Zaburi 16 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 16:1-11

Zaburi 16

Sala Ya Matumaini

Utenzi wa Daudi.

116:1 Za 25:20; 12:7; 2:12Ee Mungu, uniweke salama,

kwa maana kwako nimekimbilia.

216:2 Za 31:14; 73:25; 118:28; 140:6Nilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu;

pasipo wewe sina jambo jema.”

316:3 Kum 33:3; Rum 1:7; Dan 7:18; Mdo 9:13; Za 30:4; 85:8; 101:6Kwa habari ya watakatifu walioko duniani,

ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.

416:4 Za 32:10; Kut 13:13; 18:11; 20:3; Mit 23:29; Kum 18:19; 31:20Huzuni itaongezeka kwa wale

wanaokimbilia miungu mingine.

Sitazimimina sadaka zao za damu

au kutaja majina yao midomoni mwangu.

516:5 Law 2:2; Za 23:5; 75:8; 116:13; Isa 51:17; Hab 2:16; Ay 22:26; Mao 4:21Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu;

umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.

616:6 Kum 19:14; Za 104:9; Ay 22:26; Mit 8:29; Yer 5:22Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri,

hakika nimepata urithi mzuri.

716:7 Za 73:24; 42:8; 77:6; Mit 15:22; Isa 11:2; Ay 35:10Nitamsifu Bwana ambaye hunishauri,

hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.

816:8 Isa 36:15; 37:2016:8 1Fal 2:19; 1Nya 6:39; Za 73:23; 15:5Nimemweka Bwana mbele yangu daima.

Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume,

sitatikisika.

916:9 Za 4:7; 13:5; 28:7; 30:11; Kum 33:26Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia;

mwili wangu nao utapumzika salama,

1016:10 Za 30:3; 31:17; 49:15; 86:13; Mdo 2:27, 31; 13:35; Hos 13:14; 2Fal 19:22; Lk 1:35; Ay 17:14; Dan 9:24; Hes 16:30kwa maana hutaniacha kaburini,

wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu.

1116:11 Mdo 2:25-28; Mt 7:14; Isa 29:13; Za 139:24; 21:6; 80:1, 17; 30:10; 64:1; 140:6; 5:1, 2; 39:12; 142:6Umenijulisha njia ya uzima;

utanijaza na furaha mbele zako,

pamoja na furaha za milele

katika mkono wako wa kuume.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

诗篇 16:1-11

第16篇

信靠之福

大卫的诗。

1上帝啊!我投靠你,

求你保护我。

2我对耶和华说:“你是我的主,

我的福祉都从你而来。”

3世上的圣民极其尊贵,

是我所喜爱的。

4追随其他神明的人,其愁苦必有增无减。

我必不向他们的假神浇奠血祭,

口中也不提假神的名号。

5耶和华啊,你是我的一切,

你是我的福分,

你掌管我的一切。

6你用准绳量给我佳美之地,

我的产业何其美!

7我要称颂那训导我的耶和华,

我的良心也在夜间提醒我。

8我常以耶和华为念,

祂在我右边,我必不动摇。

9因此,我的心欢喜,

我的灵快乐,

我的身体也安然无恙。

10因为你不会把我的灵魂撇在阴间,

也不会让你的圣者身体朽坏。

11你把生命之路指示我,

你右手有永远的福乐,

我在你面前充满喜乐。