Zaburi 63
Shauku Kwa Ajili Ya Uwepo Wa Mungu
Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda.
163:1 Za 42:2; 84:2; 143:6Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu,
nakutafuta kwa moyo wote;
nafsi yangu inakuonea kiu,
mwili wangu unakuonea wewe shauku,
katika nchi kame na iliyochoka
mahali ambapo hapana maji.
263:2 Za 15:1; 27:4; 68:24; Kut 16:7; 1Nya 16:11Nimekuona katika mahali patakatifu
na kuuona uwezo wako na utukufu wako.
363:3 Isa 30:13; Yn 3:16; Za 36:7; 69:16; 106:45; 109:21Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai,
midomo yangu itakuadhimisha.
463:4 Za 28:3; 104:33; 146:2; Isa 38:20; 1Tim 2:8Nitakusifu siku zote za maisha yangu,
na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
563:5 Za 17:15; 36:8; Mt 5:6; Isa 25:6Nafsi yangu itatoshelezwa
kama kwa wingi wa vyakula;
kwa midomo iimbayo
kinywa changu kitakusifu wewe.
663:6 Kum 6:4-9; Za 119:148; 16:7; 140:5; Mt 14:25Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe,
ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.
763:7 Za 27:9; 118:7; Rum 2:12; Isa 26:9Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu,
chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
863:8 Hes 32:12; Hos 6:3; Isa 26:9; Za 41:12Nafsi yangu inaambatana nawe,
mkono wako wa kuume hunishika.
963:9 Za 40:14; 55:15; 71:20; 95:4; 139:15Wale wanaotafuta uhai wangu wataharibiwa,
watakwenda chini kwenye vilindi vya dunia.
1063:10 Yer 18:21; Eze 35:5; Amo 1:11; Mao 5:18Watatolewa wafe kwa upanga,
nao watakuwa chakula cha mbweha.
1163:11 Sef 1:5; Isa 19:18; 45:23; 65:16; Ay 5:16; Rum 3:19Bali mfalme atafurahi katika Mungu,
wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu,
bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.