Zaburi 4 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 4:1-8

Zaburi 4

Sala Ya Jioni Ya Kuomba Msaada

Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi.

14:1 Za 13:3; 27:7; 69:16; 30:10; 54:2; 84:8; 88:2; 6:7; 102:2; Mwa 32:7; Amu 2:15Nijibu nikuitapo,

Ee Mungu wangu mwenye haki!

Nipumzishe katika shida zangu;

nirehemu, usikie ombi langu.

24:2 Kut 16:7; Amo 2:4; 2Fal 19:26; Ay 8:22; Yer 13:25; 16:19; Za 12:1; 40:4; 1Sam 4:21Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu

kuwa aibu mpaka lini?

Mtapenda udanganyifu

na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?

34:3 Za 6:8; 12:1; 30:4; 31:23; 79:2; Mik 7:2, 7; Kut 33:16; 1Tim 4:7; 2Pet 3:11Fahamuni hakika kwamba Bwana amewatenga

wale wamchao kwa ajili yake;

Bwana atanisikia nimwitapo.

44:4 Efe 4:26; Za 63:6; Dan 2:28; Mit 3:74:4 Za 11:1; 25:20; 31:2; 32:11Katika hasira yako, usitende dhambi.

Mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya

mkiichunguza mioyo yenu.

54:5 Za 31:6; 37:3; 115:9; Mit 3:5; 28:26; Kum 33:19; Yn 14:1; Isa 26:44:5 Hes 14:18; Isa 65:6-7; Yer 32:17Toeni dhabihu zilizo haki;

mtegemeeni Bwana.

64:6 Hes 6:25; Za 80:3Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye

kutuonyesha jema lolote?”

Ee Bwana, tuangazie nuru ya uso wako.

74:7 Mdo 14:17; Isa 9:3; 35:10; 65:14, 18; Mwa 27:28; Kum 28:51Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa

kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.

84:8 Law 26:6; Hes 6:26; Yer 32:37; Ay 11:18; Flp 4:7; Kum 12:10; 33:28; Yn 14:274:8 Law 11:44Nitajilaza chini na kulala kwa amani,

kwa kuwa wewe peke yako, Ee Bwana,

waniwezesha kukaa kwa salama.

New Arabic Version

مزمور 4:1-8

الْمَزْمُورُ الرَّابِعُ

لِقَائِدِ الْمُنْشِدِينَ عَلَى الآلاتِ الْوَتَرِيَّةِ. مَزْمُورٌ لِدَاوُدَ

1اسْتَجِبْ لِي عِنْدَمَا أَدْعُوكَ يَا إِلَهَ بِرِّي، فَقَدْ أَفْرَجْتَ لِي دَوْماً فِي الضِّيقِ، فَأَنْعِمْ عَلَيَّ وَأَصْغِ إِلَى صَلاتِي. 2إِلَى مَتَى يَا بَنِي الْبَشَرِ تُحَوِّلُونَ مَجْدِي عَاراً؟ وَإِلَى مَتَى تُحِبُّونَ الأُمُورَ البَاطِلَةَ، وَتَسْعَوْنَ وَرَاءَ الأَكَاذِيبِ؟ 3اعْلَمُوا أَنَّ الرَّبَّ قَدْ مَيَّزَ لِنَفْسِهِ تَقِيَّهُ؛ الرَّبُّ يَسْمَعُ عِنْدَمَا أَدْعُوهُ. 4ارْتَعِدُوا وَلَا تُخْطِئُوا. فَكِّرُوا فِي قُلُوبِكُمْ عَلَى مَضَاجِعِكُمْ مُلْتَزِمِين الصَّمْتَ. 5قَدِّمُوا ذَبَائِحَ الْبِرِّ، وَاتَّكِلُوا عَلَى الرَّبِّ.

6مَا أَكْثَرَ الْمُتَسَائِلِينَ: «مَنْ يُرِينَا خَيْراً؟» أَشْرِقْ عَلَيْنَا أَيُّهَا الرَّبُّ بِنُورِ وَجْهِكَ. 7غَرَسْتَ فِي قَلْبِي فَرَحاً أَعْظَمَ مِنْ فَرَحِ مَنِ امْتَلَأَتْ بُيُوتُهُمْ وَأَجْرَانُهُمْ بِالْحِنْطَةِ وَالْخَمْرِ الْجَدِيدَةِ. 8بِسَلامٍ أَضْطَجِعُ وَأَنَامُ، لأَنَّكَ أَنْتَ وَحْدَكَ يَا رَبُّ تُنْعِمُ عَلَيَّ بِالطُّمَأْنِينَةِ وَالسَّلامِ.