Zaburi 120 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 120:1-7

Zaburi 120

Kuomba Msaada

Wimbo wa kwenda juu.

1120:1 2Sam 22:7; Za 18:1; 118:5Katika dhiki yangu namwita Bwana,

naye hunijibu.

2120:2 Za 31:18; 52:4Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo

na ndimi za udanganyifu.

3Atakufanyia nini,

au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?

4120:4 Kum 32:23Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa,

kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.

5120:5 Mwa 25:13; 2:10; Yer 2:10; 49:28; 1Sam 25:1Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki,

kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!

6Nimeishi muda mrefu mno

miongoni mwa wale wanaochukia amani.

7Mimi ni mtu wa amani;

lakini ninaposema, wao wanataka vita.