Zaburi 51 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 51:1-19

Zaburi 51

Kuomba Msamaha

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Baada ya kukemewa na nabii Nathani kwa kuzini na Bathsheba.

151:1 2Sam 24:14; 12:13; Za 39:8; 86:15; 25:7; 119:88; 9:13; Neh 4:5; 9:27; Isa 63:7; Kol 2:14; 2Nya 6:23; Mdo 3:19Ee Mungu, unihurumie,

kwa kadiri ya upendo wako usiokoma,

kwa kadiri ya huruma yako kuu,

uyafute makosa yangu.

251:2 Rum 3:3; Yer 2:22; 13:27; Mdo 22:16; Mit 20:30; Isa 4:4; Ebr 9:14; Zek 13:1; Ufu 1:5; 1Kor 6:11; Eze 13:1; 36:25; Mt 23:25, 26; 1Yn 1:7, 9Unioshe na uovu wangu wote

na unitakase dhambi yangu.

351:3 Isa 59:12; Za 32:5Kwa maana ninajua makosa yangu,

na dhambi yangu iko mbele yangu daima.

451:4 1Sam 15:24; Mwa 20:6; Lk 15:21; Rum 3:4Dhidi yako, wewe peke yako, nimetenda dhambi

na kufanya yaliyo mabaya machoni pako,

ili uthibitike kuwa wa kweli unenapo,

na kuwa na haki utoapo hukumu.

551:5 Law 5:2; Ay 5:7; 14:4; Rum 5:12; Yn 3:6Hakika mimi nilizaliwa mwenye dhambi,

mwenye dhambi tangu nilipotungwa mimba kwa mama yangu.

651:6 Ay 9:4; 34:32; Za 119:66; 143:10Hakika wewe wapendezwa na kweli itokayo moyoni,

ndani sana ya moyo wangu wanifundisha hekima.

751:7 Eze 36:25; Hes 19:6; Zek 13:1; Kut 12:22; Ebr 9:19; Isa 4:4; 1:19; 43:25; 44:22Nioshe kwa hisopo, nami nitakuwa safi,

unisafishe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.

851:8 Isa 35:10; Kut 12:46; Yer 33:11; Yoe 1:16Unipe kusikia furaha na shangwe,

mifupa uliyoiponda na ifurahi.

951:9 Yer 16:17; Zek 4:10; 2Sam 12:13Ufiche uso wako usizitazame dhambi zangu,

na uufute uovu wangu wote.

1051:10 Za 24:4; 78:37; Mt 5:8; Mdo 15:9; Eze 11:19; 18:31; 36:26; Mit 20:9; Yer 13:27; Efe 2:10Ee Mungu, uniumbie moyo safi,

uifanye upya roho ya uthabiti ndani yangu.

1151:11 Za 27:9; 138:8; 71:9; 106:3; Kut 33:15; Mwa 4:14; Isa 63:10; Eze 36:27; Efe 4:30; Rum 8:9Usinitupe kutoka mbele zako

wala kuniondolea Roho wako Mtakatifu.

1251:12 Ay 33:26; Za 110:3; 18:35; Rum 8:15; 2Kor 3:17Unirudishie tena furaha ya wokovu wako,

unipe roho ya utii, ili initegemeze.

1351:13 Kut 33:13; Za 1:1; Mdo 9:21-22; Ay 33:27Ndipo nitakapowafundisha wakosaji njia zako,

na wenye dhambi watakugeukia wewe.

1451:14 2Sam 12:9; Za 5:8; 22:5; 39:8; 68:20; 88:1; 35:28; 71:15Ee Mungu, Mungu uniokoaye,

niokoe na hatia ya kumwaga damu,

nao ulimi wangu utaimba juu ya haki yako.

1551:15 Kut 4:15Ee Bwana, fungua midomo yangu,

na kinywa changu kitatangaza sifa zako.

1651:16 1Sam 15:22Wewe hupendezwi na dhabihu, au ningaliileta,

hufurahii sadaka za kuteketezwa.

1751:17 Mit 15:8; Hag 2:14; Mt 11:29Bali dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika,

moyo uliovunjika wenye toba,

Ee Mungu, hutaudharau.

1851:18 Za 69:35; 147:2; 102:16; Zek 1:16-17; Isa 14:32; 44:26; 51:3; 51:19; Kum 33:19; Mal 3:3Kwa wema wa radhi yako uifanye Sayuni istawi,

ukazijenge upya kuta za Yerusalemu.

19Hapo ndipo kutakapokuwa na dhabihu za haki,

sadaka nzima za kuteketezwa za kukupendeza sana,

pia mafahali watatolewa

madhabahuni mwako.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

诗篇 51:1-19

第51篇

祈求上帝赦免

大卫与拔示巴通奸后,先知拿单来找他,他作了此诗,交给乐长。

1上帝啊,求你按你的慈爱怜悯我;

按你极大的怜悯除去我的过犯。

2求你洗净我的罪过,

清除我的罪恶。

3我知道自己的过犯,

我的罪恶一直萦绕眼前。

4我犯罪得罪了你,

唯独得罪了你,

做了你看为邪恶的事,

所以你责备我是正当的,

你对我的审判是公正的。

5我生来就是个罪人,

在母腹成胎的时候就有罪。

6你所喜爱的是内心的诚实,

求你使我内心有智慧。

7求你用牛膝草洁净我的罪,

使我干净;

求你洗净我,使我比雪更白。

8求你让我听到欢喜快乐的声音,

让我这被你压碎的骨头可以欢乐。

9求你掩面不看我的罪过,

除去我一切的罪恶。

10上帝啊,

求你为我造一颗纯洁的心,

使我里面重新有正直的灵。

11不要丢弃我,

使我离开你,

也不要从我身上收回你的圣灵。

12求你让我重新享受蒙你拯救的喜乐,

赐我一个乐意顺服你的心灵。

13我就会把你的法则教导悖逆之人,

使罪人归向你。

14上帝啊,拯救我的上帝啊,

求你救我脱离杀人流血的罪,

使我开口颂扬你的公义。

15主啊,求你开我的嘴唇,

我的口要向你发出赞美。

16你不喜欢祭物,

否则我会献上,

你也不喜爱燔祭。

17你所要的祭是忧伤的心灵。

上帝啊,你必不轻看忧伤痛悔的心。

18求你恩待锡安,重建耶路撒冷的城墙。

19那时,你必悦纳诚心献上的祭物、燔祭和全牲燔祭,

人们必把公牛献在你的坛上。