Zaburi 87 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 87:1-7

Zaburi 87

Sifa Za Yerusalemu

Zaburi ya wana wa Kora. Wimbo.

187:1 Za 48:1Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;

287:2 Za 2:6Bwana anayapenda malango ya Sayuni

kuliko makao yote ya Yakobo.

387:3 Za 46:4; Isa 60:1Mambo matukufu yanasemwa juu yako,

ee mji wa Mungu:

487:4 Ay 9:13; 2Sam 8:1; Za 83:7; 45:12; Yoe 3:4; Isa 19:25“Nitaweka kumbukumbu ya Rahabu87:4 Rahabu hapa ni jina la ushairi la Misri. na Babeli

miongoni mwa wale wanaonikubali mimi:

Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi,87:4 Kushi hapa ina maana ya Naili ya juu, yaani Ethiopia.

nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’ ”

587:5 Eze 48:35; Mt 16:18Kuhusu Sayuni itasemwa hivi,

“Huyu na yule walizaliwa humo,

naye Aliye Juu Sana mwenyewe

atamwimarisha.”

687:6 Isa 4:3; Kut 32:32; Yer 3:19; Eze 13:9; Za 22:30; 69:28; Mal 3:16Bwana ataandika katika orodha ya mataifa:

“Huyu alizaliwa Sayuni.”

787:7 Za 149:3; 36:9Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba,

“Chemchemi zangu zote ziko kwako.”