Zechariah 5 – NIVUK & NEN

New International Version – UK

Zechariah 5:1-11

The flying scroll

1I looked again, and there before me was a flying scroll.

2He asked me, ‘What do you see?’

I answered, ‘I see a flying scroll, twenty cubits long and ten cubits wide.5:2 That is, about 9 metres long and 4.5 metres wide

3And he said to me, ‘This is the curse that is going out over the whole land; for according to what it says on one side, every thief will be banished, and according to what it says on the other, everyone who swears falsely will be banished. 4The Lord Almighty declares, “I will send it out, and it will enter the house of the thief and the house of anyone who swears falsely by my name. It will remain in that house and destroy it completely, both its timbers and its stones.” ’

The woman in a basket

5Then the angel who was speaking to me came forward and said to me, ‘Look up and see what is appearing.’

6I asked, ‘What is it?’

He replied, ‘It is a basket.’ And he added, ‘This is the iniquity5:6 Or appearance of the people throughout the land.’

7Then the cover of lead was raised, and there in the basket sat a woman! 8He said, ‘This is wickedness,’ and he pushed her back into the basket and pushed its lead cover down on it.

9Then I looked up – and there before me were two women, with the wind in their wings! They had wings like those of a stork, and they lifted up the basket between heaven and earth.

10‘Where are they taking the basket?’ I asked the angel who was speaking to me.

11He replied, ‘To the country of Babylonia5:11 Hebrew Shinar to build a house for it. When the house is ready, the basket will be set there in its place.’

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zekaria 5:1-11

Maono Ya Sita: Kitabu Kinachoruka

15:1 Za 10:7; Yer 36:4Nikatazama tena: na hapo mbele yangu kulikuwa na kitabu kilichoruka!

25:2 Yer 1:13Akaniuliza, “Unaona nini?”

Nikamjibu, “Naona kitabu kinachoruka chenye, urefu wa dhiraa ishirini5:2 Dhiraa 20 ni sawa na mita 9. na upana wa dhiraa kumi.”5:2 Dhiraa 10 ni sawa mita 4.5.

35:3 Mal 3:9; Kut 20:15; 20:7; Isa 48:1Akaniambia, “Hii ni laana inayotoka kwenda juu ya nchi yote, kwa kuwa kufuatana na yale yaliyoandikwa katika upande mmoja, kila mwizi atafukuziwa mbali, pia kufuatana na yaliyo upande wa pili, kila aapaye kwa uongo atafukuziwa mbali. 45:4 Zek 8:17; Law 14:34-35; Mit 3:33; Hab 2:9-11; Mal 3:5Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, ‘Nitaituma hiyo laana, nayo itaingia katika nyumba ya mwizi na nyumba ya huyo aapaye kwa uongo kwa Jina langu. Itabaki katika nyumba yake na kuiharibu, pamoja na mbao zake na mawe yake.’ ”

Maono Ya Saba: Mwanamke Ndani Ya Kikapu

55:5 Mik 6:10Kisha yule malaika aliyekuwa akizungumza nami akanijia na kuniambia, “Tazama juu uone ni nini kile kinachojitokeza.”

6Nikamuuliza, “Ni kitu gani?”

Akanijibu, “Ni kikapu cha kupimia.” Kisha akaongeza kusema, “Huu ni uovu wa watu katika nchi nzima.”

7Kisha kifuniko kilichotengenezwa kwa madini ya risasi kilichokuwa kimefunika kile kikapu, kiliinuliwa na ndani ya kile kikapu alikuwako mwanamke ameketi! 85:8 Mit 6:11Akasema, “Huu ni uovu,” tena akamsukumia ndani ya kikapu na kushindilia kifuniko juu ya mdomo wa kikapu.

95:9 Law 11:19Kisha nikatazama juu: na pale mbele yangu, walikuwepo wanawake wawili, wakiwa na upepo katika mabawa yao! Walikuwa na mabawa kama ya korongo, nao wakainua kile kikapu na kuruka nacho kati ya mbingu na nchi.

10Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Wanakipeleka wapi hicho kikapu?”

115:11 Mwa 10:10; Yer 29:5, 28; Dan 1:2Akanijibu, “Wanakipeleka katika nchi ya Babeli na kujenga nyumba kwa ajili yake. Itakapokuwa tayari, kikapu kitawekwa pale mahali pake.”