Zaburi 54 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 54:1-7

Zaburi 54

Kuomba Ulinzi Wa Mungu Kutokana Na Adui

Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Wakati Wazifu walimwendea Sauli na kumjulisha, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu?”

154:1 1Sam 24:15; 20:1; 2Nya 20:6Ee Mungu uniokoe kwa jina lako,

unifanyie hukumu kwa uwezo wako.

254:2 Za 4:1; 5:1; 55:1Ee Mungu, sikia maombi yangu,

usikilize maneno ya kinywa changu.

354:3 Za 36:1; 86:14; 18:48; 140:1, 4, 11; 1Sam 20:1Wageni wananishambulia,

watu wakatili wanayatafuta maisha yangu,

watu wasiomjali Mungu.

454:4 1Nya 5:20; Za 20:2; 18:35; Isa 41:10; Ebr 13:6; Rum 8:31, 32Hakika Mungu ni msaada wangu,

Bwana ndiye anayenitegemeza.

554:5 Kum 32:35; Isa 42:3; Mit 24:12; Za 89:49; 94:23Mabaya na yawarudie wale wanaonisingizia,

kwa uaminifu wako uwaangamize.

654:6 Law 7:12, 16; Ezr 1:4; Za 27:6; 44:8; 52:9; 138:2; 142:7; 145:1; 69:30Nitakutolea dhabihu za hiari;

Ee Bwana, nitalisifu jina lako

kwa kuwa ni vyema.

7Kwa maana ameniokoa katika shida zangu zote,

na macho yangu yamewatazama adui zangu kwa ushindi.