Zaburi 130 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 130:1-8

Zaburi 130

Kuomba Msaada

Wimbo wa kwenda juu.

1130:1 Ay 30:19Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.

2130:2 Za 27:7; 28:2, 6; 31:22; 86:6; 140:6; 2Nya 6:40Ee Bwana, sikia sauti yangu.

Masikio yako na yawe masikivu

kwa kilio changu unihurumie.

3130:3 1Sam 6:20; Ezr 9:15; Hes 1:6; Za 143:2; Ufu 6:17; Yn 8:7, 9; Rum 3:20Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi,

Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?

4130:4 Kut 34:7; Efe 1:7; 2Sam 24:14; Yer 17:5-6; 31:34; 1Fal 8:40; 2The 1:6; Za 37:2; Ebr 12:28Lakini kwako kuna msamaha,

kwa hiyo wewe unaogopwa.

5130:5 Isa 8:17; 26:8; 30:18; 49:23; Za 5:3; 119:74; 27:14Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea,

katika neno lake naweka tumaini langu.

6130:6 Za 63:6; 2Sam 23:4Nafsi yangu inamngojea Bwana

kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi,

naam, kuliko walinzi

waingojeavyo asubuhi.

7130:7 1Nya 21:13; Za 25:5; 71:14; 111:9; Rum 3:24; Isa 55:7Ee Israeli, mtumaini Bwana,

maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma,

na kwake kuna ukombozi kamili.

8130:8 Lk 1:68; Kut 34:7; Mt 1:21Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli

kutoka dhambi zao zote.