Zaburi 128 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 128:1-6

Zaburi 128

Thawabu Ya Kumtii Bwana

Wimbo wa kwenda juu.

1128:1 Za 103:11; 119:1-3Heri ni wale wote wamchao Bwana,

waendao katika njia zake.

2128:2 Za 58:11; 109:11; Isa 3:10; Mwa 39:3; Mit 10:22Utakula matunda ya kazi yako;

baraka na mafanikio vitakuwa vyako.

3128:3 Mwa 49:22; Ay 29:5; Mit 5:15; Eze 19:10; Za 52:8; 144:12Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao

ndani ya nyumba yako;

wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni

kuizunguka meza yako.

4128:4 Za 1:1; 112:1Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa

mtu amchaye Bwana.

5128:5 Za 122:9; 134:3Bwana na akubariki kutoka Sayuni

siku zote za maisha yako,

na uone mafanikio ya Yerusalemu,

6128:6 Mwa 50:23; 48:11; Za 125:5nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako.

Amani iwe juu ya Israeli.