Zaburi 21 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 21:1-13

Zaburi 21

Shukrani Kwa Mungu Kwa Ajili Ya Ushindi

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

121:1 1Sam 2:10; 2Sam 22:51Ee Bwana, mfalme huzifurahia nguvu zako.

Tazama jinsi ilivyo kuu furaha yake

kwa ushindi unaompa!

221:2 Za 20:4; Yn 11:42Umempa haja ya moyo wake

na hukumzuilia maombi ya midomo yake.

321:3 2Sam 12:30; Ufu 14:14; Zek 6:11Ulimkaribisha kwa baraka tele

na kumvika taji ya dhahabu safi kichwani pake.

421:4 Za 10:16; 45:17; 48:14; 133:3; 2Sam 7:19Alikuomba maisha, nawe ukampa,

wingi wa siku milele na milele.

521:5 Za 18:50; 44:4; 8:5; 45:3; 93:1; 96:6; 104:1Kutokana na ushindi uliompa, utukufu wake ni mkubwa,

umeweka juu yake fahari na utukufu.

621:6 Za 43:4; 126:3; 1Nya 17:27Hakika umempa baraka za milele,

umemfanya awe na furaha

kwa shangwe ya uwepo wako.

721:7 2Fal 18:5; Za 6:4; 15:5; 55:22; 91:7; Mwa 14:18Kwa kuwa mfalme anamtumaini Bwana;

kwa upendo usiokoma wa Aliye Juu Sana hatatikiswa.

821:8 Isa 10:10Mkono wako utawashika adui zako wote,

mkono wako wa kuume utawakamata adui zako.

921:9 Kum 32:22; Yer 15:14Wakati utakapojitokeza

utawafanya kama tanuru ya moto.

Katika ghadhabu yake Bwana atawameza,

moto wake utawateketeza.

1021:10 Kum 28:18Utawaangamiza wazao wao kutoka duniani,

uzao wao kutoka wanadamu.

1121:11 Za 2:1; 10:2; 26:10; 37:7; Ay 10:3Ingawa watapanga mabaya dhidi yako

na kutunga hila, hawawezi kufanikiwa,

1221:12 Kut 23:27kwa kuwa utawafanya wakimbie

utakapowalenga usoni pao

kwa mshale kutoka kwenye upinde wako.

1321:13 Za 18:46; Ufu 15:3, 4Ee Bwana, utukuzwe katika nguvu zako,

tutaimba na kusifu nguvu zako.