Zaburi 129 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 129:1-8

Zaburi 129

Maombi Dhidi Ya Adui Za Israeli

Wimbo wa kwenda juu.

1129:1 Kut 1:13; Eze 23:3; Za 88:15; 124:1; Hos 2:15Wamenionea mno tangu ujana wangu;

Israeli na aseme sasa:

2129:2 Yer 1:19; 15:20; 20:11wamenionea mno tangu ujana wangu,

lakini bado hawajanishinda.

3129:3 Ebr 11:26Wakulima wamelima mgongo wangu,

na kufanya mifereji yao mirefu.

4129:4 Kut 9:27; 2The 1:6; Za 37:9; 140:5Lakini Bwana ni mwenye haki;

amenifungua toka kamba za waovu.

5129:5 Mik 4:11; Za 70:2Wale wote waichukiao Sayuni

na warudishwe nyuma kwa aibu.

6129:6 Isa 37:27; 2Fal 19:26; Za 102:11; 37:2; Yer 17:5-6Wawe kama majani juu ya paa,

ambayo hunyauka kabla hayajakua;

7129:7 Kum 28:38; Za 79:12kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake,

wala akusanyaye kujaza mikono yake.

8129:8 Za 118:26; Rut 2:4Wale wapitao karibu na wasiseme,

“Baraka ya Bwana iwe juu yako;

tunakubariki katika jina la Bwana.”