Zaburi 35 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 35:1-28

Zaburi 35

Kuomba Msaada: Kuokolewa Kutokana Na Maadui

Zaburi ya Daudi.

135:1 1Sam 24:15; Kut 14:14Ee Bwana, pingana na wale wanaopingana nami,

upigane na hao wanaopigana nami.

235:2 Za 3:3, 7; Ay 17:3; Mwa 50:24; 35:3; Hes 25:7; Za 27:1; Yos 8:18Chukua ngao na kigao.

Inuka unisaidie.

3Inua mkuki wako na fumo35:3 Fumo ni sawa na sagai, maana yake ni mkuki mfupi. lako

dhidi ya hao wanaonifuatia.

Iambie nafsi yangu,

“Mimi ni wokovu wako.”

435:4 Za 38:12; 40:14; 69:6, 19; 70:2; 83:17; 25:3; 129:5; Yer 4:30; Mal 2:9; Isa 45:16Wafedheheshwe na waaibishwe

wale wanaotafuta uhai wangu.

Wanaofanya shauri kuniangamiza

warudishwe nyuma kwa hofu.

535:5 Ay 13:25; Za 1:4; 34:7Wawe kama makapi yapeperushwayo na upepo,

malaika wa Bwana akiwafukuza.

6Njia yao na iwe giza na ya utelezi,

malaika wa Bwana akiwafuatilia.

735:7 Ay 18:8; 9:31; Za 7:4; 7:15; 55:23Kwa vile walinifichia wavu wao bila sababu,

na bila sababu wamenichimbia shimo,

835:8 Isa 47:11; 1The 5:3; Za 7:15; Mit 5:22maafa na yawapate ghafula:

wavu walionifichia na uwatege wenyewe,

na waanguke katika shimo hilo,

kwa maangamizo yao.

935:9 Za 2:11; 9:14; 13:5; 27:1; Lk 1:47; 1Sam 2:1; Isa 61:10; Ebr 3:18Ndipo nafsi yangu itashangilia katika Bwana

na kuufurahia wokovu wake.

1035:10 Kut 9:14; Za 12:5; 71:19; 18:17, 31; 113:5; 37:14; 86:1; 74:21; 109:16; 140:12; Isa 41:17Nitapaza sauti yangu nikisema,

“Ni nani aliye kama wewe, Ee Bwana?

Wewe huwaokoa maskini kutokana na wale walio na nguvu kuliko wao,

maskini na mhitaji kutokana na wanaowanyangʼanya!”

1135:11 Kut 23:1; Mt 26:60Mashahidi wakatili wanainuka,

wananiuliza mambo nisiyoyajua.

1235:12 Yer 18:20; Za 38:20; 109:5; Mit 17:13Wananilipa baya kwa jema

na kuiacha nafsi yangu ukiwa.

1335:13 2Sam 3:31; 1Fal 20:31; Za 30:11; 69:10, 11; 109:24; Ay 30:25Lakini walipokuwa wagonjwa, nilivaa nguo ya gunia

na nikajinyenyekesha kwa kufunga.

Maombi yangu yaliponirudia bila kujibiwa,

1435:14 Za 38:6; 42:9; 43:2niliendelea kuomboleza

kama vile wao ni rafiki au ndugu.

Niliinamisha kichwa chini kwa huzuni

kama ninayemwombolezea mama yangu.

1535:15 Ay 31:29; 16:10Lakini nilipojikwaa,

walikusanyika kwa shangwe;

washambuliaji walijikusanya dhidi yangu

bila mimi kujua.

Walinisingizia pasipo kukoma.

1635:16 Za 22:7; Mk 10:34; 9:18; Ay 16:9; Mdo 7:54Kama watu wasiomcha Mungu, wamenidhihaki,

wamenisagia meno.

1735:17 Za 6:3; 22:20, 21; 57:4; 58:6Ee Bwana, utatazama mpaka lini?

Niokoe maisha yangu na maangamizi yao,

uhai wangu wa thamani

kutokana na simba hawa.

1835:18 Za 22:20, 25; 42:4; 109:30Nami nitakushukuru mbele ya kusanyiko kubwa,

nitakusifu katikati ya watu wengi.

1935:19 Za 9:13; 38:19; 69:4; Yn 15:25; Mit 6:13; 10:10Usiwaache wale wanaonisimanga,

wale ambao ni adui zangu bila sababu;

usiwaache wale ambao ni adui zangu bila sababu

wakonyeze jicho kwa hila.

2035:20 Za 38:12; 55:21; Yer 9:8; Mik 6:12Hawazungumzi kwa amani,

bali wanatunga mashtaka ya uongo

dhidi ya wale wanaoishi

kwa utulivu katika nchi.

2135:21 Ay 16:10; Eze 25:3; Za 40:15; 70:3Hunifumbulia vinywa vyao wakisema, “Aha! Aha!

Kwa macho yetu wenyewe tumeliona.”

2235:22 Kut 3:7; Za 10:1, 14Ee Bwana, umeona hili, usiwe kimya.

Usiwe mbali nami, Ee Bwana.

2335:23 Za 7:6; 80:2; 17:13; 1Sam 24:15Amka, inuka unitetee!

Unipiganie Mungu wangu na Bwana wangu.

2435:24 Za 22:17; 7:8; 26:11; 2The 1:6Nihukumu kwa haki yako, Ee Bwana Mungu wangu,

sawasawa na haki yako;

usiwaache wakusimange.

2535:25 Mit 1:12; Za 35:21; 124:3; Mao 2:16Usiwaache wafikiri, “Aha, hili ndilo tulilotaka!”

Au waseme, “Tumemmeza.”

2635:26 Za 22:17; 4:1; 109:29; 38:16; Ay 8:22; 19:5; Mik 7:10Wote wanaofurahia dhiki yangu

waaibishwe na wachanganyikiwe;

hao wanaojiinua dhidi yangu

wavikwe aibu na dharau.

2735:27 Za 9:4; 20:5; 33:3; 147:11; 149:4; Ay 17:3Wale wanaofurahia hukumu yangu ya haki

wapige kelele za shangwe na furaha;

hebu waseme siku zote, “Bwana atukuzwe,

ambaye amefurahia mafanikio ya mtumishi wake.”

2835:28 Za 5:8; 51:14; 71:15, 24; 72:15Ulimi wangu utanena haki yako

na sifa zako mchana kutwa.

New Russian Translation

Псалтирь 35:1-13

Псалом 35

1Дирижеру хора. Псалом Давида, слуги Господа.

2Грех говорит нечестивому

глубоко в его сердце;

нет Божьего страха в глазах его.

3Льстит он себе в своих же глазах,

что ищет грех свой,

чтобы возненавидеть его.35:3 Или: «Он так превозносит себя, что не видит порок свой, чтобы возненавидеть его».

4Слова его уст — беззаконие и обман;

он отрекся от мудрости и не делает добра.

5Даже на ложе своем замышляет он беззаконие.

Он встал на недобрый путь

и не отвергает зла.

6Господи, милость Твоя до небес,

до облаков Твоя верность.

7Праведность Твоя велика, как горы,

Твоя справедливость глубока, как бездна.

Ты хранишь человека и зверя, Господи.

8Боже, милость Твоя драгоценна!

В тени Твоих крыл укрываются смертные.

9Пируют они от щедрот Твоего дома;

из реки отрад Твоих Ты их поишь.

10Ведь у Тебя источник жизни,

и во свете Твоем мы видим свет.

11Излей Свою милость на знающих Тебя,

праведность Свою — на правых сердцем.

12Да не наступит на меня нога гордеца;

да не изгонит меня рука нечестивого.

13Посмотри, как пали беззаконники:

повергнуты они и не могут подняться.