Zaburi 39
Maombi Ya Mtu Anayeteseka
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa Yeduthuni. Zaburi ya Daudi.
139:1 1Fal 2:4; Kol 4:5; Ebr 2:1; Ay 1:22; 6:24; Yak 1:26; 3:2; Za 34:13; 119:9, 59; Mit 4:26, 27; 20:11Nilisema, “Nitaziangalia njia zangu
na kuuzuia ulimi wangu usije ukatenda dhambi;
nitaweka lijamu kinywani mwangu
wakati wote waovu wanapokuwa karibu nami.”
239:2 Za 6:3; 25:17; 39:9; 77:4; 31:10; Ay 31:34Lakini niliponyamaza kimya na kutulia,
hata pasipo kusema lolote jema,
uchungu wangu uliongezeka.
339:3 Yer 20:9; Lk 24:32; Za 1:2; 119:15; Yer 5:14; 20:9; 23:29Moyo wangu ulipata moto ndani yangu,
nilipotafakari, moto uliwaka,
ndipo nikasema kwa ulimi wangu:
439:4 Ay 14:5; 14:2; 7:7; Mwa 47:9“Ee Bwana, nijulishe mwisho wa maisha yangu
na hesabu ya siku zangu;
nijalie kujua jinsi maisha yangu
yanavyopita upesi.
539:5 Ay 10:20; 7:7; Za 62:9; 90:4; 89:45; 102:23Umefanya maisha yangu mafupi kama pumzi;
muda wangu wa kuishi ni kama
hauna thamani kwako.
Maisha ya kila mwanadamu
ni kama pumzi.
639:6 Ay 8:9; 27:17; Mhu 6:12; Lk 12:20; Yak 4:14; 1:11; Za 102:11; 127:2Hakika kila binadamu ni kama njozi
aendapo huku na huko:
hujishughulisha na mengi lakini ni ubatili;
anakusanya mali nyingi,
wala hajui ni nani atakayeifaidi.
739:7 Za 9:18“Lakini sasa Bwana, nitafute nini?
Tumaini langu ni kwako.
839:8 Isa 53:5, 8, 10; 43:28; Kum 28:37; Za 69:7; 51:1, 14; 32:1; 6:4; 79:4; Dan 9:16Niokoe kutoka kwenye makosa yangu yote,
usinifanye kuwa dhihaka ya wapumbavu.
939:9 Za 38:13; Isa 38:15Nilinyamaza kimya,
sikufumbua kinywa changu,
kwa sababu wewe ndiwe uliyetenda hili.
1039:10 2Nya 21:14; Eze 7:9; 24:16; Kut 9:3Niondolee mjeledi wako,
nimeshindwa kwa mapigo ya mkono wako.
1139:11 Kum 28:20; Isa 26:16; 51:8; 66:15; Eze 5:15; 2Pet 2:16; Za 94:10; 90:7; Ay 7:7; 13:28; Lk 12:33; Yak 5:2Unakemea na kuadhibu wanadamu
kwa ajili ya dhambi zao;
unaharibu utajiri wao kama nondo aharibuvyo:
kila mwanadamu ni kama pumzi tu.
1239:12 Za 17:1; 1Nya 29:15; Ebr 11:13; Law 25:23; Kum 1:45; 2Fal 20:5; Mwa 23:4; 47:9“Ee Bwana, usikie maombi yangu,
usikie kilio changu unisaidie,
usiwe kiziwi kwa kulia kwangu.
Kwani mimi ninaishi na wewe kama mgeni,
kama walivyokuwa baba zangu wote,
1339:13 Ay 10:20, 21Tazama mbali nami, ili niweze kufurahi tena
kabla sijaondoka na nisiwepo tena.”
الْمَزْمُورُ التَّاسِعُ والثَّلاثُونَ
لِقَائِدِ الْمُنْشِدِينَ، مَزْمُورٌ لِدَاوُدَ
1قُلْتُ: «أَحْرِصُ عَلَى حُسْنِ الْمَسْلَكِ فَلَا يُخْطِئُ لِسَانِي الْقَوْلَ. سَأَكُمُّ فَمِي عَنِ الْكَلامِ مَادَامَ الشِّرِّيرُ أَمَامِي». 2صَمَتُّ صَمْتاً. أَمْسَكْتُ حَتَّى عَنِ الْخَيْرِ، فَثَارَ وَجَعِي. 3الْتَهَبَ قَلْبِي فِي دَاخِلِي، وَفِي تَأَمُّلِي اشْتَعَلَتْ فِيَّ النَّارُ، فَأَطْلَقْتُ لِسَانِي بِالْكَلامِ. 4يَا رَبُّ عَرِّفْنِي مَتَى تَكُونُ نِهَايَتِي، وَكَمْ تَطُولُ أَيَّامِي فَأُدْرِكَ أَنَّنِي إِنْسَانٌ زَائِلٌ. 5هُوَذَا قَدْ جَعَلْتَ حَيَاتِي قَصِيرَةً، وَعُمْرِي كَلَا شَيْءَ أَمَامَكَ. كُلُّ إِنْسَانٍ حَيٍّ لَيْسَ سِوَى نَفْخَةٍ! 6إِنَّمَا كَخَيَالٍ يَتَمَشَّى الإِنْسَانُ، فَعَبَثاً يُكَافِحُ النَّاسُ. يَجْمَعُ الْوَاحِدُ مِنْهُمْ ثَرْوَةً وَلَا يَدْرِي مَنْ يَرِثُهَا مِنْ بَعْدِهِ.
7وَالآنَ، فَأَيُّ شَيْءٍ أَنْتَظِرُ يَا رَبُّ؟ إِنَّمَا فِيكَ رَجَائِي. 8نَجِّنِي مِنْ جَمِيعِ مَعَاصِيَّ، وَلَا تَجْعَلْنِي عَاراً عِنْدَ الأَحْمَقِ. 9صَمَتُّ. لَا أَفْتَحُ فَمِي، لأَنَّكَ أَنْتَ فَعَلْتَ هَذَا. 10ارْفَعْ عَنِّي ضَرْبَتَكَ فَقَدْ فَنِيْتُ مِنْ صَفْعَةِ يَدِكَ. 11عِنْدَمَا تُؤَدِّبُ الإِنْسَانَ بِالتَّوْبِيخِ عَلَى الإِثْمِ، تُتْلِفُ بَهَاءَهُ إِتْلافَ الْعُثِّ. إِنَّمَا كُلُّ إِنْسَانٍ نَفْخَةٌ. 12يَا رَبُّ اسْمَعْ صَلاتِي. وَأَصْغِ إِلَى صُرَاخِي، وَلَا تَسْكُتْ أَمَامَ دُمُوعِي، لأَنِّي غَرِيبٌ عِنْدَكَ وَعَابِرُ سَبِيلٍ كَجَمِيعِ آبَائِي. 13حَوِّلْ غَضَبَكَ عَنِّي فَأَنْتَعِشَ، قَبْلَ أَنْ أَمُوتَ وَيَخْتَفِيَ أَثَرِي.