Zaburi 125 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 125:1-5

Zaburi 125

Usalama Wa Watu Wa Mungu

Wimbo wa kwenda juu.

1125:1 Za 46:5; 48:2-5; 48:12; Isa 33:20Wale wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni,

ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.

2125:2 1Nya 21:15; Za 32:10; Zek 2:4-5Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,

ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake

sasa na hata milele.

3125:3 Es 4:11; Za 89:22; Mit 22:8; Isa 13:11; 14:5; 24:10Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi

waliopewa wenye haki,

ili wenye haki wasije wakatumia

mikono yao kutenda ubaya.

4125:4 Za 119:65; 36:10Ee Bwana, watendee mema walio wema,

wale walio wanyofu wa moyo.

5125:5 Ay 23:11; Isa 59:8; Za 92:7; 128:6; Mit 2:15; 17:6; Gal 6:16Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka,

Bwana atawafukuza pamoja na watenda mabaya.

Amani iwe juu ya Israeli.