Numbers 28 – NIV & NEN

New International Version

Numbers 28:1-31

Daily Offerings

1The Lord said to Moses, 2“Give this command to the Israelites and say to them: ‘Make sure that you present to me at the appointed time my food offerings, as an aroma pleasing to me.’ 3Say to them: ‘This is the food offering you are to present to the Lord: two lambs a year old without defect, as a regular burnt offering each day. 4Offer one lamb in the morning and the other at twilight, 5together with a grain offering of a tenth of an ephah28:5 That is, probably about 3 1/2 pounds or about 1.6 kilograms; also in verses 13, 21 and 29 of the finest flour mixed with a quarter of a hin28:5 That is, about 1 quart or about 1 liter; also in verses 7 and 14 of oil from pressed olives. 6This is the regular burnt offering instituted at Mount Sinai as a pleasing aroma, a food offering presented to the Lord. 7The accompanying drink offering is to be a quarter of a hin of fermented drink with each lamb. Pour out the drink offering to the Lord at the sanctuary. 8Offer the second lamb at twilight, along with the same kind of grain offering and drink offering that you offer in the morning. This is a food offering, an aroma pleasing to the Lord.

Sabbath Offerings

9“ ‘On the Sabbath day, make an offering of two lambs a year old without defect, together with its drink offering and a grain offering of two-tenths of an ephah28:9 That is, probably about 7 pounds or about 3.2 kilograms; also in verses 12, 20 and 28 of the finest flour mixed with olive oil. 10This is the burnt offering for every Sabbath, in addition to the regular burnt offering and its drink offering.

Monthly Offerings

11“ ‘On the first of every month, present to the Lord a burnt offering of two young bulls, one ram and seven male lambs a year old, all without defect. 12With each bull there is to be a grain offering of three-tenths of an ephah28:12 That is, probably about 11 pounds or about 5 kilograms; also in verses 20 and 28 of the finest flour mixed with oil; with the ram, a grain offering of two-tenths of an ephah of the finest flour mixed with oil; 13and with each lamb, a grain offering of a tenth of an ephah of the finest flour mixed with oil. This is for a burnt offering, a pleasing aroma, a food offering presented to the Lord. 14With each bull there is to be a drink offering of half a hin28:14 That is, about 2 quarts or about 1.9 liters of wine; with the ram, a third of a hin28:14 That is, about 1 1/3 quarts or about 1.3 liters; and with each lamb, a quarter of a hin. This is the monthly burnt offering to be made at each new moon during the year. 15Besides the regular burnt offering with its drink offering, one male goat is to be presented to the Lord as a sin offering.28:15 Or purification offering; also in verse 22

The Passover

16“ ‘On the fourteenth day of the first month the Lord’s Passover is to be held. 17On the fifteenth day of this month there is to be a festival; for seven days eat bread made without yeast. 18On the first day hold a sacred assembly and do no regular work. 19Present to the Lord a food offering consisting of a burnt offering of two young bulls, one ram and seven male lambs a year old, all without defect. 20With each bull offer a grain offering of three-tenths of an ephah of the finest flour mixed with oil; with the ram, two-tenths; 21and with each of the seven lambs, one-tenth. 22Include one male goat as a sin offering to make atonement for you. 23Offer these in addition to the regular morning burnt offering. 24In this way present the food offering every day for seven days as an aroma pleasing to the Lord; it is to be offered in addition to the regular burnt offering and its drink offering. 25On the seventh day hold a sacred assembly and do no regular work.

The Festival of Weeks

26“ ‘On the day of firstfruits, when you present to the Lord an offering of new grain during the Festival of Weeks, hold a sacred assembly and do no regular work. 27Present a burnt offering of two young bulls, one ram and seven male lambs a year old as an aroma pleasing to the Lord. 28With each bull there is to be a grain offering of three-tenths of an ephah of the finest flour mixed with oil; with the ram, two-tenths; 29and with each of the seven lambs, one-tenth. 30Include one male goat to make atonement for you. 31Offer these together with their drink offerings, in addition to the regular burnt offering and its grain offering. Be sure the animals are without defect.

Kiswahili Contemporary Version

Hesabu 28:1-31

Sadaka Za Kila Siku

(Kutoka 29:38-46)

1Bwana akamwambia Mose, 228:2 Law 23:1-44; 3:11; 1:9; Mal 1:7-12“Wape Waisraeli agizo hili na uwaambie: ‘Hakikisheni kwamba mnaniletea mimi kwa wakati uliowekwa chakula kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, kama harufu nzuri ya kupendeza.’ 328:3 Kut 12:3; 29:38; Amo 4:4; Kut 29:38Waambie: ‘Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto mnayomtolea Bwana: wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasio na dosari, kama sadaka ya kawaida ya kuteketezwa kila siku. 428:4 Kut 29:39; 12:6Andaa mwana-kondoo mmoja asubuhi na mwingine jioni, 528:5 Hes 29:6; Law 6:20; 2:1; Kut 16:36; 29:38-42; Hes 15:4kila mmoja atolewe pamoja na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi ya efa28:5 Sehemu ya kumi ya efa ni sawa na kilo moja. ya unga laini uliochanganywa pamoja na robo ya hini28:5 Robo ya hini ni sawa na lita moja. ya mafuta ya zeituni. 628:6 Law 1:3; Kut 19:3; Law 1:9Hii ni sadaka ya kawaida ya kuteketezwa iliyoanzishwa katika Mlima Sinai kama harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto. 728:7 Hes 6:15; Law 10:9; 3:7; Hes 3:28; Kut 29:42; 30:9; Law 23:13; Hes 15:5-10; Isa 57:1Sadaka ya kinywaji itakayotolewa pamoja na kila mwana-kondoo ni robo ya hini ya kinywaji kilichochachuka. Mimina sadaka ya kinywaji kwa Bwana mahali patakatifu. 828:8 Kut 29:39; Law 23:7; 1:9Andaa yule mwana-kondoo wa pili jioni, pamoja na sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kama ulivyofanya kwa ile sadaka nyingine ya asubuhi. Hii ni sadaka iliyotolewa kwa kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.

Sadaka Za Sabato

928:9 Kut 20:10; Mt 12:5; Law 23:13; Eze 46:4; 40:4“ ‘Siku ya Sabato, utatoa sadaka ya wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari pamoja na sadaka yake ya kinywaji na sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu mbili za kumi za efa28:9 Sehemu mbili za kumi za efa ni sawa na kilo 2. za unga laini uliochanganywa na mafuta. 1028:10 Law 23:38; 1Sam 20:5; 1Nya 23:31; Neh 10:33; Isa 1:13-14; Eze 45:17; Hos 2:11; Kol 2:16Hii ni sadaka ya kuteketezwa itakayotolewa kwa ajili ya kila Sabato, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya kinywaji.

Sadaka Za Kila Mwezi

1128:11 Hes 10:10; 7:15; Law 5:15; 1:3“ ‘Siku ya kwanza ya kila mwezi, mtamletea Bwana sadaka ya kuteketezwa ya fahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasiokuwa na dosari. 1228:12 Hes 15:6; 29:3; 15:9Pamoja na kila fahali, kutakuwa na sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa,28:12 Sehemu tatu za kumi za efa ni sawa na kilo 3. uliochanganywa na mafuta, pamoja na kondoo dume mmoja, sadaka ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; 1328:13 Law 6:14; Hes 15:3; Law 1:9pamoja na kila mwana-kondoo, sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na mafuta. Hii ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri, sadaka ya kuteketezwa iliyotolewa kwa moto kwa Bwana. 1428:14 Hes 15:11; 2Nya 2:4; Eze 3:5Pamoja na kila fahali kutakuwa na sadaka ya kinywaji nusu ya hini28:14 Nusu ya hini ni sawa na lita 2. ya divai; pamoja na kila kondoo dume, theluthi moja ya hini,28:14 Theluthi moja ya hini ni sawa na lita 1.2. na pamoja na kila mwana-kondoo robo hini. Hii ni sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi itakayotolewa kila mwandamo wa mwezi kwa mwaka. 1528:15 Hes 4:3; 29:16Zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya kinywaji, mbuzi mmoja dume atatolewa kwa Bwana kama sadaka ya dhambi.

Pasaka

(Walawi 23:5-14)

1628:16 Kut 12:11; 2Nya 30:13; 35:1; Kut 12:6; Law 23:5; Lk 22:7“ ‘Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, itafanyika Pasaka ya Bwana. 1728:17 Kut 12:19; 12:15Katika siku ya kumi na tano ya mwezi huo itakuwa sikukuu; kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. 1828:18 Kut 12:16; Law 23:7Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, msifanye kazi za kawaida. 1928:19 Law 1:9; 22:20; Hes 29:8; Kum 15:21Leteni mbele za Bwana sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo dume saba wenye umri wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari. 2028:20 Law 14:10Pamoja na kila fahali, andaa sadaka ya nafaka sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa; 21pia pamoja na kila mmoja wa wale wana-kondoo saba, andaa sehemu ya kumi ya efa. 2228:22 Law 4:2; 8:3; Hes 15:28; Law 16:18; Rum 8:3; Gal 4:4; Ebr 9:12; 10:1Pia mtoe beberu mmoja kama sadaka ya dhambi ambaye atafanya upatanisho kwa ajili yenu. 23Andaa hizi licha ya zile sadaka za kawaida za kuteketezwa za kila asubuhi. 2428:24 Law 1:9; 2Kor 2:15; Efe 5:2Kwa njia hii andaa chakula cha sadaka ya kuteketezwa kila siku, kwa siku saba kama harufu nzuri impendezayo Bwana. Hii itaandaliwa licha ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji. 2528:25 Kut 12:16; 13:6; Law 23:8Siku ya saba mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.

Sikukuu Ya Majuma

(Walawi 23:15-22)

2628:26 Kut 34:2; 23:16; Law 23:10; Kum 16:10; Mit 3:9; Mdo 2:1“ ‘Siku ya malimbuko, mnapomletea Bwana sadaka ya nafaka mpya wakati wa Sikukuu ya Majuma, mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida. 2728:27 Law 23:18-19Mlete sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na pia wana-kondoo saba wenye umri wa mwaka mmoja, kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. 28Pamoja na kila fahali itatolewa sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini; 29na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba. 30Ongeza beberu mmoja kwa kufanya upatanisho kwa ajili yenu. 31Andaa hizi sadaka pamoja na sadaka zake za vinywaji, kuwa nyongeza ya sadaka za kawaida za kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya nafaka. Hakikisha kuwa wanyama hao hawana dosari.