Zaburi 57 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 57:1-11

Zaburi 57

Kuomba Msaada

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni.

157:1 Isa 26:20Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie,

kwa maana nafsi yangu inakukimbilia.

Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia

mpaka maafa yapite.

257:2 Za 138:8Namlilia Mungu Aliye Juu Sana,

Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.

357:3 Za 18:9, 16; 69:14; 142:5, 7; 56:1; 25:10; 40:11; 115:1Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa,

akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali;

Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.

457:4 Za 35:17; 55:21; 64:3; Mit 30:14Niko katikati ya simba,

nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu:

watu ambao meno yao ni mikuki na mishale,

ambao ndimi zao ni panga kali.

557:5 Za 108:5Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,

utukufu wako na uenee duniani kote.

657:6 Es 6:13; Za 31:4; 9:15; 140:5; 7:15; 38:6; 10:9; 145:14; Mit 28:10; Mhu 10:8Waliitegea miguu yangu nyavu,

nikainamishwa chini na dhiki.

Wamechimba shimo katika njia yangu,

lakini wametumbukia humo wao wenyewe.

757:7 Za 112:7; 108:1Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti;

nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.

857:8 Za 33:2; 149:3; 150:3; Amu 5:12Amka, nafsi yangu!

Amka, kinubi na zeze!

Nitayaamsha mapambazuko.

9Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa;

nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.

1057:10 Za 36:5; 108:4Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni,

uaminifu wako unazifikia anga.

1157:11 Za 8:1; 149:3; 150:3; Amu 5:12Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni,

utukufu wako na uwe duniani pote.