Zaburi 18 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 18:1-50

Zaburi 18

Wimbo Wa Daudi Wa Ushindi

(2 Samweli 22:1-51)

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana aliyomwimbia Bwana wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. Alisema hivi:

118:1 Kut 15:2; Yer 16:19; Kum 32:4; 33:29; Za 91:2; 22:19; 59:9; 81:1; 1Sam 2:2; Isa 2:10; 12:2; 49:5Nakupenda wewe, Ee Bwana,

nguvu yangu.

218:2 Kut 33:22; Isa 2:1; 17:10; Yer 16:19; Za 40:17; 114:2; 2:12; 9:9; 94:20; 28:7, 8; 31:2, 3; 84:9; 119:114; Ebr 2:13; Mwa 15:1; Lk 1:69Bwana ni mwamba wangu,

ngome yangu na mwokozi wangu,

Mungu wangu ni mwamba,

ambaye kwake ninakimbilia.

Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu,

ngome yangu.

318:3 1Nya 16:25; Za 9:13; 76:4Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa,

nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.

418:4 Za 116:4; 93:4; 124:6; Eze 43:2; Isa 5:30; 17:12; Yer 6:23; 51:42, 55Kamba za mauti zilinizunguka,

mafuriko ya maangamizi yalinilemea.

518:5 Mit 14:13Kamba za kuzimu zilinizunguka,

mitego ya mauti ilinikabili.

618:6 Kum 4:30; Za 30:2; 99:6; 102; 120:1; 66:19; 116:1; Ay 16:18Katika shida yangu nalimwita Bwana,

nilimlilia Mungu wangu anisaidie.

Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu,

kilio changu kikafika mbele zake,

masikioni mwake.

718:7 Za 97:4; Isa 5:25; 64:3; Amu 5:4, 5; Ay 9:5; Yer 10:10; Mdo 4:31Dunia ilitetemeka na kutikisika,

misingi ya milima ikatikisika,

vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.

818:8 Ay 41:20, 21; Kut 15:17; 19:18; Mit 25:22; Za 50:3; 97:3; Dan 7:10; Rum 12:20Moshi ukapanda kutoka puani mwake,

moto uteketezao ukatoka kinywani mwake,

makaa ya moto yawakayo

yakatoka ndani mwake.

918:9 Mwa 11:5; Isa 64:1; Za 57:3; 104:3; Kut 20:21; Kum 33:26Akazipasua mbingu akashuka chini,

mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.

1018:10 Mwa 3:24; Eze 10:18; Kum 33:26; Za 104:3; 99:1Alipanda juu ya kerubi akaruka,

akapaa juu kwa mbawa za upepo.

1118:11 Za 97:2; Kut 19:9; Ay 22:14; Isa 4:5; Kum 4:11; Yer 43:10Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika,

hema lake kumzunguka,

mawingu meusi ya mvua ya angani.

1218:12 Za 104:2; Yos 10:10; Ay 36:30Kutokana na mwanga wa uwepo wake

mawingu yalisogea,

ikanyesha mvua ya mawe

na umeme wa radi.

1318:13 Kut 9:23; Za 29:3; 2Sam 2:10Bwana alinguruma kutoka mbinguni,

sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.

1418:14 Kum 32:23; Ay 6:4; 36:30; Ufu 4:5; Za 21:12; Amu 4:15; Hes 24:8Aliipiga mishale yake na kutawanya adui,

naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza.

1518:15 Za 11:3; 76:6; 104:7; 106:9; Isa 50:2; Kut 15:8Mabonde ya bahari yalifunuliwa,

na misingi ya dunia ikawa wazi

kwa kukaripia kwako, Ee Bwana,

kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako.

1618:16 Kut 15:5; Mit 18:4; 20:5; Za 69:2; 144:7Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika;

alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.

1718:17 Za 38:19; 59:1; 143:9; Amu 18:26Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi,

kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.

1818:18 Mit 1:27; 16:4; Yer 17:17; 40:2; Oba 1:13; Za 20:2; Isa 3:1Walinikabili siku ya msiba wangu,

lakini Bwana alikuwa msaada wangu.

1918:19 Za 31:8; 118:5; Hes 14:8Alinileta nje mahali penye nafasi tele,

akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.

2018:20 1Sam 22:21; 26:23; Ay 22:30; Za 24:4; Rum 2:12; 2Nya 15:7; 1Kor 3:8; Mit 6:4Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu;

sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.

2118:21 2Nya 34:33; Za 37:34; 119:2; 102; Mit 8:32; 23:26Kwa maana nimezishika njia za Bwana;

sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.

2218:22 Za 119:30Sheria zake zote zi mbele yangu,

wala sijayaacha maagizo yake.

2318:23 Mwa 6:9Nimekuwa sina hatia mbele zake,

nami nimejilinda nisitende dhambi.

2418:24 1Sam 26:23; Rut 2:12; Mt 10:41-42Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu;

sawasawa na usafi wa mikono yangu machoni pake.

2518:25 Za 31:23; 37:23; 50:5; 25:10; 40:11; 89:24; 146:6; Mit 2:8; Mt 18:32-35Kwa yeye aliye mwaminifu, unajionyesha kuwa mwaminifu,

kwa asiye na hatia, unajionyesha kutokuwa na hatia.

2618:26 Mit 15:26; Mt 5:8; Flp 1:10; 1Tim 5:22; Tit 1:15; 1Yn 3:3; Mit 3:34; Mt 10:16; Lk 16:8; Law 26:23Kwa aliye mtakatifu, unajionyesha kuwa mtakatifu,

lakini kwa aliyepotoka, unajionyesha kuwa mkaidi.

2718:27 2Nya 33:23; Mt 23:12; Ay 41:34; Za 10:5; Mit 3:33-35; 6:17Wewe huwaokoa wanyenyekevu,

lakini huwashusha wenye kiburi.

2818:28 1Fal 11:36; Za 132:17; Ay 29:3; Za 97:11; 112:4; Yn 1:5; Mdo 26:18; 2Kor 4:6; 2Pet 1:19; Ay 18:6Wewe, Ee Bwana, unaifanya taa yangu iendelee kuwaka;

Mungu wangu hulifanya giza langu kuwa mwanga.

2918:29 Isa 45:5; Ebr 11:34Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi,

nikiwa pamoja na Mungu wangu

nitaweza kuruka ukuta.

3018:30 Kum 32:4; Za 12:6; 3:3; 2:12; Mit 30:5; Ufu 15:3; Rum 12:3Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu,

neno la Bwana halina dosari.

Yeye ni ngao kwa wote

wanaokimbilia kwake.

3118:31 Kum 4:5; 32:39; Za 35:10; 86:8; 89:6; Isa 46:9; 44:6, 8; 45:5, 6, 14, 18, 21; Mwa 49:24Kwa maana ni nani aliye Mungu

zaidi ya Bwana?

Ni nani aliye Mwamba

isipokuwa Mungu wetu?

3218:32 1Pet 5:10; Yak 3:2; Za 15:2; 19:13; Ebr 10:14Mungu ndiye anivikaye nguvu

na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.

3318:33 Za 42:1; Mit 5:19; Isa 35:6; Hab 3:19; Kum 32:13Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu,

huniwezesha kusimama mahali palipo juu.

3418:34 Za 144:1Huifundisha mikono yangu kupigana vita;

mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.

3518:35 Za 3:5; 37:5, 17; 41:3; 51:2; 54:4; 55:22; 119:116; Isa 41:4, 10, 13; 43:2; 46:4Hunipa ngao yako ya ushindi,

nao mkono wako wa kuume hunitegemeza,

unajishusha chini ili kuniinua.

3618:36 Ay 18:7; Za 31:8; 66:9Huyapanua mapito yangu,

ili miguu yangu isiteleze.

3718:37 Law 26:7Niliwafuatia adui zangu na nikawapata,

sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.

3818:38 Za 68:21; 110:6; 36:12; 47:3; 140:10; Isa 26:14Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena;

walianguka chini ya miguu yangu.

3918:39 Za 18:32, 47; Isa 45:5, 24; Za 47:3; 144:2Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita;

uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.

4018:40 Yos 7:12; Za 18:37Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia,

nami nikawaangamiza adui zangu.

4118:41 2Fal 14:26; Za 50:22; 1Sam 8:18; 14:37; Yer 11:11; Mit 1:28Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa;

walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.

4218:42 Kum 9:21; Isa 2:22Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo;

niliwamwaga nje kama tope barabarani.

4318:43 2Sam 8:1-14; Isa 55:5Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu;

umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa,

watu ambao sikuwajua wananitumikia.

4418:44 Za 144:7, 11; 54:3; Isa 25:5Mara wanisikiapo hunitii,

wageni hunyenyekea mbele yangu.

4518:45 2Kor 4:1; Ebr 12:3; 1Sam 17:32; Isa 66:2; Hos 3:5; 11:10; Za 9:9; Mik 7:17Wote wanalegea,

wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.

4618:46 Yos 3:10; 2Kor 13:4; 1Sam 14:39; Kut 33:22; Za 21:13; 35:27; 40:16; 108:5; 1Nya 16:35; Lk 1:47; Yer 10:10Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu!

Atukuzwe Mungu Mwokozi wangu!

4718:47 Mwa 4:24; Za 18:29; Amu 4:23Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi,

awatiishaye mataifa chini yangu,

4818:48 Dan 3:17; Za 7:10; 37:40; 140:2; 18:49aniokoaye na adui zangu.

Uliniinua juu ya adui zangu;

uliniokoa toka kwa watu wajeuri.

4918:49 Za 101:1; 7:17; 9:2; 108:1; 146:2; Rum 15:9Kwa hiyo nitakusifu katikati ya mataifa, Ee Bwana;

nitaliimbia sifa jina lako.

5018:50 2Sam 23:1; Za 144:10; 89:4Humpa mfalme wake ushindi mkuu,

huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake,

kwa Daudi na wazao wake milele.

New Arabic Version

مزمور 18:1-50

الْمَزْمُورُ الثَّامِنُ عَشَرَ

لِقَائِدِ الْمُنْشِدِينَ. لِعَبْدِ الرَّبِّ دَاوُدَ. قَصِيدَةٌ خَاطَبَ بِها الرَّبَّ يَوْمَ أَنْقَذَهُ مِنْ قَبْضَةِ كُلِّ أَعْدَائِهِ وَمِنْ يَدِ شَاوُلَ. فَقَالَ:

1أُحِبُّكَ يَا رَبُّ، يَا قُوَّتِي. 2الرَّبُّ صَخْرَتِي وَحِصْنِي وَمُنْقِذِي. إِلَهِي صَخْرَتِي بِهِ أَحْتَمِي. تُرْسِي وَرُكْنُ خَلاصِي، وَقَلْعَتِي الْحَصِينَةُ. 3أَدْعُو الرَّبَّ الْجَدِيرَ بِكُلِّ حَمْدٍ فَيُخَلِّصُنِي مِنْ أَعْدَائِي. 4قَدْ أَحْدَقَتْ بِي حِبَالُ الْمَوْتِ، وَأَفْزَعَتْنِي سُيُولُ الْهَلاكِ. 5أَحَاطَتْ بِي حِبَالُ الْهَاوِيَةِ، وَأَطْبَقَتْ عَلَيَّ فِخَاخُ الْمَوْتِ. 6فِي ضِيقِي دَعَوْتُ الرَّبَّ وَصَرَخْتُ إِلَى إِلَهِي، فَسَمِعَ صَوْتِي مِنْ هَيْكَلِهِ، وَصَعِدَ صُرَاخِي أَمَامَهُ، بَلْ دَخَلَ أُذُنَيْهِ. 7عِنْدَئِذٍ ارْتَجَّتِ الأَرْضُ وَتَزَلْزَلَتْ. ارْتَجَفَتْ أَسَاسَاتُ الْجِبَالِ وَاهْتَزَّتْ، لأَنَّ الرَّبَّ غَضِبَ. 8نَفَثَ أَنْفُهُ دُخَاناً، وَانْقَذَفَتْ نَارٌ آكِلَةٌ مِنْ فَمِهِ، وَكَأَنَّهَا جَمْرٌ مُلْتَهِبٌ. 9طَأْطَأَ السَّمَاوَاتِ وَنَزَلَ، فَكَانَتِ الْغُيُومُ الْمُتَجَهِّمَةُ تَحْتَ قَدَمَيْهِ. 10امْتَطَى مَرْكَبَةً مِنْ مَلائِكَةِ الْكَرُوبِيمِ، وَطَارَ مُسْرِعاً عَلَى أَجْنِحَةِ الرِّيْاحِ. 11جَعَلَ الظُّلْمَةَ سِتَاراً لَهُ، وَصَارَ ضَبَابُ الْمِيَاهِ وَسُحُبُ الْسَّمَاءِ الدَّاكِنَةُ مِظَلَّتَهُ الْمُحِيطَةَ بِهِ. 12مِنْ بَهَاءِ طَلْعَتِهِ عَبَرَتِ السُّحُبُ أَمَامَهُ. حَدَثَتْ عَاصِفَةُ بَرَدٍ وَبَرْقٍ كَالْجَمْرِ الْمُلْتَهِبِ. 13أَرْعَدَ الرَّبُّ فِي السَّمَاوَاتِ، أَطْلَقَ الْعَلِيُّ صَوْتَهُ فَانْهَمَرَ بَرَدٌ، وَانْدَلَعَتْ نَارُ! 14أَطْلَقَ سِهَامَهُ فَبَدَّدَ أَعْدَائِي، وَأَرْسَلَ بُرُوقَهُ فَأَزْعَجَهُمْ. 15ظَهَرَتْ مَجَارِي الْمِيَاهِ الْعَمِيقَةِ، وَانْكَشَفَتْ أُسُسُ الْمَسْكُونَةِ مِنْ زَجْرِكَ يَا رَبُّ، وَمِنْ أَنْفِكَ اللّافِحَةِ. 16مَدَّ الرَّبُّ يَدَهُ مِنَ الْعُلَى وَأَمْسَكَنِي، وَانْتَشَلَنِي مِنَ السُّيُولِ الْغَامِرَةِ. 17أَنْقَذَنِي مِنْ عَدُوِّي الْقَويِّ، وَمِنَ مُبْغِضِيَّ، لأَنَّهُمْ كَانُوا أَقْوَى مِنِّي. 18تَصَدَّوْا لِي فِي يَوْمِ بَلِيَّتِي، فَكَانَ الرَّبُّ سَنَدِي، 19وَاقْتَادَنِي إِلَى مَكَانٍ رَحِيبٍ. أَنْقَذَنِي لأَنَّهُ سُرَّ بِي. 20يُكَافِئُنِي الرَّبُّ بِمُقْتَضَى بِرِّي وَيُعَوِّضُنِي حَسَبَ طَهَارَةِ يَدَيَّ، 21لأَنِّي سَلَكْتُ دَائِماً فِي طُرُقِ الرَّبِّ وَلَمْ أَعْصَ إِلَهِي. 22جَعَلْتُ أَحْكَامَهُ دَائِماً نُصْبَ عَيْنَيَّ، وَلَمْ أَحِدْ عَنْ فَرَائِضِهِ. 23وَأَكُونُ مَعَهُ كَامِلاً وَأَصُونُ نَفْسِي مِنْ إِثْمِي. 24فَيُكَافِئُنِي الرَّبُّ وَفْقاً لِبِرِّي، بِحَسَبِ طَهَارَةِ يَدَيَّ أَمَامَ عَيْنَيْهِ.

25مَعَ الرَّحِيمِ تَكُونُ رَحِيماً، وَمَعَ الْكَامِلِ تَكُونُ كَامِلاً، 26وَمَعَ الطَّاهِرِ تَكُونُ طَاهِراً، وَمَعَ الْمُعْوَجِّ تَكُونُ مُعْوَجّاً. 27لأَنَّكَ أَنْتَ تُخَلِّصُ الشَّعْبَ الْمُتَضَايِقَ، أَمَّا الْمُتَرَفِّعُونَ فَتَخْفِضُ عُيُونَهُمْ. 28لأَنَّكَ أَيُّهَا الرَّبُّ إِلَهِي تَضِيءُ مِصْبَاحِي، وَتُحَوِّلُ ظَلامِي نُوراً 29لأَنِّي بِكَ اقْتَحَمْتُ جَيْشاً، وَبِمَعُونَةِ إِلَهِي اخْتَرَقْتُ أَسْوَاراً. 30مَا أَكْمَلَ طَرِيقَ الرَّبِّ! إِنَّ كَلِمَتَهُ نَقِيَّةٌ، وَهُوَ تُرْسٌ يَحْمِي جَمِيعَ الْمُلْتَجِئِينَ إِلَيْهِ. 31فَمَنْ هُوَ إِلْهٌ غَيْرُ الرَّبِّ؟ وَمَنْ هُوَ صَخْرَةٌ سِوَى إِلَهِنَا؟ 32يَشُدُّنِي اللهُ بِحِزامٍ مِنَ الْقُوَّةِ، وَيَجْعَلُ طَرِيقِي كَامِلاً، 33يُثَبِّتُ قَدَمَيَّ كَأَقْدَامِ الإيَّلِ وَيُصْعِدُنِي عَلَى مُرْتَفَعَاتِي الْوَعِرَةِ. 34يُدَرِّبُ يَدَيَّ عَلَى فَنِّ الْحَرْبِ، فَتَشُدُّ ذِرَاعَايَ قَوْساً مِنْ نُحَاسٍ. 35تَجْعَلُ أَيْضاً خَلاصَكَ تُرْساً لِي، فَتُعَضِّدُنِي بِيَمِينِكَ، وَيُعَظِّمُنِي لُطْفُكَ. 36وَسَّعْتَ طَرِيقِي تَحْتَ قَدَمَيَّ، فَلَمْ تَتَقَلْقَلْ عَقِبَايَ. 37أُطَارِدُ أَعْدَائِي فَأُدْرِكُهُمْ، وَلَا أَرْجِعُ حَتَّى أُبِيدَهُمْ. 38أَسْحَقُهُمْ فَلَا يَسْتَطِيعُونَ النُّهُوضَ. يَسْقُطُونَ تَحْتَ قَدَمَيَّ. 39تُمَنْطِقُنِي بِحِزَامٍ مِنَ الْقُوَّةِ تَأَهُّباً لِلْقِتَالِ. تُخْضِعُ لِسُلْطَانِي الْمُتَمَرِّدِينَ عَلَيَّ. 40يُوَلُّونَ الأَدْبَارَ هَرَباً أَمَامِي. وَأُفْنِي الَّذِينَ يُبْغِضُونَنِي. 41يَسْتَغِيثُونَ وَلَا مُخَلِّصَ. يُنَادُونَ الرَّبَّ فَلَا يَسْتَجِيبُ لَهُمْ. 42فَأَسْحَقُهُمْ كَالْغُبَارِ فِي مَهَبِّ الرِّيحِ، وَأَطْرَحُهُمْ مِثْلَ الطِّينِ فِي الشَّوَارِعِ. 43تُنْقِذُنِي مِنْ ثَوْرَاتِ الشَّعْبِ، وَتَجْعَلُنِي سَيِّداً لِلأُمَمِ، حَتَّى صَارَ شَعْبٌ لَمْ أَكُنْ أَعْرِفُهُ عَبْداً يَخْدِمُنِي. 44فَمَا إِنْ يَسْمَعُوا أَمْرِي حَتَّى يُلَبُّوهُ. الْغُرَبَاءُ يَتَذَلَّلُونَ لِي 45الْغُرَبَاءُ يَخُورُونَ، يَخْرُجُونَ مِنْ حُصُونِهِمْ مُرْتَعِدِينَ. 46حَيٌّ هُوَ الرَّبُّ، وَمُبَارَكٌ صَخْرَتِي، وَمُتَعَالٍ إِلَهُ خَلاصِي، 47الإِلَهُ الْمُنْتَقِمُ لِي، يُخْضِعُ الشُّعُوبَ لِسُلْطَانِي، 48مُنْقِذِي مِنْ أَعْدَائِي، رَافِعِي عَلَى الْمُتَمَرِّدِينَ عَلَيَّ، وَمِنَ الرَّجُلِ الطَّاغِي تُخَلِّصُنِي. 49لِهَذَا أَعْتَرِفُ لَكَ بَيْنَ الأُمَمِ وَأُرَتِّلُ لاِسْمِكَ. 50يَا مَانِحَ الْخَلاصِ الْعَظِيمِ لِمَلِكِهِ، وَصَانِعَ الرَّحْمَةِ لِمَسِيحِهِ، لِدَاوُدَ وَنَسْلِهِ إِلَى الأَبَدِ.