Zaburi 41
Maombi Ya Mtu Mgonjwa
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
141:1 Kum 14:29; Ay 24:4; Za 25:17; Mit 14:21; Mk 10:21Heri mtu yule anayemjali mnyonge,
Bwana atamwokoa wakati wa shida.
241:2 Za 12:5; 32:7; 71:20; 119:88, 159; 138:7; 143:1; 37:22; Ezr 9:9; Kum 6:24Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake,
atambariki katika nchi
na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
341:3 Za 6:6; 2Fal 1:4; 2Sam 13:5Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani,
atamwinua kutoka kitandani mwake.
441:4 Za 6:2; 9:13; Kum 32:39; Za 51:4Nilisema, “Ee Bwana nihurumie,
niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
541:5 Za 38:12Adui zangu wanasema kwa hila,
“Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
641:6 Za 12:2; 101:7; Mt 5:11; Mit 26:24; Law 19:16Kila anapokuja mtu kunitazama,
huzungumza uongo,
huku moyo wake hukusanya masingizio;
kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
741:7 Za 71:10Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu,
hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
841:8 2Fal 1:4“Ugonjwa mbaya sana umempata,
kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
941:9 Oba 1:7; Yn 13:18; 2Sam 15:12; Ay 19:14, 19; Hes 30:2; Lk 22:21; Za 55:20; 89:34; Mt 26:23Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini,
yule aliyekula chakula changu
ameniinulia kisigino chake.
1041:10 Za 3:3; 9:13; 2Sam 3:39Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie,
ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
1141:11 Hes 14:8; Za 25:2Najua kwamba wapendezwa nami,
kwa kuwa adui yangu hanishindi.
1241:12 Za 21:6; 61:7; 34:15; 25:21; 18:35; 37:17; 63:8; Ay 4:7; Mdo 2:38Katika uadilifu wangu unanitegemeza
na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
1341:13 Mwa 24:27; Za 72:18, 19; 89:52; 106:48Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli,
tangu milele na hata milele.
Amen na Amen.