Zaburi 35 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 35:1-28

Zaburi 35

Kuomba Msaada: Kuokolewa Kutokana Na Maadui

Zaburi ya Daudi.

135:1 1Sam 24:15; Kut 14:14Ee Bwana, pingana na wale wanaopingana nami,

upigane na hao wanaopigana nami.

235:2 Za 3:3, 7; Ay 17:3; Mwa 50:24; 35:3; Hes 25:7; Za 27:1; Yos 8:18Chukua ngao na kigao.

Inuka unisaidie.

3Inua mkuki wako na fumo35:3 Fumo ni sawa na sagai, maana yake ni mkuki mfupi. lako

dhidi ya hao wanaonifuatia.

Iambie nafsi yangu,

“Mimi ni wokovu wako.”

435:4 Za 38:12; 40:14; 69:6, 19; 70:2; 83:17; 25:3; 129:5; Yer 4:30; Mal 2:9; Isa 45:16Wafedheheshwe na waaibishwe

wale wanaotafuta uhai wangu.

Wanaofanya shauri kuniangamiza

warudishwe nyuma kwa hofu.

535:5 Ay 13:25; Za 1:4; 34:7Wawe kama makapi yapeperushwayo na upepo,

malaika wa Bwana akiwafukuza.

6Njia yao na iwe giza na ya utelezi,

malaika wa Bwana akiwafuatilia.

735:7 Ay 18:8; 9:31; Za 7:4; 7:15; 55:23Kwa vile walinifichia wavu wao bila sababu,

na bila sababu wamenichimbia shimo,

835:8 Isa 47:11; 1The 5:3; Za 7:15; Mit 5:22maafa na yawapate ghafula:

wavu walionifichia na uwatege wenyewe,

na waanguke katika shimo hilo,

kwa maangamizo yao.

935:9 Za 2:11; 9:14; 13:5; 27:1; Lk 1:47; 1Sam 2:1; Isa 61:10; Ebr 3:18Ndipo nafsi yangu itashangilia katika Bwana

na kuufurahia wokovu wake.

1035:10 Kut 9:14; Za 12:5; 71:19; 18:17, 31; 113:5; 37:14; 86:1; 74:21; 109:16; 140:12; Isa 41:17Nitapaza sauti yangu nikisema,

“Ni nani aliye kama wewe, Ee Bwana?

Wewe huwaokoa maskini kutokana na wale walio na nguvu kuliko wao,

maskini na mhitaji kutokana na wanaowanyangʼanya!”

1135:11 Kut 23:1; Mt 26:60Mashahidi wakatili wanainuka,

wananiuliza mambo nisiyoyajua.

1235:12 Yer 18:20; Za 38:20; 109:5; Mit 17:13Wananilipa baya kwa jema

na kuiacha nafsi yangu ukiwa.

1335:13 2Sam 3:31; 1Fal 20:31; Za 30:11; 69:10, 11; 109:24; Ay 30:25Lakini walipokuwa wagonjwa, nilivaa nguo ya gunia

na nikajinyenyekesha kwa kufunga.

Maombi yangu yaliponirudia bila kujibiwa,

1435:14 Za 38:6; 42:9; 43:2niliendelea kuomboleza

kama vile wao ni rafiki au ndugu.

Niliinamisha kichwa chini kwa huzuni

kama ninayemwombolezea mama yangu.

1535:15 Ay 31:29; 16:10Lakini nilipojikwaa,

walikusanyika kwa shangwe;

washambuliaji walijikusanya dhidi yangu

bila mimi kujua.

Walinisingizia pasipo kukoma.

1635:16 Za 22:7; Mk 10:34; 9:18; Ay 16:9; Mdo 7:54Kama watu wasiomcha Mungu, wamenidhihaki,

wamenisagia meno.

1735:17 Za 6:3; 22:20, 21; 57:4; 58:6Ee Bwana, utatazama mpaka lini?

Niokoe maisha yangu na maangamizi yao,

uhai wangu wa thamani

kutokana na simba hawa.

1835:18 Za 22:20, 25; 42:4; 109:30Nami nitakushukuru mbele ya kusanyiko kubwa,

nitakusifu katikati ya watu wengi.

1935:19 Za 9:13; 38:19; 69:4; Yn 15:25; Mit 6:13; 10:10Usiwaache wale wanaonisimanga,

wale ambao ni adui zangu bila sababu;

usiwaache wale ambao ni adui zangu bila sababu

wakonyeze jicho kwa hila.

2035:20 Za 38:12; 55:21; Yer 9:8; Mik 6:12Hawazungumzi kwa amani,

bali wanatunga mashtaka ya uongo

dhidi ya wale wanaoishi

kwa utulivu katika nchi.

2135:21 Ay 16:10; Eze 25:3; Za 40:15; 70:3Hunifumbulia vinywa vyao wakisema, “Aha! Aha!

Kwa macho yetu wenyewe tumeliona.”

2235:22 Kut 3:7; Za 10:1, 14Ee Bwana, umeona hili, usiwe kimya.

Usiwe mbali nami, Ee Bwana.

2335:23 Za 7:6; 80:2; 17:13; 1Sam 24:15Amka, inuka unitetee!

Unipiganie Mungu wangu na Bwana wangu.

2435:24 Za 22:17; 7:8; 26:11; 2The 1:6Nihukumu kwa haki yako, Ee Bwana Mungu wangu,

sawasawa na haki yako;

usiwaache wakusimange.

2535:25 Mit 1:12; Za 35:21; 124:3; Mao 2:16Usiwaache wafikiri, “Aha, hili ndilo tulilotaka!”

Au waseme, “Tumemmeza.”

2635:26 Za 22:17; 4:1; 109:29; 38:16; Ay 8:22; 19:5; Mik 7:10Wote wanaofurahia dhiki yangu

waaibishwe na wachanganyikiwe;

hao wanaojiinua dhidi yangu

wavikwe aibu na dharau.

2735:27 Za 9:4; 20:5; 33:3; 147:11; 149:4; Ay 17:3Wale wanaofurahia hukumu yangu ya haki

wapige kelele za shangwe na furaha;

hebu waseme siku zote, “Bwana atukuzwe,

ambaye amefurahia mafanikio ya mtumishi wake.”

2835:28 Za 5:8; 51:14; 71:15, 24; 72:15Ulimi wangu utanena haki yako

na sifa zako mchana kutwa.

New Arabic Version

مزمور 35:1-28

الْمَزْمُورُ الْخَامِسُ وَالثَّلاثُونَ

لِدَاوُدَ

1يَا رَبُّ كُنْ خَصْماً لِمَنْ يُخَاصِمُونَنِي، وَحَارِبِ الَّذِينَ يُحَارِبُونَنِي. 2تَقَلَّدِ التُّرْسَ وَالدِّرْعَ وَهُبَّ لِنَجْدَتِي. 3جَرِّدْ رُمْحاً وَتَصَدَّ لِمُطَارِدِيَّ، وَقُلْ لِنَفْسِي: خَلاصُكِ أَنَا. 4لِيَخْزَ وَلْيَخْجَلِ السَّاعُونَ إِلَى قَتْلِي. لِيَنْهَزِمْ وَيَخْجَلِ الْمُتَوَاطِئُونَ عَلَى أَذِيَّتِي. 5لِيَكُونُوا مِثْلَ ذَرَّاتِ التِّبْنِ فِي مَهَبِّ الرِّيحِ. وَلْيَدْحَرْهُمْ مَلاكُ الرَّبِّ. 6لِتَكُنْ طَرِيقُهُمْ مُظْلِمَةً وَزَلِقَةً، وَلْيَتَعَقَّبْهُمْ مَلاكُ الرَّبِّ. 7فَإِنَّهُمْ مِنْ غَيْرِ سَبَبٍ أَخْفَوْا لِي شَبَكَةً فَوْقَ الْهُوَّةِ، وَمِنْ غَيْرِ عِلَّةٍ حَفَرُوا لِي حُفْرَةً. 8لِيُطْبِقِ الْهَلاكُ فَجْأَةً عَلَى عَدُوِّي، وَلْتُمْسِكْ بِهِ الشَّبَكَةُ الَّتِي أَخْفَاهَا، فَيَهْلِكَ فِيهَا. 9أَمَّا نَفْسِي فَتَفْرَحُ بِالرَّبِّ وَتَبْتَهِجُ بِخَلاصِهِ. 10جَمِيعُ عِظَامِي تَقُولُ: يَا رَبُّ مَنْ مِثْلُكَ، المُخَلِّصُ الْمِسْكِينَ مِمَّنْ هُوَ أَقْوَى مِنْهُ وَمُنْقِذُ الْفَقِيرِ وَالْبَائِسِ مِنْ يَدِ نَاهِبِهِ؟

11يَقُومُ عَلَيَّ شُهُودُ زُورٍ يَتَّهِمُونَنِي ظُلْماً بِمَا لَا أَعْلَمُ. 12يُجَازُونَنِي عَنِ الْخَيْرِ شَرّاً إِتْعَاساً لِنَفْسِي. 13أَمَّا أَنَا فَقَدْ لَبِسْتُ الْمِسْحَ حُزْناً عَلَى مَرَضِهِمْ، وَأَذْلَلْتُ نَفْسِي بِالصَّوْمِ، وَلَكِنَّ صَلاتِي كَانَتْ تَرْتَدُّ إِلَى صَدْرِي مِنْ غَيْرِ اسْتِجَابَةٍ. 14لَقَدْ عَامَلْتُ كُلًّا مِنْهُمْ كَأَنَّهُ صَدِيقِي وَأَخِي، وَأَطْرَقْتُ حُزْناً كَمَنْ يَنْدُبُ أُمَّهُ. 15وَأَمَّا هُمْ فَشَمِتُوا فَرَحاً عِنْدَ سَقْطَتِي، وَتَجَمَّعُوا عَلَيَّ شَاتِمِينَ، وَشَرَعَ غُرَبَاءُ لَا أَعْرِفُهُمْ يَضْرِبُونَنِي. مَزَّقُونِي وَلَمْ يَرْتَدِعُوا. 16كَفُجَّارٍ مَاجِنِينَ مُجْتَمِعِينَ حَوْلَ وَلِيمَةٍ حَرَّقُوا عَلَيَّ أَسْنَانَهُمْ.

17يَا سَيِّدُ، حَتَّى مَتَى تَظَلُّ مُتَفَرِّجاً؟ نَجِّ نَفْسِي مِنْ مَهَالِكِهِمْ وَخَلِّصْ حَيَاتِي مِنْ بَيْنِ الأَشْبَالِ. 18أَشْكُرُكَ فِي جَمَاعَةِ الْعَابِدِينَ، وَأَحْمَدُكَ فِي وَسَطِ حُشُودٍ كَثِيرَةٍ. 19لَا يَشْمَتْ بِي أَعْدَائِي بِحُجَّةٍ بَاطِلَةٍ، وَلَا يَتَغَامَزْ مُبْغِضِيَّ عَلَيَّ، بِغَيْرِ عِلَّةٍ. 20فَإِنَّهُمْ لَا يَتَكَلَّمُونَ بِالسَّلامِ، وَلَكِنَّهُمْ يَتَآمَرُونَ بِمَكْرٍ لِلإِيقَاعِ بِالْمُسَالِمِينَ السَّاكِنِينَ فِي الأَرْضِ. 21فَغَرُوا علَيَّ أَفْوَاهَهُمْ عَلَى وِسْعِهَا، وَقَالُوا: «هَهْ! هَهْ! قَدْ رَأَيْنَا بِأَعْيُنِنَا (مَا فَعَلْتَ).» 22قَدْ رَأَيْتَ يَا رَبُّ ذَلِكَ. لَا تَسْكُتْ وَلَا تَبْتَعِدْ عَنِّي. 23انْهَضْ يَا إِلَهِي وَسَيِّدِي وَاسْتَيْقِظْ لإِحْقَاقِ حَقِّي وَإِنْصَافِ دَعْوَايَ. 24احْكُمْ بِبَرَاءَتِي يَا رَبُّ يَا إِلَهِي حَسَبَ عَدْلِكَ، وَلَا تَدَعْهُمْ يَشْمَتُونَ بِي. 25لِئَلّا يَقُولُوا فِي أَنْفُسِهِمْ: «هَهْ! قَدْ ظَفِرْنَا بِهِ» أَوْ يَقُولُوا: «قَدِ ابْتَلَعْنَاهُ!» 26لِيَخْزَ وَيَخْجَلْ جَمِيعُ الشَّامِتِينَ بِي فِي مُصِيبَتِي. لِيَرْتَدِ الْمُتَعَظِّمُونَ عَلَيَّ لِبَاسَ الْخِزْيِ وَالْعَارِ. 27وَلْيَهْتِفِ الْمَسْرُورُونَ بِبِرِّي بِهُتَافِ الْفَرَحِ وَالابْتِهَاجِ، قَائِلِينَ فِي كُلِّ حِينٍ: «لِيَتَمَجَّدِ الرَّبُّ الَّذِي يَبْتَهِجُ بِنَجَاحِ عَبْدِهِ». 28فَيُذِيعَ لِسَانِي عَدْلَكَ، وَيَتَرَنَّمَ بِحَمْدِكَ النَّهَارَ كُلَّهُ.