Zaburi 28 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 28:1-9

Zaburi 28

Kuomba Msaada

Zaburi ya Daudi.

128:1 Kum 1:45; Es 4:14; Ay 33:18Ninakuita wewe, Ee Bwana, Mwamba wangu;

usiwe kwangu kama kiziwi.

Kwa sababu ukinyamaza

nitafanana na walioshuka shimoni.

228:2 Za 17:1; 61:1; 5:7; 11:4; 116:1; 63:4; 130:2; 142:1; 143:1; 141:2; Mao 2:19; Ezr 9:5; 1Tim 2:8Sikia kilio changu unihurumie

ninapokuita kwa ajili ya msaada,

niinuapo mikono yangu kuelekea

Patakatifu pa Patakatifu pako.

328:3 Za 12:2; 26:4; 55:21; Yer 9:8Usiniburute pamoja na waovu,

pamoja na hao watendao mabaya,

ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri,

lakini mioyoni mwao wameficha chuki.

428:4 Za 62:12; 2Tim 4:14; Mao 3:64; Ufu 18:6; 22:12Walipe sawasawa na matendo yao,

sawasawa na matendo yao maovu;

walipe sawasawa na kazi za mikono yao,

uwalipe wanavyostahili.

528:5 Isa 5:12Kwa kuwa hawaheshimu kazi za Bwana,

na yale ambayo mikono yake imetenda,

atawabomoa na kamwe

hatawajenga tena.

628:6 Mwa 24:27; Efe 1:3; 2Kor 1:3; 1Pet 1:3Bwana asifiwe,

kwa maana amesikia kilio changu

nikimwomba anihurumie.

728:7 Za 144:9; 13:5; 16:9; 33:3; 40:3; 69:30; 149:1; 18:1; 112:7; Isa 26:3; Kum 16:15Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu,

moyo wangu umemtumaini yeye,

nami nimesaidiwa.

Moyo wangu unarukaruka kwa furaha

nami nitamshukuru kwa wimbo.

828:8 Za 18:1; 27:1; 20:6; Kut 15:2; Hab 3:13Bwana ni nguvu ya watu wake,

ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.

928:9 Za 78:52, 71; 80:1; 106:47; 118:25; 23:1; 1Nya 6:35; 11:2; Kut 34:9; Isa 40:11; 46:3; 63:9; Eze 34:12; Yer 31:10; Mik 7:14; Kum 1:31; 32:11Waokoe watu wako na uubariki urithi wako;

uwe mchungaji wao na uwabebe milele.

New International Version

Psalms 28:1-9

Psalm 28

Of David.

1To you, Lord, I call;

you are my Rock,

do not turn a deaf ear to me.

For if you remain silent,

I will be like those who go down to the pit.

2Hear my cry for mercy

as I call to you for help,

as I lift up my hands

toward your Most Holy Place.

3Do not drag me away with the wicked,

with those who do evil,

who speak cordially with their neighbors

but harbor malice in their hearts.

4Repay them for their deeds

and for their evil work;

repay them for what their hands have done

and bring back on them what they deserve.

5Because they have no regard for the deeds of the Lord

and what his hands have done,

he will tear them down

and never build them up again.

6Praise be to the Lord,

for he has heard my cry for mercy.

7The Lord is my strength and my shield;

my heart trusts in him, and he helps me.

My heart leaps for joy,

and with my song I praise him.

8The Lord is the strength of his people,

a fortress of salvation for his anointed one.

9Save your people and bless your inheritance;

be their shepherd and carry them forever.