Zaburi 55 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 55:1-23

Zaburi 55

Maombi Ya Mtu Aliyesalitiwa Na Rafiki

Kwa mwimbishaji. Na ala za uimbaji. Utenzi wa Daudi.

155:1 Za 27:9; Mao 3:56Ee Mungu, sikiliza maombi yangu,

wala usidharau hoja yangu.

255:2 1Sam 1:15-16; Za 4:1; 77:3; 86:6-7; 142:2Nisikie na unijibu.

Mawazo yangu yananisumbua na nimehangaishwa

355:3 2Sam 16:6-8; 17:9; Za 143:3; 44:16; 71:11kwa sauti ya adui,

kwa kukaziwa macho na waovu,

kwa sababu wananiletea mateso juu yangu

na kunitukana kwa hasira zao.

455:4 Ay 18:11; Za 6:3; 102:3-5; Yn 12:27; Mt 26:37, 38; 2Kor 1:8-10Moyo wangu umejaa uchungu,

hofu ya kifo imenishambulia.

555:5 Ay 4:14; Eze 7:18; 2Kor 7:15; Isa 21:4; Kum 28:67; Yer 46:5; 49:5Woga na kutetemeka vimenizunguka,

hofu kuu imenigharikisha.

6Nilisema, “Laiti ningekuwa na mbawa za njiwa!

Ningeruka niende mbali kupumzika.

755:7 1Sam 23:14Ningalitorokea mbali sana

na kukaa jangwani,

855:8 Za 31:20; 77:18; Isa 4:6; 25:4; 28:2; 29:6; 32:2ningaliharakisha kwenda mahali pa salama,

mbali na tufani kali na dhoruba.”

955:9 Mwa 4:17; 11:9; Mdo 2:4; Za 11:5; Isa 59:6; Yer 6:7; Eze 7:11; Hab 1:3Ee Bwana, uwatahayarishe waovu

na uwachanganyishie semi zao,

maana nimeona jeuri na ugomvi mjini.

1055:10 1Pet 5:8Usiku na mchana wanazunguka juu ya kuta zake,

uovu na dhuluma vimo ndani yake.

1155:11 Za 5:9; 10:7Nguvu za uharibifu zinatenda kazi mjini,

vitisho na uongo haviondoki mitaani mwake.

12Kama aliyenitukana ni adui yangu, ningevumilia,

kama mtu mwovu angejiinua dhidi yangu,

ningejificha asinione.

1355:13 2Sam 15:12Kumbe ni wewe, mwenzangu,

mshiriki na rafiki yangu wa karibu,

1455:14 Mdo 1:16-17; Za 42:4ambaye awali tulifurahia ushirika mzuri,

tulipokuwa tukienda na umati hekaluni mwa Mungu.

1555:15 Za 64:7; 49:14; Mit 6:5; Isa 29:5; 47:9, 11; 1The 5:3; Hes 16:30Kifo na kiwajie adui zangu ghafula,

na washuke kuzimu wangali hai,

kwa maana uovu upo ndani yao.

16Lakini ninamwita Mungu,

naye Bwana huniokoa.

1755:17 Za 141:2; 88:13; 92:2; 5:3; Mdo 3:1; 10:9; 10:3, 30; Lk 18:1; Dan 6:10Jioni, asubuhi na adhuhuri

ninalia kwa huzuni,

naye husikia sauti yangu.

1855:18 2Nya 32:7Huniokoa nikawa salama katika vita

vilivyopangwa dhidi yangu,

ingawa watu wengi hunipinga.

1955:19 Kum 33:27; Za 29:10; 78:59; 36:1; 64:4; Kut 15:18Mungu anayemiliki milele,

atawasikia na kuwaadhibu,

watu ambao hawabadilishi njia zao,

wala hawana hofu ya Mungu.

2055:20 Za 7:4; 41:9Mwenzangu hushambulia rafiki zake,

naye huvunja agano lake.

2155:21 Za 59:7; 57:4; 12:2; 64:3; Ufu 1:16; Mit 5:3; 6:24; 12:18Mazungumzo yake ni laini kama siagi,

hata hivyo vita vimo moyoni mwake.

Maneno yake ni mororo kuliko mafuta,

hata hivyo ni upanga mkali uliofutwa.

2255:22 1Pet 5:7; Za 15:5; 18:35; 112:6; 21:7; 37:24; Mt 6:25-34Mtwike Bwana fadhaa zako,

naye atakutegemeza,

hatamwacha kamwe mwenye haki wake aanguke.

2355:23 Za 5:6; 11:1; 9:15; 73:18; 94:13; 25:2; 30:3; 56:3; Isa 14:15; Eze 28:8; Lk 8:31; Ay 15:32Lakini wewe, Ee Mungu,

utawashusha waovu katika shimo la uharibifu.

Wenye kiu ya kumwaga damu na wenye hila,

hawataishi nusu ya siku zao.

Lakini mimi ninakutumaini wewe.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

詩篇 55:1-23

第55篇

被朋友出賣者的禱告

大衛作的訓誨詩,交給樂長,用弦樂器。

1上帝啊,

求你垂聽我的禱告,

不要對我的呼求置之不理。

2求你垂聽、應允我的呼求。

我思緒煩亂,坐立不安。

3仇敵向我咆哮,

惡人迫害我。

他們帶給我苦難,

怒氣沖沖地攻擊我。

4我內心悲痛,

被死亡的恐怖籠罩。

5我嚇得渾身顫慄,驚恐不已。

6我說:「但願我像鴿子一樣有翅膀,

我好飛去,得享安息。

7我要飛到遠方,宿在曠野。(細拉)

8我要趕快躲進避難所,

避過暴雨狂風。」

9主啊,

我在城中看見暴力和爭鬥,

求你使他們言語混亂。

10他們晝夜在城牆上出沒,

城內充滿了邪惡和壓迫,

11毀壞的勢力在城內肆虐,

恐嚇與欺詐遍佈街市。

12倘若是仇敵辱罵我,

我還能忍受;

倘若是恨我的人欺凌我,

我還可以躲開。

13可是,竟然是你,我志同道合的夥伴,我的摯友!

14從前我們情誼深厚,

與眾人同去上帝的殿。

15願死亡突然抓住我的仇敵,

願他們活活地下陰間,

因為他們的內心和家中罪惡充斥。

16但我要呼求上帝,

耶和華必拯救我。

17晚上、早晨和中午,

我痛苦地呼求,

祂必垂聽我的聲音。

18雖然許多人攻擊我,

祂必救我平安脫險。

19永掌王權的上帝必鑒察並懲罰他們,

因為他們頑固不化、不敬畏上帝。

20我的同伴違背盟約,出手攻擊朋友。

21他口蜜腹劍,笑裡藏刀。

22把你的重擔卸給耶和華,

祂必扶持你。

祂絕不讓義人跌倒。

23上帝啊,

你必把惡人送進滅亡的坑裡。

嗜血成性的騙子必早早夭亡。

但我要信靠你。