Zaburi 138
Maombi Ya Shukrani
Zaburi ya Daudi.
1138:1 Za 95:3; 96:4; 27:6; 108:1Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote,
mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
2138:2 1Fal 8:29; Za 74:21; 97:12; 5:7; 108:4; 115:1; 140:13; 119:9Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu,
nami nitalisifu jina lako
kwa ajili ya upendo wako
na uaminifu,
kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako
juu ya vitu vyote.
3138:3 Za 28:7; 18:6; 30:2; 99:6; 116:4; 118:5; Mit 28:1; Mdo 4:29Nilipoita, ulinijibu;
ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
4138:4 Za 72:11; 102:15Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana,
wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
5138:5 Za 51:14; 71:16; 145:7; 21:5Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana,
kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
6138:6 Za 113:6; 40:4; Mt 23:12Ingawa Bwana yuko juu,
humwangalia mnyonge,
bali mwenye kiburi
yeye anamjua kutokea mbali.
7138:7 Za 7:6; 23:4; 41:2; 20:6; 60:5; 108:6; 17:7, 14; Kut 7:5Nijapopita katikati ya shida,
wewe unayahifadhi maisha yangu,
unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu,
kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
8138:8 Flp 1:6; Ezr 3:11; Za 100:5; 51:11; Ay 10:3, 8Bwana atatimiza kusudi lake kwangu,
Ee Bwana, upendo wako wadumu milele:
usiziache kazi za mikono yako.