Zaburi 121
Bwana Mlinzi Wetu
Wimbo wa kwenda juu.
1Nayainua macho yangu nitazame vilima,
msaada wangu utatoka wapi?
2121:2 Mwa 1:1; Za 104:5Msaada wangu hutoka kwa Bwana,
Muumba wa mbingu na dunia.
3121:3 1Sam 2:9; Isa 27:3Hatauacha mguu wako uteleze,
yeye akulindaye hatasinzia,
4121:4 Za 127:1hakika, yeye alindaye Israeli
hatasinzia wala hatalala usingizi.
5121:5 Za 1:6Bwana anakulinda,
Bwana ni uvuli wako mkono wako wa kuume,
6121:6 Isa 49:10jua halitakudhuru mchana,
wala mwezi wakati wa usiku.
7121:7 Za 9:9, 10; 91:9, 10; Ay 5:19; Mit 12:21Bwana atakukinga na madhara yote,
atayalinda maisha yako,
8121:8 Kum 28:6; Mit 2:8Bwana atakulinda unapoingia na unapotoka,
tangu sasa na hata milele.