Zaburi 28 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 28:1-9

Zaburi 28

Kuomba Msaada

Zaburi ya Daudi.

128:1 Kum 1:45; Es 4:14; Ay 33:18Ninakuita wewe, Ee Bwana, Mwamba wangu;

usiwe kwangu kama kiziwi.

Kwa sababu ukinyamaza

nitafanana na walioshuka shimoni.

228:2 Za 17:1; 61:1; 5:7; 11:4; 116:1; 63:4; 130:2; 142:1; 143:1; 141:2; Mao 2:19; Ezr 9:5; 1Tim 2:8Sikia kilio changu unihurumie

ninapokuita kwa ajili ya msaada,

niinuapo mikono yangu kuelekea

Patakatifu pa Patakatifu pako.

328:3 Za 12:2; 26:4; 55:21; Yer 9:8Usiniburute pamoja na waovu,

pamoja na hao watendao mabaya,

ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri,

lakini mioyoni mwao wameficha chuki.

428:4 Za 62:12; 2Tim 4:14; Mao 3:64; Ufu 18:6; 22:12Walipe sawasawa na matendo yao,

sawasawa na matendo yao maovu;

walipe sawasawa na kazi za mikono yao,

uwalipe wanavyostahili.

528:5 Isa 5:12Kwa kuwa hawaheshimu kazi za Bwana,

na yale ambayo mikono yake imetenda,

atawabomoa na kamwe

hatawajenga tena.

628:6 Mwa 24:27; Efe 1:3; 2Kor 1:3; 1Pet 1:3Bwana asifiwe,

kwa maana amesikia kilio changu

nikimwomba anihurumie.

728:7 Za 144:9; 13:5; 16:9; 33:3; 40:3; 69:30; 149:1; 18:1; 112:7; Isa 26:3; Kum 16:15Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu,

moyo wangu umemtumaini yeye,

nami nimesaidiwa.

Moyo wangu unarukaruka kwa furaha

nami nitamshukuru kwa wimbo.

828:8 Za 18:1; 27:1; 20:6; Kut 15:2; Hab 3:13Bwana ni nguvu ya watu wake,

ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.

928:9 Za 78:52, 71; 80:1; 106:47; 118:25; 23:1; 1Nya 6:35; 11:2; Kut 34:9; Isa 40:11; 46:3; 63:9; Eze 34:12; Yer 31:10; Mik 7:14; Kum 1:31; 32:11Waokoe watu wako na uubariki urithi wako;

uwe mchungaji wao na uwabebe milele.

New Arabic Version

مزمور 28:1-9

الْمَزْمُورُ الثَّامِنُ وَالْعِشْرُونَ

لِدَاوُدَ

1يَا رَبُّ إِلَيْكَ أَصْرُخُ، فَلَا تَتَصَامَمْ عَنِّي يَا صَخْرَتِي، لِئَلّا أَكُونَ، إِذَا سَكَتَّ عَنِّي، مِثْلَ الْمُنْحَدِرِينَ إِلَى الْهَاوِيَةِ. 2اسْتَمِعْ صَوْتَ تَضَرُّعِي عِنْدَمَا أَسْتَغِيثُ بِكَ، رَافِعاً يَدَيَّ نَحْوَ مِحْرَابِ قَدَاسَتِكَ. 3لَا تَطْرَحْنِي مَعَ الأَشْرَارِ وَفَاعِلِي الإِثْمِ، الَّذِينَ يُظْهِرُونَ الْوُدَّ لأَصْحَابِهِمْ، وَهُمْ يَكُنُّونَ لَهُمُ الشَّرَّ فِي قُلُوبِهِمْ. 4جَازِهِمْ وَفْقاً لِفِعْلِهِمْ وَشَرِّ أَعْمَالِهِمْ. أَعْطِهِمْ مَا يَسْتَحِقُّ صَنِيعُ أَيْدِيهِمْ، وَرُدَّ عَلَيْهِمْ جَزَاءَهُمْ. 5وَلأَنَّهُمْ لَا يُبَالُونَ بِأَفْعَالِ الرَّبِّ وَلَا بِصَنِيعِ يَدَيْهِ، فَإِنَّهُ يُدَمِّرُهُمْ وَلَا يُعِيدُ بِنَاءَهُمْ.

6مُبَارَكٌ الرَّبُّ فَقَدْ سَمِعَ صَوْتَ تَضَرُّعِي. 7الرَّبُّ قُوَّتِي وَتُرْسِي. عَلَيْهِ اتَّكَلَ قَلْبِي، فَنِلْتُ الْغَوْثَ. لِذَلِكَ يَبْتَهِجُ قَلْبِي وَأَحْمَدُهُ بِنَشِيدِي. 8الرَّبُّ قُوَّةُ شَعْبِهِ، وَهُوَ حِصْنُ خَلاصِ مَسِيحِهِ. 9خَلِّصْ يَا رَبُّ شَعْبَكَ وَبَارِكْ مِيرَاثَكَ. كُنْ رَاعِياً لَهُمْ وَاحْمِلْهُمْ إِلَى الأَبَدِ.