Zekaria 3 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zekaria 3:1-10

Maono Ya Nne: Mavazi Safi Kwa Ajili Ya Kuhani Mkuu

13:1 Ezr 2:2; Zek 6:11; 2Sam 24:1; 2Nya 18:21; Za 109:6; Mt 4:10; Ay 1:6; Ufu 12:10Kisha akanionyesha Yoshua,3:1 Yoshua kwa Kiebrania ni Yeshua, maana yake ni Yehova ni wokovu. kuhani mkuu, akiwa amesimama mbele ya malaika wa Bwana, naye Shetani amesimama upande wake wa kuume ili amshtaki. 23:2 Yud 9, 23; Isa 14:1; 7:4; Za 109:31; Mt 4:10; Lk 22:31; Rum 16:20; 8:33; 11:5Bwana akamwambia Shetani, “Bwana akukemee Shetani! Bwana, ambaye ameichagua Yerusalemu, akukemee! Je, mtu huyu siyo kijinga kinachowaka kilichonyakuliwa kwenye moto?”

33:3 Isa 64:6Wakati huu, Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu alipokuwa amesimama mbele ya malaika. 43:4 2Sam 12:13; Eze 36:25; Mik 7:18; Mwa 41:42; Za 132:9; Ufu 19:8; Isa 52:1Malaika akawaambia wale waliokuwa wamesimama mbele yake, “Mvueni hizo nguo zake chafu.”

Kisha akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeiondoa dhambi yako, nami nitakuvika mavazi ya kitajiri.”

53:5 Kut 29:6Kisha nikasema, “Mvike kilemba kilicho safi kichwani mwake.” Kwa hiyo wakamvika kilemba safi kichwani na kumvika yale mavazi mengine, wakati malaika wa Bwana akiwa amesimama karibu.

6Malaika wa Bwana akamwamuru Yoshua: 73:7 Law 8:35; Kum 17:8-113:7 Eze 44:15-16; 2Nya 23:6; Yer 15:19; Zek 6:15“Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Ikiwa utakwenda katika njia zangu na kushika masharti yangu, basi utaitawala nyumba yangu na kuwa na amri juu ya nyua zangu, nami nitakupa nafasi miongoni mwa hawa wasimamao hapa.

83:8 Kum 28:46; Eze 12:11; Isa 4:2; 49:3“ ‘Sikiliza, ee Yoshua kuhani mkuu, pamoja na wenzako walioketi mbele yako, ambao ni watu walio ishara ya mambo yatakayokuja: Ninakwenda kumleta mtumishi wangu, Tawi. 9Tazama, jiwe nililoliweka mbele ya Yoshua! Kuna macho saba juu ya jiwe lile moja, nami nitachora maandishi juu yake,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitaiondoa dhambi ya nchi hii kwa siku moja.

103:10 Ay 11:18; Hes 16:14; 1Fal 4:25; Mik 4:4“ ‘Katika siku hiyo kila mmoja wenu atamwalika jirani yake akae chini ya mzabibu wake na mtini wake,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”

New International Reader’s Version

Zechariah 3:1-10

A Vision of the High Priest Dressed in Fine Clothes

1Then the Lord showed me Joshua the high priest. He was standing in front of the angel of the Lord. Satan was standing to the right of Joshua. He was there to bring charges against the high priest. 2The Lord said to Satan, “May the Lord correct you! He has chosen Jerusalem. So may he correct you! Isn’t this man Joshua like a burning stick pulled out of the fire?”

3Joshua stood in front of the angel. He was wearing clothes that were very dirty. 4The angel spoke to those who were standing near him. He said, “Take his dirty clothes off.”

He said to Joshua, “I have taken your sin away. I will put fine clothes on you.”

5I added, “Put a clean turban on his head.” So they did. And they dressed him while the angel of the Lord stood by.

6Then the angel spoke to Joshua. He said, 7“The Lord who rules over all says, ‘You must obey me. You must do what I have commanded. Then you will rule in my temple. You will be in charge of my courtyards. And I will give you a place among these who are standing here.

8“ ‘High Priest Joshua, pay attention! I want you other priests who are sitting with Joshua to listen also. All you men are signs of things to come. I am going to bring to you my servant the Branch. 9Look at the stone I have put in front of Joshua! There are seven eyes on that one stone. I will carve a message on it,’ says the Lord who rules over all. ‘And I will remove the sin of this land in one day.

10“ ‘At that time each of you will invite your neighbors to visit you. They will sit under your vines and fig trees,’ announces the Lord.”