Zaburi 138 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 138:1-8

Zaburi 138

Maombi Ya Shukrani

Zaburi ya Daudi.

1138:1 Za 95:3; 96:4; 27:6; 108:1Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote,

mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.

2138:2 1Fal 8:29; Za 74:21; 97:12; 5:7; 108:4; 115:1; 140:13; 119:9Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu,

nami nitalisifu jina lako

kwa ajili ya upendo wako

na uaminifu,

kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako

juu ya vitu vyote.

3138:3 Za 28:7; 18:6; 30:2; 99:6; 116:4; 118:5; Mit 28:1; Mdo 4:29Nilipoita, ulinijibu;

ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.

4138:4 Za 72:11; 102:15Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana,

wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.

5138:5 Za 51:14; 71:16; 145:7; 21:5Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana,

kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.

6138:6 Za 113:6; 40:4; Mt 23:12Ingawa Bwana yuko juu,

humwangalia mnyonge,

bali mwenye kiburi

yeye anamjua kutokea mbali.

7138:7 Za 7:6; 23:4; 41:2; 20:6; 60:5; 108:6; 17:7, 14; Kut 7:5Nijapopita katikati ya shida,

wewe unayahifadhi maisha yangu,

unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu,

kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.

8138:8 Flp 1:6; Ezr 3:11; Za 100:5; 51:11; Ay 10:3, 8Bwana atatimiza kusudi lake kwangu,

Ee Bwana, upendo wako wadumu milele:

usiziache kazi za mikono yako.