Zaburi 43 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 43:1-5

Zaburi 43

Maombi Ya Mtu Aliyeko Uhamishoni Yanaendelea

143:1 Amu 6:31; Za 25:20; 36:3; 109:2; 7:8Ee Mungu unihukumu,

nitetee dhidi ya taifa lisilomcha Mungu,

niokoe na watu wadanganyifu na waovu.

243:2 Za 44:9; 74:1; 88:14; 89:38; 35:14; 42:9; 28:7; Isa 26:4Wewe ni Mungu ngome yangu.

Kwa nini umenikataa?

Kwa nini niendelee kuomboleza,

nikiwa nimeonewa na adui?

343:3 Za 2:6; 3:4; 27:1; 26:3; 25:5; 2Sam 15:25Tuma hima nuru yako na kweli yako

na viniongoze;

vinilete mpaka mlima wako mtakatifu,

mpaka mahali unapoishi.

443:4 Za 42:2; 26:6; 84:3; 21:6; 16:3; Mwa 4:21Ndipo nitakwenda madhabahuni pa Mungu,

kwa Mungu, furaha yangu na shangwe yangu.

Nitakusifu kwa kinubi,

Ee Mungu, Mungu wangu.

543:5 Za 42:5, 6, 11Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka?

Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?

Weka tumaini lako kwa Mungu,

kwa sababu bado nitamsifu

Mwokozi wangu na Mungu wangu.