Zaburi 124 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 124:1-8

Zaburi 124

Shukrani Kwa Ukombozi Wa Israeli

Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.

1124:1 Za 129:1; Mwa 15:1; Hes 14:9; Yos 1:5Kama Bwana asingalikuwa upande wetu;

Israeli na aseme sasa:

2kama Bwana asingalikuwa upande wetu,

wakati watu walipotushambulia,

3124:3 Za 35:25; Mit 1:12; Yer 51:34wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu,

wangalitumeza tungali hai,

4124:4 Za 88:17; 18:4mafuriko yangalitugharikisha,

maji mengi yangalitufunika,

5maji yaendayo kasi

yangalituchukua.

6Bwana asifiwe,

yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.

7124:7 Za 91:3; 25:15Tumeponyoka kama ndege

kutoka mtego wa mwindaji;

mtego umevunjika,

nasi tukaokoka.

8124:8 1Sam 17:45; Mwa 1:1; Za 115:15; 121:2; 134:3; Kut 18:4; Mit 18:10; Isa 50:10Msaada wetu ni katika jina la Bwana,

Muumba wa mbingu na dunia.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

詩篇 124:1-8

第124篇

上帝保護祂的子民

大衛的上聖殿朝聖之詩。

1以色列人說:

若不是耶和華幫助我們,

2若不是耶和華幫助我們,

人們起來攻擊我們、

3向我們發怒的時候,

我們早已被他們生吞,

4被狂濤淹沒,被洪流捲走,

5被怒海吞噬。

6耶和華當受稱頌!

祂沒有讓我們像獵物一樣被敵人撕咬。

7我們像鳥一樣逃出了獵人的網羅。

網羅破裂,我們逃了出去。

8我們的幫助來自創造天地的耶和華的名。