, “Hatauawa ndani ya Hekalu la Bwana.” 16Basi wakamkamata Athalia, na alipofika mahali ambapo farasi huingilia katika viwanja vya jumba la mfalme, wakamuulia hapo.

1711:17 Kut 24:8; Yer 34:8Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Bwana na mfalme na watu kwamba watakuwa watu wa Bwana. Akafanya pia agano kati ya mfalme na watu. 1811:18 Kum 12:3; 1Fal 18:40; 2Fal 10:25Watu wote wa nchi wakaenda kwenye hekalu la Baali na kulibomoa. Wakavunjavunja madhabahu na sanamu, na kumuua Matani kuhani wa Baali mbele ya hayo madhabahu.

Kisha Yehoyada kuhani akawaweka walinzi kwenye Hekalu la Bwana. 1911:19 2Fal 11:4Pamoja naye akawachukua majemadari wa mamia, Wakari, walinzi na watu wote wa nchi, nao kwa pamoja wakamteremsha mfalme kutoka Hekalu la Bwana na kwenda kwenye jumba la mfalme, wakiingilia njia ya lango la walinzi. Ndipo mfalme akachukua nafasi yake kwenye kiti cha enzi, 2011:20 Mit 11:10nao watu wote wa nchi wakafurahi. Mji ukatulia, kwa sababu Athalia alikuwa ameuawa kwa upanga nyumbani kwa mfalme.

21Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala.