Zaburi 73 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 73:1-28

KITABU CHA TATU

(Zaburi 73–89)

Zaburi 73

Haki Ya Mungu

Zaburi ya Asafu.

173:1 Za 24:4; 5:8Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli,

kwa wale ambao mioyo yao ni safi.

273:2 Kum 32:35; Za 69:2; Efe 4:27Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza;

nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.

373:3 Mit 3:31; 23:17; 24:1-2; Ay 9:24; 21:7; Yer 12:1; Mal 3:15Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna

nilipoona kufanikiwa kwa waovu.

4Wao hawana taabu,73:4 Tafsiri nyingine zinasema: hawana maumivu katika kufa kwao.

miili yao ina afya na nguvu.

573:5 Za 73:12; Eze 23:42Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine,

wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.

673:6 Law 26:19; Mwa 6:11; 41:42; Wim 4:9; Eze 16:11; Mit 4:17; Mhu 8:11Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao,

wamejivika jeuri.

773:7 Za 7:10Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi,

majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.

873:8 Za 10:7; 12:5; 41:5; Eze 25:15; Kol 3:8; 2Pet 2:18; Yud 16Hudhihaki na kusema kwa ukorofi,

katika majivuno yao wanatishia kutesa.

973:9 Ufu 13:6Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu,

nazo ndimi zao humiliki duniani.

10Kwa hiyo watu wao huwageukia

na kunywa maji tele.73:10 Au: na kupokea yote wasemayo.

1173:11 Ay 22:13; Za 94:7Wanasema, “Mungu awezaje kujua?

Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”

1273:12 Za 73:5; 49:6Hivi ndivyo walivyo waovu:

siku zote hawajali,

wanaongezeka katika utajiri.

1373:13 Ay 9:29-31; 21:15; Za 24:4; Mal 3:14; Mwa 44:16; Ebr 10:19-22Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure,

ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.

1473:14 Za 73:5Mchana kutwa nimetaabika,

nimeadhibiwa kila asubuhi.

15Kama ningesema, “Nitasema hivi,”

ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.

1673:16 Mhu 8:17Nilipojaribu kuelewa haya yote,

yalikuwa magumu kwangu kuelewa.

1773:17 Kut 15:17; Ay 8:13; Flp 3:19; Za 15:1; 77:13Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu,

ndipo nilipotambua mwisho wao.

1873:18 Kum 32:35; Za 35:6; 17:13Hakika unawaweka mahali pa utelezi,

unawaangusha chini kwa uharibifu.

1973:19 Kum 28:20; Mit 24:22; Isa 47:11; Mwa 19:15Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula,

wanatoweshwa kabisa na vitisho!

2073:20 Za 78:65; Isa 29:8; Ay 20:8; Mit 12:11; 28:19Kama ndoto mtu aamkapo,

hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana,

utawatowesha kama ndoto.

21Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa,

na roho yangu ilipotiwa uchungu,

2273:22 Za 49:10; 92:6; 49:12, 20; Mhu 3:18; 9:12nilikuwa mpumbavu na mjinga,

nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.

2373:23 Mwa 48:13Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote,

umenishika mkono wangu wa kuume.

2473:24 Za 48:14; 1Fal 22:5; Isa 58:8; Yn 14:3; 2Kor 5:1Unaniongoza kwa shauri lako,

hatimaye utaniingiza katika utukufu.

2573:25 Za 16:2; Flp 3:8Nani niliye naye mbinguni ila wewe?

Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.

2673:26 Kum 32:9; Za 18:1; 84:2; 31:10; 40:12Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa,

bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu

na fungu langu milele.

2773:27 Za 34:21; Law 6:2; Yer 5:11; Hos 4:12; 9:1Wale walio mbali nawe wataangamia,

unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.

2873:28 Sef 3:2; Yak 4:8; Za 40:5; 26:7; 9:9; Ebr 10:22Lakini kwangu mimi,

ni vyema kuwa karibu na Mungu.

Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu;

nami nitayasimulia matendo yako yote.

New International Version – UK

Psalms 73:1-28

Book III

Psalms 73–89

Psalm 73

A psalm of Asaph.

1Surely God is good to Israel,

to those who are pure in heart.

2But as for me, my feet had almost slipped;

I had nearly lost my foothold.

3For I envied the arrogant

when I saw the prosperity of the wicked.

4They have no struggles;

their bodies are healthy and strong.73:4 With a different word division of the Hebrew; Masoretic Text struggles at their death; / their bodies are healthy

5They are free from common human burdens;

they are not plagued by human ills.

6Therefore pride is their necklace;

they clothe themselves with violence.

7From their callous hearts comes iniquity73:7 Syriac (see also Septuagint); Hebrew Their eyes bulge with fat;

their evil imaginations have no limits.

8They scoff, and speak with malice;

with arrogance they threaten oppression.

9Their mouths lay claim to heaven,

and their tongues take possession of the earth.

10Therefore their people turn to them

and drink up waters in abundance.73:10 The meaning of the Hebrew for this verse is uncertain.

11They say, ‘How would God know?

Does the Most High know anything?’

12This is what the wicked are like –

always free of care, they go on amassing wealth.

13Surely in vain I have kept my heart pure

and have washed my hands in innocence.

14All day long I have been afflicted,

and every morning brings new punishments.

15If I had spoken out like that,

I would have betrayed your children.

16When I tried to understand all this,

it troubled me deeply

17till I entered the sanctuary of God;

then I understood their final destiny.

18Surely you place them on slippery ground;

you cast them down to ruin.

19How suddenly are they destroyed,

completely swept away by terrors!

20They are like a dream when one awakes;

when you arise, Lord,

you will despise them as fantasies.

21When my heart was grieved

and my spirit embittered,

22I was senseless and ignorant;

I was a brute beast before you.

23Yet I am always with you;

you hold me by my right hand.

24You guide me with your counsel,

and afterwards you will take me into glory.

25Whom have I in heaven but you?

And earth has nothing I desire besides you.

26My flesh and my heart may fail,

but God is the strength of my heart

and my portion for ever.

27Those who are far from you will perish;

you destroy all who are unfaithful to you.

28But as for me, it is good to be near God.

I have made the Sovereign Lord my refuge;

I will tell of all your deeds.