Zaburi 114
Maajabu Ya Mungu Wakati Israeli Walipotoka Misri
1114:1 Kut 13:3; 29:46Wakati Israeli walipotoka Misri,
nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2114:2 Kut 15:17; Za 76:1; 78:68, 69Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu,
Israeli akawa milki yake.
3114:3 Kut 14:21; Za 77:16; Kut 15:8; Yos 3; 16Bahari ilitazama ikakimbia,
Yordani ulirudi nyuma,
4114:4 Amu 5:5milima ilirukaruka kama kondoo dume,
vilima kama wana-kondoo.
5114:5 Kut 14:21Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia,
nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume,
enyi vilima, kama wana-kondoo?
7114:7 Kut 15:14; 1Nya 16:30Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana,
mbele za Mungu wa Yakobo,
8114:8 Kut 17:6; Hes 20:11aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji,
mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.
Salmo 114
1Quando Israel saiu do Egito
e a casa de Jacó saiu do meio de um povo de língua estrangeira,
2Judá tornou-se o santuário de Deus;
Israel, o seu domínio.
3O mar olhou e fugiu,
o Jordão retrocedeu;
4os montes saltaram como carneiros;
as colinas, como cordeiros.
5Por que fugir, ó mar?
E você, Jordão, por que retroceder?
6Por que vocês saltaram como carneiros, ó montes?
E vocês, colinas, porque saltaram como cordeiros?
7Estremeça na presença do Soberano, ó terra,
na presença do Deus de Jacó!
8Ele fez da rocha um açude,
do rochedo uma fonte.