Zaburi 115 – Kiswahili Contemporary Version NEN

Kiswahili Contemporary Version

Zaburi 115:1-18

Zaburi 115

Mungu Mmoja Wa Kweli

1115:1 Za 29:2; 96:8; Kut 34:6Sio kwetu sisi, Ee Bwana, sio kwetu sisi,

bali utukufu ni kwa jina lako,

kwa sababu ya upendo

na uaminifu wako.

2115:2 Za 42:3, 10; 79:10; Yoe 2:17Kwa nini mataifa waseme,

“Yuko wapi Mungu wao?”

3115:3 Ezr 5:11; Neh 1:4; Za 136:26; 135:6; 103:19; Mit 6:9; Dan 4:35; 1Nya 16:26Mungu wetu yuko mbinguni,

naye hufanya lolote limpendezalo.

4115:4 2Fal 19:18; 2Nya 32:19; Yer 10:3-5; Mdo 19:26; Kum 4:28; Ufu 9:20; Za 135:15, 16; Isa 40:19; Hos 8:6; 1Kor 10:19, 20Lakini sanamu zao ni za fedha na dhahabu,

zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.

5115:5 Yer 10:5Zina vinywa, lakini haziwezi kusema,

zina macho, lakini haziwezi kuona;

6zina masikio, lakini haziwezi kusikia,

zina pua, lakini haziwezi kunusa;

7zina mikono, lakini haziwezi kupapasa,

zina miguu, lakini haziwezi kutembea;

wala koo zao haziwezi kutoa sauti.

8115:8 Za 135:18; Isa 44:9, 10; Yon 2:8; Hab 2:18Wale wanaozitengeneza watafanana nazo,

vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.

9115:9 Za 37:3; 62:8; 33:20; Mit 30:5Ee nyumba ya Israeli, mtumainini Bwana,

yeye ni msaada na ngao yao.

10115:10 Kut 30:30; Za 118:3; Mal 2:7Ee nyumba ya Aroni, mtumainini Bwana,

yeye ni msaada na ngao yao.

11115:11 Za 22:23; 103:11; 118:4Ninyi mnaomcha, mtumainini Bwana,

yeye ni msaada na ngao yao.

12115:12 1Nya 16:15; Mwa 12:2; Efe 1:3Bwana anatukumbuka na atatubariki:

ataibariki nyumba ya Israeli,

ataibariki nyumba ya Aroni,

13115:13 Za 24:4; 112:1; Law 26:3; Mit 10:6; Kum 11:27atawabariki wale wanaomcha Bwana,

wadogo kwa wakubwa.

14115:14 Kum 1:11Bwana na awawezeshe kuongezeka,

ninyi na watoto wenu.

15115:15 Mdo 14:15; Ufu 10:6; Za 96:5; Mwa 1:1; 14:19Mbarikiwe na Bwana

Muumba wa mbingu na dunia.

16115:16 Za 89:11; Mwa 1:28; 8:6-8Mbingu zilizo juu sana ni mali ya Bwana,

lakini dunia amempa mwanadamu.

17115:17 Za 88:10-12Sio wafu wanaomsifu Bwana,

wale washukao mahali pa kimya,115:17 Mahali pa kimya maana yake ni Kuzimu, yaani Sheol kwa Kiebrania.

18115:18 Za 111:1; 113:2; 28:6; 33:2; 105:1; 145:2; Dan 2:20bali ni sisi tunaomtukuza Bwana,

sasa na hata milele.

Msifuni Bwana.115:18 Msifuni Bwana ni Kiebrania Hallelu Yah.