Zaburi 27 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 27:1-14

Zaburi 27

Sala Ya Kusifu

Zaburi ya Daudi.

127:1 2Sam 22:29; Ay 13:5; Za 3:8; 9:9; 56:4, 11; 118:6; Kut 15:2Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu,

nimwogope nani?

Bwana ni ngome ya uzima wangu,

nimhofu nani?

227:2 Za 9:3; 20:8; 37:24; Dan 11:19; Rum 11:11Waovu watakaposogea dhidi yangu

ili wanile nyama yangu,

adui zangu na watesi wangu watakaponishambulia,

watajikwaa na kuanguka.

327:3 Mwa 4:7; Za 3:6; Ay 4:6Hata jeshi linizunguke pande zote,

moyo wangu hautaogopa;

hata vita vitokee dhidi yangu,

hata hapo nitakuwa na ujasiri.

427:4 Lk 10:42; Za 23:6; 61:4Jambo moja ninamwomba Bwana,

hili ndilo ninalolitafuta:

niweze kukaa nyumbani mwa Bwana

siku zote za maisha yangu,

niutazame uzuri wa Bwana

na kumtafuta hekaluni mwake.

527:5 Ay 38:23; Za 12:7, 8; 40:2Kwa kuwa siku ya shida,

atanihifadhi salama katika maskani yake,

atanificha uvulini mwa hema yake

na kuniweka juu kwenye mwamba.

627:6 2Sam 22:49; Za 3:3; 33:2; 54:6; 18:48; 22:12; 92:1; 50:14; 107:22; 116:17; 147:7; Ezr 3:13; Ay 22:26; Kut 15:1; Efe 5:19Kisha kichwa changu kitainuliwa

juu ya adui zangu wanaonizunguka.

Katika maskani yake nitatoa dhabihu kwa kelele za shangwe;

nitamwimbia Bwana na kumsifu.

727:7 Za 4:1; 5:3; 18:6; 55:17; 119:149; 130:2; Isa 28:23Isikie sauti yangu nikuitapo, Ee Bwana,

unihurumie na unijibu.

827:8 1Nya 16:11Moyo wangu unasema kuhusu wewe,

“Utafute uso wake!”

Uso wako, Bwana “Nitautafuta.”

927:9 Za 2:5; 119:8; 18:46; 22:24; 37:28; Mwa 49:25; Kum 31:17; 33:29; 4:31; Isa 41:17; 62:12; Yer 14:9Usinifiche uso wako,

usimkatae mtumishi wako kwa hasira;

wewe umekuwa msaada wangu.

Usinikatae wala usiniache,

Ee Mungu Mwokozi wangu.

10Hata kama baba yangu na mama wakiniacha,

Bwana atanipokea.

1127:11 Ezr 8:21; Za 5:8; 72:4; 78:42; 106:10; Yer 21:12; Kut 33:13Nifundishe njia yako, Ee Bwana,

niongoze katika njia iliyonyooka

kwa sababu ya watesi wangu.

1227:12 Kum 19:16; Mt 26:60; Mdo 6:13; 1Kor 15:15Usiniachilie kwa nia za adui zangu,

kwa maana mashahidi wa uongo

wameinuka dhidi yangu,

wakipumua ujeuri.

1327:13 Kut 33:19; 2Nya 6:41; Za 33:6; 31:19; 145:7; Ay 18:13Nami bado nina tumaini hili:

nitauona wema wa Bwana

katika nchi ya walio hai.

1427:14 Efe 6:10; Amu 5:21; Kum 1:21; Sef 3:8; Hab 2:3; Za 33:20; 130:5, 6; Mdo 1:4; Isa 8:17; 30:18Mngojee Bwana,

uwe hodari na mwenye moyo mkuu,

nawe, umngojee Bwana.