Zaburi 29 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 29:1-11

Zaburi 29

Sauti Ya Bwana Wakati Wa Dhoruba

Zaburi ya Daudi.

129:1 1Nya 16:28; 2Sam 1:19; Isa 10:13; Za 103:20; 8:1Mpeni Bwana, enyi mashujaa,

mpeni Bwana utukufu na nguvu.

229:2 1Nya 16:29; Za 96:7-9Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake;

mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.

329:3 Ay 37:5; Za 24:7; 18:13; 46:6; 68:33; 77:17; Mdo 7:2; 1Sam 2:10; Yer 10:13; 25:30; Yoe 2:11; Amo 1:2; Kut 15:10Sauti ya Bwana iko juu ya maji;

Mungu wa utukufu hupiga radi,

Bwana hupiga radi juu ya maji makuu.

429:4 Za 68:33Sauti ya Bwana ina nguvu;

sauti ya Bwana ni tukufu.

529:5 Amu 9:15Sauti ya Bwana huvunja mierezi;

Bwana huvunja vipande vipande

mierezi ya Lebanoni.

629:6 Za 92:10; 114:4; Kum 3:9; Ay 39:9; Hes 23:22Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama,

Sirioni29:6 Yaani Mlima Hermoni. urukaruke kama mwana nyati.

729:7 Eze 1:14; Ufu 8:5Sauti ya Bwana hupiga kwa miali

ya umeme wa radi.

829:8 Hes 13:26; 20:1Sauti ya Bwana hutikisa jangwa;

Bwana hutikisa Jangwa la Kadeshi.

929:9 Isa 2:13; Eze 27:6; Amo 2:9; Za 26:8Sauti ya Bwana huzalisha ayala,

na huuacha msitu wazi.

Hekaluni mwake wote wasema,

“Utukufu!”

1029:10 Mwa 6:17; Kut 15:18Bwana huketi akiwa ametawazwa juu ya gharika;

Bwana ametawazwa kuwa Mfalme milele.

1129:11 Za 18:1; 28:8; 68:35; Law 26:6; Hes 6:26; Isa 40:29Bwana huwapa watu wake nguvu;

Bwana huwabariki watu wake kwa kuwapa amani.