Zaburi 59
Kuomba Ulinzi Wa Mungu
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Wakati Sauli alipotuma wapelelezi nyumbani mwa Daudi ili wamuue.
159:1 Za 82:259:1 Za 143:9; 20:1Ee Mungu, uniokoe na adui zangu,
unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu.
259:2 Za 14:4; 36:12; 53:4; 92:7; 94:16; 26:9; 139:19; Mit 29:10Uniponye na watu watendao mabaya,
uniokoe kutokana na wamwagao damu.
359:3 Za 56:6; 1Sam 26:18Tazama wanavyonivizia!
Watu wakali wananifanyia hila,
ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea
wala kutenda dhambi.
459:4 Za 13:3; 119:3; Mt 5:11Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia.
Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya!
559:5 Za 69:6; 80:4; 84:8; 44:23; 9:5; Isa 10:3; Yer 18:23; Dan 4:35Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli!
Zinduka uyaadhibu mataifa yote,
usionyeshe huruma kwa wasaliti.
659:6 Za 22:16Hurudi wakati wa jioni,
wakibweka kama mbwa,
wakiuzurura mji.
759:7 Za 55:21; 94:4; Mit 10:32; 12:23; 15:2, 28; Ay 22:13Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao,
hutema upanga kutoka midomo yao,
nao husema, “Ni nani atakayetusikia?”
859:8 Za 2:4; 37:13; Mit 1:26Lakini wewe, Bwana, uwacheke;
unayadharau mataifa hayo yote.
959:9 Za 18:1; 9:9; 18:2; 62:2; 71:3Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe,
wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
10Mungu wangu unipendaye.
Mungu atanitangulia,
naye atanifanya niwachekelee
wale wanaonisingizia.
1159:11 Kum 4:9; 6:12; Za 3:3; 84:9; 89:10; 106:27; 144:6; Isa 33:3; Mwa 4:12, 13Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu,
au sivyo watu wangu watasahau.
Katika uwezo wako wafanye watangetange
na uwashushe chini.
1259:12 Za 10:7; 64:8; Mit 10:14; 12:13; Isa 2:12; 5:15; Sef 3:11Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao,
kwa ajili ya maneno ya midomo yao,
waache wanaswe katika kiburi chao.
Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka,
1359:13 Za 83:18; 104:35wateketeze katika ghadhabu,
wateketeze hadi wasiwepo tena.
Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia
kwamba Mungu anatawala juu ya Yakobo.
14Hurudi jioni,
wakibweka kama mbwa,
wakiuzurura mji.
1559:15 Ay 15:23Wanatangatanga wakitafuta chakula,
wasipotosheka hubweka kama mbwa.
1659:16 Za 5:3; 88:13; 101:1; 108:1; 1Sam 2:10; 2Sam 22:3; Kum 4:30Lakini mimi nitaziimba nguvu zako,
asubuhi nitaimba juu ya upendo wako;
kwa maana wewe ndiwe ngome yangu
na kimbilio langu wakati wa shida.
1759:17 Za 59:1Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa.
Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
Mungu unipendaye.