Zaburi 147
Kumsifu Mungu Mwenye Nguvu Zote
1147:1 Za 135:3; 33:1Msifuni Bwana.
Tazama jinsi ilivyo vyema kumwimbia Mungu wetu sifa,
jinsi inavyopendeza na kustahili kumsifu yeye!
2147:2 Za 51:18; 106:47; Kum 30:3; Isa 27:13; Yer 32:37; Eze 36:24Bwana hujenga Yerusalemu,
huwakusanya Israeli walio uhamishoni.
3147:3 Za 34:18; Isa 1:6; 61:1; Eze 34:16; Ebr 12:13; Ay 5:18; Lk 4:18Anawaponya waliovunjika mioyo
na kuvifunga vidonda vyao.
4147:4 Mwa 15:5; Isa 40:26Huzihesabu nyota
na huipa kila moja jina lake.
5147:5 Kut 14:31; Nah 1:3; 1Nya 16:25; Za 48:1; 145:3; Isa 40:28Bwana wetu ni mkuu na mwenye uwezo mwingi,
ufahamu wake hauna kikomo.
6147:6 2Nya 33:23; Za 146:8, 9; 37:9, 10; 145:20Bwana huwahifadhi wanyenyekevu
lakini huwashusha waovu mpaka mavumbini.
7147:7 Za 30:4; 33:3; 42:4; 27:6; 98:5; Efe 2:20Mwimbieni Bwana kwa shukrani,
mpigieni Mungu wetu kinubi.
8147:8 Kum 32:2; 11:14; 2Sam 1:21; Ay 26:8; 38:26; 5:10; 28:26; Za 104:14Yeye huzifunika anga kwa mawingu,
huinyeshea ardhi mvua,
na kuzifanya nyasi kuota juu ya vilima.
9147:9 Ay 38:41; Mt 6:26; Mwa 8:7; 1:30; Lk 12:24; Za 104:27, 28Huwapa chakula mifugo
na pia makinda ya kunguru yanapolia.
10147:10 1Sam 16:7; Hos 1:7; Ay 39:11; Za 33:16-17Furaha yake haipo katika nguvu za farasi,
wala furaha yake kwenye miguu ya mwanadamu.
11147:11 Za 35:27; 33:18; 103:11; 119:43; 6:4Bwana hupendezwa na wale wamchao,
wale wanaoweka tumaini lao katika upendo wake usiokoma.
12147:12 Za 48:1Mtukuze Bwana, ee Yerusalemu,
msifu Mungu wako, ee Sayuni,
13147:13 Kum 33:25; Law 25:21; Za 128:5; 134:3kwa maana huimarisha makomeo ya malango yako
na huwabariki watu wako walio ndani yako.
14147:14 Law 26:6; 2Sam 7:10; Isa 48:18; Za 132:15; Kum 32:14Huwapa amani mipakani mwenu
na kukushibisha kwa ngano safi kabisa.
15147:15 Ay 37:12; Za 33:9; 148:5; Isa 55:11Hutuma amri yake duniani,
neno lake hukimbia kasi.
16147:16 Za 148:8; Ay 37:12; 38:29Anatandaza theluji kama sufu
na kutawanya umande kama majivu.
17147:17 Kut 9:22, 23; Ay 38:22; Za 78:47Huvurumisha mvua yake ya mawe kama changarawe.
Ni nani awezaye kustahimili ukali wa baridi yake?
18147:18 Za 33:9; 107:20; 50:3Hutuma neno lake na kuviyeyusha,
huvumisha upepo wake, nayo maji hutiririka.
19147:19 Kut 20:1; Mal 4:4; Za 78:5; Yos 1:8; Kum 33:4; 2Fal 22:8; Rum 3:2; 9:4Amemfunulia Yakobo neno lake,
sheria zake na maagizo yake kwa Israeli.
20147:20 Rum 3:1-2; Kum 4:7-8, 32-34; Za 79:6; 103:1; 33:2; Mdo 14:16Hajafanya hivyo kwa taifa lingine lolote,
hawazijui sheria zake.
Msifuni Bwana.