Zaburi 42 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 42:1-11

KITABU CHA PILI

(Zaburi 42–72)

Zaburi 42

Maombi Ya Mtu Aliye Uhamishoni

Kwa mwimbishaji. Utenzi wa wana wa Kora.

142:1 Ay 19:27; Yoe 1:20; Za 18:33; 119:131; Kum 10:7Kama vile ayala aoneavyo shauku vijito vya maji,

ndivyo nafsi yangu ikuoneavyo shauku, Ee Mungu.

242:2 Za 43:4; 143:6; 84:7; 63:1; Yos 3:10; 1The 1:9; Yn 7:37; Rum 9:26; 1Sam 14:19; Mt 16:16; 9:26Nafsi yangu inamwonea Mungu kiu, Mungu aliye hai.

Ni lini nitaweza kwenda kukutana na Mungu?

342:3 Ay 3:24; Mik 7:10; Za 79:10; 115:2; Yoe 2:17Machozi yangu yamekuwa chakula changu

usiku na mchana,

huku watu wakiniambia mchana kutwa,

“Yuko wapi Mungu wako?”

442:4 1Sam 1:15; Isa 2:2; 30:29; Yon 2:9; Ezr 3:13; Yos 6:5; Za 35:18; 109:30; 55:14; 122:1; 95:2; 100:4; 147:7Mambo haya nayakumbuka

ninapoimimina nafsi yangu:

Jinsi nilivyokuwa nikienda na umati wa watu,

nikiongoza maandamano kuelekea kwenye nyumba ya Mungu,

kwa kelele za shangwe na za shukrani

katikati ya umati uliosherehekea.

542:5 Mao 3:20; Mt 26:38; Za 9:1; 38:6; 77:3; 25:5; 71:14; 56:3, 11; 18:46; Ay 20:2; Isa 50:10Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka?

Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?

Weka tumaini lako kwa Mungu,

kwa sababu bado nitamsifu,

Mwokozi wangu na 642:6 Za 43:5; 63:6; 7:11; Mwa 13:10; Hes 13:29; Kum 3:8; 4:48Mungu wangu.

Nafsi yangu inasononeka ndani yangu;

kwa hiyo nitakukumbuka

kutoka nchi ya Yordani,

katika vilele vya Hermoni,

kutoka Mlima Mizari.

742:7 Eze 7:26; Mwa 1:2; 7:11; Za 69:2; Yon 2:3Kilindi huita kilindi,

katika ngurumo za maporomoko ya maji yako;

mawimbi yako yote pamoja na viwimbi

vimepita juu yangu.

842:8 Za 57:3; 16:7; 133:3; Mhu 5:18; 8:15; Kum 28:8Mchana Bwana huelekeza upendo wake,

usiku wimbo wake uko nami:

maombi kwa Mungu wa uzima wangu.

942:9 Za 18:31; 10:11; 35:14; 106:42; 9:13; 43:2; Ay 20:19Ninamwambia Mungu Mwamba wangu,

“Kwa nini umenisahau?

Kwa nini niendelee kuomboleza,

nikiwa nimeonewa na adui?”

1042:10 Za 89:51; 119:42; 44:16; 6:2; 102:8; Kum 32:27Mifupa yangu inateseka kwa maumivu makali

adui zangu wanaponidhihaki,

wakiniambia mchana kutwa,

“Yuko wapi Mungu wako?”

1142:11 Za 43:5Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka?

Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?

Weka tumaini lako kwa Mungu,

kwa sababu bado nitamsifu,

Mwokozi wangu na Mungu wangu.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

詩篇 42:1-11

卷二:詩篇42—72

第42篇

流落異鄉者的禱告

可拉後裔作的訓誨詩,交給樂長。

1上帝啊,我的心切慕你,

像鹿切慕溪水。

2我心裡渴慕上帝,

渴慕永活的上帝,

我何時才能去朝見祂呢?

3我晝夜以淚為食,

人們整天譏笑我:

「你的上帝在哪裡?」

4從前我與眾人同行,帶領大家去上帝的殿,

在歡呼、感恩聲中一起過節。

我回想這些事,

心中無限憂傷。

5我的心啊!

你為何沮喪?為何在我裡面煩躁?

要仰望上帝,

因為我還要讚美祂——我的救主,我的上帝。

6我的上帝啊,我心中沮喪,

便在約旦之地、黑門山和米薩山想起你。

7你的瀑布發出巨響,

迴盪在深淵之間,

你的洪濤巨浪淹沒我。

8白天耶和華將祂的慈愛澆灌我;

夜間我歌頌祂,

向賜我生命的上帝禱告。

9我對我的磐石上帝說:

「你為何忘記我?

為何要我受仇敵的攻擊,使我哀傷不已呢?」

10仇敵的辱罵刺骨鑽心。

他們整天對我說:

「你的上帝在哪裡?」

11我的心啊!

你為何沮喪?為何在我裡面煩躁?

要仰望上帝,

因為我還要讚美祂——我的救主,我的上帝。