Zekaria 5 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Zekaria 5:1-11

Maono Ya Sita: Kitabu Kinachoruka

15:1 Za 10:7; Yer 36:4Nikatazama tena: na hapo mbele yangu kulikuwa na kitabu kilichoruka!

25:2 Yer 1:13Akaniuliza, “Unaona nini?”

Nikamjibu, “Naona kitabu kinachoruka chenye, urefu wa dhiraa ishirini5:2 Dhiraa 20 ni sawa na mita 9. na upana wa dhiraa kumi.”5:2 Dhiraa 10 ni sawa mita 4.5.

35:3 Mal 3:9; Kut 20:15; 20:7; Isa 48:1Akaniambia, “Hii ni laana inayotoka kwenda juu ya nchi yote, kwa kuwa kufuatana na yale yaliyoandikwa katika upande mmoja, kila mwizi atafukuziwa mbali, pia kufuatana na yaliyo upande wa pili, kila aapaye kwa uongo atafukuziwa mbali. 45:4 Zek 8:17; Law 14:34-35; Mit 3:33; Hab 2:9-11; Mal 3:5Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, ‘Nitaituma hiyo laana, nayo itaingia katika nyumba ya mwizi na nyumba ya huyo aapaye kwa uongo kwa Jina langu. Itabaki katika nyumba yake na kuiharibu, pamoja na mbao zake na mawe yake.’ ”

Maono Ya Saba: Mwanamke Ndani Ya Kikapu

55:5 Mik 6:10Kisha yule malaika aliyekuwa akizungumza nami akanijia na kuniambia, “Tazama juu uone ni nini kile kinachojitokeza.”

6Nikamuuliza, “Ni kitu gani?”

Akanijibu, “Ni kikapu cha kupimia.” Kisha akaongeza kusema, “Huu ni uovu wa watu katika nchi nzima.”

7Kisha kifuniko kilichotengenezwa kwa madini ya risasi kilichokuwa kimefunika kile kikapu, kiliinuliwa na ndani ya kile kikapu alikuwako mwanamke ameketi! 85:8 Mit 6:11Akasema, “Huu ni uovu,” tena akamsukumia ndani ya kikapu na kushindilia kifuniko juu ya mdomo wa kikapu.

95:9 Law 11:19Kisha nikatazama juu: na pale mbele yangu, walikuwepo wanawake wawili, wakiwa na upepo katika mabawa yao! Walikuwa na mabawa kama ya korongo, nao wakainua kile kikapu na kuruka nacho kati ya mbingu na nchi.

10Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Wanakipeleka wapi hicho kikapu?”

115:11 Mwa 10:10; Yer 29:5, 28; Dan 1:2Akanijibu, “Wanakipeleka katika nchi ya Babeli na kujenga nyumba kwa ajili yake. Itakapokuwa tayari, kikapu kitawekwa pale mahali pake.”

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

撒迦利亞書 5:1-11

飛行的書卷

1我又舉目觀看,見有書卷在飛。 2天使問我:「你看見什麼?」我說:「我看見一本飛行的書卷,長九米,寬四米半。」 3他說:「這是臨到全天下的咒詛,因為書卷一面寫著『凡偷盜的必被清除』,另一面寫著『凡起假誓的必被清除』。」 4萬軍之耶和華說:「我要使這咒詛進入盜賊和奉我的名起假誓者的家,留在他們家裡,直到毀滅一切,不留一木一石。」

量器中的女子

5與我說話的天使又來對我說:「你舉目觀看,看看出現了什麼?」 6我問道:「這是什麼?」他說:「這是一個量器。」接著他又說:「裡面盛著天下人的罪。」 7只見量器的鉛蓋打開了,裡面坐著一個女子。 8天使說:「這是罪惡。」他把女子推回量器中,蓋上鉛蓋。 9我又舉目觀看,見有兩個女子展翅飛來,她們的翅膀像鸛鳥的翅膀。她們把量器提到空中。 10我問與我說話的天使:「她們要把量器帶到哪裡?」 11他說:「要帶到示拿5·11 「示拿」巴比倫的別名。,在那裡為它建造房屋,建好後就把它安置在底座上。」